The Informer
Senior Member
- Jun 14, 2010
- 119
- 29
Asalaam Aleykum,
Taarifa nilizokuwa nazo ni kuwa Chama Cha Mapinduzi kimeunda kamati
ya propaganda kwenye kampeni za uchaguzi inayo ongozwa na PRINCE BAGENDA
akisaidiwa na MUHINGO RWEYEMAMU.
Kamati hii ndiyo inayofanya kazi za kumchafua Dk. Willibrod Slaa kupitia magazeti na waandishi walionunuliwa na CCM.
Magazeti haya yakiandika habari za ndoa ya Slaa au taarifa zozote za uzushi, basi hununuliwa nakala zote na CCM na kugawiwa bure kwenye mikutano ya chama hiko.
Pia, CCM imekuwa inaongoza kwa kutoa rushwa kwa waandishi wa habari kwenye kampeni zao. Posho ambayo CCM inatoa kwa waandishi wa habari kwenye kampeni zao ni zaidi ya mara mbili ya posho inayotolewa na vyama vya upinzani.
Vifuatavyo ni viwango vya posho (daily allowances) ambazo timu za wagombea wa Urais zinatoa kwa waandishi wa habari:
1. Jakaya Kikwete (100,000/-)
2. Dk. Willibrod Slaa (45,000/-)
3. Prof. Ibrahim Lipumba (40,000/-)
Waandishi wa habari wote sasa hivi wanakimbilia kuwepo kwenye timu ya kampeni ya Kikwete kwani huko ndiko kwenye pesa nyingi. Wanalipwa milioni 1 kwa siku 10 tu.
Hii ndiyo maana kuwa wamekuwa wakitumwa na CCM kuandika habari za kumpamba JK na mwandishi anayeandika habari tofauti na matakwa ya CCM anatimuliwa kwenye posho.
Kulipwa posho kwa waandishi na vyama vya siasa ni kinyume kabisa na maadili ya uandishi wa habari na ni ishara kuwa waandishi, wahariri na wamiliki wa vyombo vya habari Tanzania wananunulika kirahisi.
Taarifa nilizokuwa nazo ni kuwa Chama Cha Mapinduzi kimeunda kamati
ya propaganda kwenye kampeni za uchaguzi inayo ongozwa na PRINCE BAGENDA
akisaidiwa na MUHINGO RWEYEMAMU.
Kamati hii ndiyo inayofanya kazi za kumchafua Dk. Willibrod Slaa kupitia magazeti na waandishi walionunuliwa na CCM.
Magazeti haya yakiandika habari za ndoa ya Slaa au taarifa zozote za uzushi, basi hununuliwa nakala zote na CCM na kugawiwa bure kwenye mikutano ya chama hiko.
Pia, CCM imekuwa inaongoza kwa kutoa rushwa kwa waandishi wa habari kwenye kampeni zao. Posho ambayo CCM inatoa kwa waandishi wa habari kwenye kampeni zao ni zaidi ya mara mbili ya posho inayotolewa na vyama vya upinzani.
Vifuatavyo ni viwango vya posho (daily allowances) ambazo timu za wagombea wa Urais zinatoa kwa waandishi wa habari:
1. Jakaya Kikwete (100,000/-)
2. Dk. Willibrod Slaa (45,000/-)
3. Prof. Ibrahim Lipumba (40,000/-)
Waandishi wa habari wote sasa hivi wanakimbilia kuwepo kwenye timu ya kampeni ya Kikwete kwani huko ndiko kwenye pesa nyingi. Wanalipwa milioni 1 kwa siku 10 tu.
Hii ndiyo maana kuwa wamekuwa wakitumwa na CCM kuandika habari za kumpamba JK na mwandishi anayeandika habari tofauti na matakwa ya CCM anatimuliwa kwenye posho.
Kulipwa posho kwa waandishi na vyama vya siasa ni kinyume kabisa na maadili ya uandishi wa habari na ni ishara kuwa waandishi, wahariri na wamiliki wa vyombo vya habari Tanzania wananunulika kirahisi.