Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,928
- 30,279
Nimesoma kuhusu kifo cha Dr. Edith Kitambi leo keshafariki muda mrefu na watu wameandika kama kumbukumbu.
Kwangu mimi ikawa ni msiba mpya na machungu yake naomboleza wakati wenzangu weshapoa.
Nilimfahamu Edith University of Wales Cardiff mwaka wa 1991 sote tukiwa Postgraduate Students kutoka Tanzania.
Alinizoea zaidi alipojua kuwa mimi na Ledgar Tenga aliyekuwa mchezaji wa Yanga na Timu ya Taifa ni marafiki.
Tenga ni kaka yake.
Alikuwa bint mzuri wa tabia na sura.
Nakumbuka yeye ndiye aliyenipa jina la "Sheikh" pale Cardiff na likaniganda kiasi jina langu likafa na wanafunzi kutoka Tanzania wote wakawa wananiita, "Sheikh."
Ukisikia Sheikh basi hakuna mwengine ila mimi.
Sababu ya jina hili ni kuwa ilikuwa kila Jumamosi kuna mahali nadhani ilikuwa club wanafunzi wengi wakienda kucheza disco na kujiburudisha na vinywaji.
Cardiff ni mji mdogo sana ukifananisha na London na miji mingine ya Uingereza kama Liverpool hivyo hata sehemu za starehe si nyingi watu hukutana mahali pamoja siku zote.
Ikawa siku zinapita wanafunzi wenzangu hawanioni kujumuika na wao.
Ulaya kwa mgeni ni mahali pa upweke sana ingawa mimi nilikuwa nimeshafika Uingereza kabla na napaelewa kwa kiasi kidogo.
Siku moja Edith akaniuliza kulikoni?
Nikistarehe sana kuzungumza na Edith sababu yeye tofauti na wengine wote alikuwa akisema Kiswahili kwa "accent" ya Dar es Salaam kabisa, utasema mwanamke wa Kizaramo wa Kariakoo.
Nilipata kumuuliza imekuwaje akaniambia kuwa yeye lau ni Mchagga lakini kazaliwa na kukulia Dar-es-Salaam.
Ikawa sasa hata tukiwa na party za Watanzania 9 Desemba au Sabasaba hanioni kucheza muziki na Edith akitaka kuninyanyua kucheza namtuliza kwa kumwambia Sheikh hachezi dansi.
Yeye akiishia kucheka.
Na Edith akifanya hivi kwa kutumwa na wenzake ili wapate kucheka kwa kumuona sheikh anamwagika kwenye "dance floor."
Miaka ile kulikuwa na bendi kutoka Kenya, "Virunga," "Mazembe" ambazo miziki yake ikipendwa na kuvuma hadi Ulaya katika jumuiya za watu weusi.
Nakumbuka hawa Virunga walipata kufika Cardiff na wanafunzi kutoka Kenya wakawa wanauza tiketi za dansi.
Kulikuwa katika party zile muziki wa Judy Baucher sina hakika na hili jina yeye alikuwa na nyimbo za "blues" hizi zikiwatoa fahamu vijana wengi khasa mashairi yake ya mapenzi.
Nyimbo hizi zilikuwa lazima zipigwe.
Party za Watanzania zikinoga sana.
Vijana wa Kizungu walikuwa haziwapiti wakiwapenda sana dada zetu zaidi wanavyojua kucheza.
Ulaya ukialikwa party unakwenda na kinywaji chako.
Edith masikini akipenda kunitania nami siku zote nikimchekesha kwa kumwambia mie mzee na sheikh siwezi kucheza muziki afanye staha.
Tukazoeana sana nikawa nimepata pia daktari kidogo nikijisikia namwendea.
Edith alikuwa anafanya shahada ya pili katika Public Health.
Nakumbuka alipata kuniambia kuwa kwa tatizo nililokuwanalo la tumbo atanitibia kwa njia ya "food elimination," na akaniwekea orodha ya kutokula vyakula fulani kimoja baada ya kingine kwa muda mfupi niangalie tatizo langu kama litaendelea au la.
Nilipona.
Alipata siku moja kunipa mhadhara mzima wa ukimwi.
Akaniambia ni tabu mtu kupata ukimwi akiwa kajituliza lakini ni rahisi kuugua akiwa kinyume chake.
Akanieleza kuwa yeye katibia wagonjwa wengi na hili kaligundua kutokana na utafiti wake katika "lifestyles."
Nilimwacha Dr. Edith Kitambi Cardiff lakini nilipata kurudi tena Uingereza, London kwa muda mfupi nilimtembelea nyumbani kwake.
Baada ya hapo sikupata taarifa zake hadi leo zaidi ya miaka 30 kupita nasikia amefariki.
Nitaingia Maktaba kuangalia picha za Cardiff nikipata picha yake In Shaa Allah nitaiweka hapa.
