Tanzania Yapoteza Askari Wake Watatu DRC CONGO

Tanzania Yapoteza Askari Wake Watatu DRC CONGO

SAVERA

Senior Member
Joined
Jun 25, 2013
Posts
114
Reaction score
43
Askari watatu walio kwenye kikosi cha kulinda amani huko DRC Congo,wamekufa kwa ajali jana jioni'
=========================================

Askari 3 wakulinda amani toka Tanzania wafariki Dunia katika ajali ya barabara katika mbuga ya wanyama pori la Virunga na wengi wawili wakijeruhiwa vibaya sana.

Askari hao waliokuwa katika kikosi maalumu cha UN walikuwa wakitoka BENI kuelekea Goma huko Kivu kaskazini. Miili ya askari hao imewasili kunako uwanja wa ndege wa Goma
10615993_758240744218262_4964285106085451455_n.jpg

Askari wa tanzania waliofariki Dunia kupitia ajali ya barabara huko mashariki mwa Congo wapelekwa kwao nyumbani.

Askari hao watatu walikuwa katika kikosi maalum cha UN kinacho saidi jeshi la Congo FARDC kuyapokonya silaha makundi ya wapiganaji mashariki mwa nchi hiyo hasa eneo la Beni.

Chanzo: VOA
 
Ajali neno pana sana haswa katika mazingira hayo!!!!

Hebu weka kitu kamili
 
Leta chanzo cha habari na chanzo cha ajari tufuatilie
 
ungesaidia pia, kama utaweza kupata na majina aisee, tuna marafiki zetu huko, maana wengine tunapoishi tumezungukwa na vikosi kama vi3.
 
R.I.P and condolences to their families. Sadly, they died in vain. Bring our boys back home, screw the DRC.
 
Askari watatu walio kwenye kikosi cha kulinda amani huko DRC Congo,wamekufa kwa ajali jana jioni'

Duh kuba kaka yangu huko kaenda huko nitapaje taarifa kamili maana napiga namba anayoitumia huko hapatikani
 
Innaa lillahi wainnaa ilayhi raaji'uun...Bwana ametoa na Bwana ametwaa, jina la mola lihidimiwe...Rest in peace...R.I.P...Allahumma ghfirlahum warhamhum waskinhum fil janna...Mwenyezimungu azilaze roho za marehem mahala pema peponi....AMINA!
 
Innaa lillahi wainnaa ilayhi raaji'uun...Bwana ametoa na Bwana ametwaa, jina la mola lihidimiwe...Rest in peace...R.I.P...Allahumma ghfirlahum warhamhum waskinhum fil janna...Mwenyezimungu azilaze roho za marehem mahala pema peponi....AMINA!
Khaaaaaa!
 
Kamanda akifa hakuna kulia ni kwa uzalendo wa taifa lake na afrika kwa ujumla.
 
Majeshi ya UN yako Congo kulinda Interest za USA kwa miaka mingi... Wakongoma hawafaidi utajiri wa madini yao bali mateso na mauaji ya kila aina; mabomu, risasi za moto, magonjwa ya kuambukiza, njaa ... Is it Worth Majeshi yetu kutumika kwa niaba yao? Kagame alitumika baadae akaanza kujigawia mwenyewe! Walimtumia M7 nae akawa anajigawia madini ... sisi Kama kawaida yetu ni watu wa kutekeleza TORs za Wakubwa wa Dunia hii kwa ujira wa Mwiha... R.I.P Vijana wetu...
 
Back
Top Bottom