Bilionea Asigwa
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 16,578
- 28,698
Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) wameingia mkataba wa kujenga bandari za nchi kavu katika nchi zote mbili.
Taarifa kutoka Tanzania zinasema DRC ndiye mtumiaji mkubwa wa Bandari ya Dar kuliko nchi zote majirani
Pia kumekuwa na ongezeko la mizigo inayokwenda Kongo inayopitia Bandari ya Dar kwa 180% ndani ya miaka minne, ambapo mizigo imeongezeka kutoka tani milioni 14 kwa mwaka mpaka tani milioni 28 kwa mwaka.
Kwa upande wa Tanzania, maeneo yaliyotengwa kwa ujenzi huo ni Kwala mkoani Pwani pamoja na Katosho mkoani Kigoma
Kwa upande wa Kongo maeneo yaliyotengwa ni Kasulambesa, Kasenga na Kalemie.
Ujenzi wa miradi hii utakamilika ndani ya miezi 18
Source: The Citizen