Kwangu mimi ikawa ni msiba mpya na machungu yake naomboleza wakati wenzangu weshapoa.
Nilimfahamu Edith University of Wales Cardiff mwaka wa 1991 sote tukiwa Postgraduate Students kutoka Tanzania.
Alinizoea zaidi alipojua kuwa mimi na Ledgar Tenga aliyekuwa mchezaji wa Yanga na Timu ya Taifa ni marafiki.
Tenga ni kaka yake.
Alikuwa bint mzuri wa tabia na sura.
Nakumbuka yeye ndiye aliyenipa jina la "Sheikh" pale Cardiff na likaniganda kiasi jina langu likafa na wanafunzi kutoka Tanzania wote wakawa wananiita, "Sheikh."
Ukisikia Sheikh basi hakuna mwengine ila mimi.
Sababu ya jina hili ni kuwa ilikuwa kila Jumamosi kuna mahali nadhani ilikuwa club wanafunzi wengi wakienda kucheza disco na kujiburudisha na vinywaji.
Cardiff ni mji mdogo sana ukifananisha na London na miji mingine ya Uingereza kama Liverpool hivyo hata sehemu za starehe si nyingi watu hukutana mahali pamoja siku zote.
Ikawa siku zinapita wanafunzi wenzangu hawanioni kujumuika na wao.
Ulaya kwa mgeni ni mahali pa upweke sana ingawa mimi nilikuwa nimeshafika Uingereza kabla na napaelewa kwa kiasi kidogo.
Siku moja Edith akaniuliza kulikoni?
Nikistarehe sana kuzungumza na Edith sababu yeye tofauti na wengine wote alikuwa akisema Kiswahili kwa "accent" ya Dar es Salaam kabisa, utasema mwanamke wa Kizaramo wa Kariakoo.
Nilipata kumuuliza imekuwaje akaniambia kuwa yeye lau ni Mchagga lakini kazaliwa na kukulia Dar-es-Salaam.
Ikawa sasa hata tukiwa na party za Watanzania 9 Desemba au Sabasaba hanioni kucheza muziki na Edith akitaka kuninyanyua kucheza namtuliza kwa kumwambia Sheikh hachezi dansi.
Yeye akiishia kucheka.
Na Edith akifanya hivi kwa kutumwa na wenzake ili wapate kucheka kwa kumuona sheikh anamwagika kwenye "dance floor."
Miaka ile kulikuwa na bendi kutoka Kenya, "Virunga," "Mazembe" ambazo miziki yake ikipendwa na kuvuma hadi Ulaya katika jumuiya za watu weusi.
Nakumbuka hawa Virunga walipata kufika Cardiff na wanafunzi kutoka Kenya wakawa wanauza tiketi za dansi.
Kulikuwa katika party zile muziki wa Judy Baucher sina hakika na hili jina yeye alikuwa na nyimbo za "blues" hizi zikiwatoa fahamu vijana wengi khasa mashairi yake ya mapenzi.
Nyimbo hizi zilikuwa lazima zipigwe.
Party za Watanzania zikinoga sana.
Vijana wa Kizungu walikuwa haziwapiti wakiwapenda sana dada zetu zaidi wanavyojua kucheza.
Ulaya ukialikwa party unakwenda na kinywaji chako.
Edith masikini akipenda kunitania nami siku zote nikimchekesha kwa kumwambia mie mzee na sheikh siwezi kucheza muziki afanye staha.
Tukazoeana sana nikawa nimepata pia daktari kidogo nikijisikia namwendea.
Edith alikuwa anafanya shahada ya pili katika Public Health.
Nakumbuka alipata kuniambia kuwa kwa tatizo nililokuwanalo la tumbo atanitibia kwa njia ya "food elimination," na akaniwekea orodha ya kutokula vyakula fulani kimoja baada ya kingine kwa muda mfupi niangalie tatizo langu kama litaendelea au la.
Nilipona.
Alipata siku moja kunipa mhadhara mzima wa ukimwi.
Akaniambia ni tabu mtu kupata ukimwi akiwa kajituliza lakini ni rahisi kuugua akiwa kinyume chake.
Akanieleza kuwa yeye katibia wagonjwa wengi na hili kaligundua kutokana na utafiti wake katika "lifestyles."
Nilimwacha Dr. Edith Kitambi Cardiff lakini nilipata kurudi tena Uingereza, London kwa muda mfupi nilimtembelea nyumbani kwake.
Baada ya hapo sikupata taarifa zake hadi leo zaidi ya miaka 30 kupita nasikia amefariki.
Nitaingia Maktaba kuangalia picha za Cardiff nikipata picha yake In Shaa Allah nitaiweka hapa.
Kulia Mwandishi na anefuatia ni Dr. Edith Kitambi