Mkuu
Allen Kilewella labda niweke senti moja kwa uchache. Kwanza, mleta mada kaleta mada nzuri tu inayotugusa kama Taifa na wananchi. Haya ndiyo mambo ya kujadili ingawa yanavurugwa makusudi
Mag3 alileta uzi 'kelele' zinavyotumika kuua hoja za msingi
Nikirudi kwenye mada, mletaji kasema nchi za viwanda ziliwekeza katika human capital
Hoja hii inaeleza kwanini ''viwanda'' tulivyokuwa navyo vichache vilikufa.
Hakuna postmortem wala utafiti wa kisayansi unaojibu hoja hiyo.
Ndipo tunakwenda katika hoja ya mleta mada nyingine
Research and Development: Hii inaeleza kwanini tunahitaji viwanda na kwasababu zipi, katika soko gani na tutawezaje kukabaliana na ushindani.
Pia inaeleza gharama za uzalishaji na jinsi ya kukabiliana na bidhaaza bei rahisi
Tatu, kuna suala la nishati.
Je tutaweza kuwa na nishati ya uhakika na nafuu itakayokidhi gharama za uendeshaji?
Kumbuka nishati ni factor kubwa katika kuamua gharama na uzalishaji
Ikiwa hatujaweza kusambaza gesi, kwa miaka 4 tutawezeshaje viwanda?
Nne, katika region integrations na globalization tutalindaje viwanda tarajiwa?
Kama tutafanya protectionism,tutaweza kumlinda consumer asiwe victim?
Hayo ni kwa uchache,yote yapo katika mwamvuli wa jambo muhimu tusilotaka kuliongelea ambalo ni Dira ya Taifa.
Dira na sera ni vitu viwili tofauti. Hapa tunaongelea vision na policy, na kwamba sera lazima zi reflect dira irrespective ya nani au chama gani kinakuwa madarakani
Wanatuambia wameandika sera ya viwanda ni kwa kutumia dira gani?
Tulikuwa na elimu kwa wote, ikaja kilimo kwanza na kuua sera ya elimu.
Ghafla kama walivyosema wachangiaji wengine BRN na sasa sera za viwanda.
Policy hizi zina reflect dira gani ya Taifa?
Pengine kushindwa kwa viwanda kutatokana na mambo mengi, kubwa ni siasa.
Tatizo letu ni kutokaa pamoja kama Taifa na kupanga kisha kuchagua tunataka nini.
Hatuna hamasa ya kujifunza kutokana na makosa yetu (retrospective) na tunaendesha mambo kisiasa kuliko utaalamu.
Tungerafuta kwanza, kwanini Tanganyika packers, Mutex, Mwatex, Mgololo, Kilimanjaro match box, Tanalec, General tyre, Moshi machine, Mangula Machine, Moro polyester, Morproco n.k. n.k. vilikufa tukipata jibu tuanzie hapo
Je, hatuna pamba ya kutosha, hatuna wavaaji wa kutosha, hatuna magari ya kutosha, hatuhitaji vipuri n.k.
Jibu rahisi ni ndiyo kama ni hivyo tulifeli wapi na je sababu za kufeli tumezibaini na kuziondoa?