Tanzania ya miaka ya 1980

Tanzania ya miaka ya 1980

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
3,621
Reaction score
6,512
Tanzania ya miaka ya 60, 70, 90 na kuendelea ina kumbukumbu nyingi ambazo nyingi tunaziongelea katika mazungumzo yetu ya kila siku kila tunapozungumza mambo ya siasa, uchumi, kijamii na historia yetu kwa ujumla.

Ila kwa muda nimegundua kuna uhaba wa mazungumzo na kumbukumbu za kutosha kuhusu kipindi cha miaka ya 80. Najua kilikuwa ni kipindi kilichokuwa na changamoto na pilikapilika nyingi, mfano hali ya kisiasa huko Zanzibar, mwisho wa vita vya Kagera na changamoto zake, kung'atuka kwa Mwalimu nk. Ila naona bado sipati picha kamili ya hali ya kijamii ilivyokuwa kiujumla hapa Tanzania.

Nikiongezea, naweza kusema muongo ule wa 1980 inawezekana ndiyo umetoa athari kubwa zaidi (nzuri na mbaya) za kisiasa, kiuchumi na kijamii tulizonazo leo hii.

Wahenga embu mtujuze basi.
 
la Kipindi kile nchi ilikua mbele kimaendeleo kuliko sasa!Ajira zilikuwepo angalau,viwanda vingi nchi nzima railway ilikua na ufanisi mkubwa,mashirika ya umma yalimea mf NMC,RTC, nk,Hatukulipia huduma za matibabu hosp ilikua bure!elimu ilikua bora zaidi shule za government...faftari,kalamu bure!
 
Majibu yanayotofautiana ninayopata mpaka sasa yanadhihirisha kwamba ni kipindi ambacho ni mystery sana kwenye kumbukumbu zetu. Hivi hii ni kwa makusudi au?
 
Miaka ya 80 filamu za Kihindi zilikuwa maarufu sana.

Baadhi ya wacheza filamu nyota wa kipindi hicho, kama Mithun Chakraborty, kwa mfano, walikuwa wanakuja hadi Tanzania.

Pia ni miaka ambayo mitindo ya nywele kama 'shegi' na 'panki' ilivuma sana.

Na kama sijakosea, madawa ya kubadilisha nywele [kali kiti - curl kit] ndo yaliingia nchini.
 
Miaka ya 80 filamu za Kihindi zilikuwa maarufu sana.

Baadhi ya wacheza filamu nyota wa kipindi hicho, kama Mithun Chakraborty, kwa mfano, walikuwa wanakuja hadi Tanzania.

Pia ni miaka ambayo mitindo ya nywele kama 'shegi' na 'panki' ilivuma sana.

Na kama sijakosea, madawa ya kubadilisha nywele [kali kiti - curl kit] ndo yaliingia nchini.
Raizon na bwanga (bana juu achia chini ndio kipindi chake) ,pia ndio kipindi cassete za vhs ziliingia
 
Baada ya vita ya Kagera.Kulikuwa na msemo wa miazi 18
Ya uvumilivu.Kila Jumatatu na Jumatano tunakwenda duka la ushirika(baada ya kuchukua bidhaa RTC) tunapiga foleni ndefu ya Unga wa Yanga(manjano) mafuta ya kupikia na sukari.Shule nyingi zilikuwa za kulipia serikali ikazi fanya bure.Mabasi ya railway na ya kamata ndio usafiri.Pamoja na yote hayo Tanzania ilikuwa nzuri.Tulikuwa hatujali TV maana hakuna.Simu inabidi uende kwa jirani(waringaji wakubwa na simu zao) au uende posta unaingizwa kwenye (call box) Duh tumetoka mbali.Dar,Mwanza,Tanga na Arusha zilikuwa safiiiiiiii
Na ukifika katika Hiyo miji lazima uripoti kwa mjumbe wa nyumba kumi.
 
Tanzania ya miaka ya 60, 70, 90 na kuendelea ina kumbukumbu nyingi ambazo nyingi tunaziongelea katika mazungumzo yetu ya kila siku kila tunapozungumza mambo ya siasa, uchumi, kijamii na historia yetu kwa ujumla.

Ila kwa muda nimegundua kuna uhaba wa mazungumzo na kumbukumbu za kutosha kuhusu kipindi cha miaka ya 80. Najua kilikuwa ni kipindi kilichokuwa na changamoto na pilikapilika nyingi, mfano hali ya kisiasa huko Zanzibar, mwisho wa vita vya Kagera na changamoto zake, kung'atuka kwa Mwalimu nk. Ila naona bado sipati picha kamili ya hali ya kijamii ilivyokuwa kiujumla hapa Tanzania.

Nikiongezea, naweza kusema muongo ule wa 1980 inawezekana ndiyo umetoa athari kubwa zaidi (nzuri na mbaya) za kisiasa, kiuchumi na kijamii tulizonazo leo hii.

Wahenga embu mtujuze basi.
Vijana wa hapo jijini Dar miongoni pamoja na wengineo ni Lemutuz na mh Mbowe. Pia Bonnie Love.
cc Mkandara
 
Miaka ya 80 filamu za Kihindi zilikuwa maarufu sana.

Baadhi ya wacheza filamu nyota wa kipindi hicho, kama Mithun Chakraborty, kwa mfano, walikuwa wanakuja hadi Tanzania.

Pia ni miaka ambayo mitindo ya nywele kama 'shegi' na 'panki' ilivuma sana.

Na kama sijakosea, madawa ya kubadilisha nywele [kali kiti - curl kit] ndo yaliingia nchini.
Bila kusahau break dance shebedoo na boogaloo ndio walikuwa wakali wa kalikiti, kwetu hapo utamkuta black Moses, blood Moses, queen tiffa. Digadiga. ,Kelly jhon sammy cool hawa wote uzao wa kwa macheni
 
Tanzania ya miaka ya 60, 70, 90 na kuendelea ina kumbukumbu nyingi ambazo nyingi tunaziongelea katika mazungumzo yetu ya kila siku kila tunapozungumza mambo ya siasa, uchumi, kijamii na historia yetu kwa ujumla.

Ila kwa muda nimegundua kuna uhaba wa mazungumzo na kumbukumbu za kutosha kuhusu kipindi cha miaka ya 80. Najua kilikuwa ni kipindi kilichokuwa na changamoto na pilikapilika nyingi, mfano hali ya kisiasa huko Zanzibar, mwisho wa vita vya Kagera na changamoto zake, kung'atuka kwa Mwalimu nk. Ila naona bado sipati picha kamili ya hali ya kijamii ilivyokuwa kiujumla hapa Tanzania.

Nikiongezea, naweza kusema muongo ule wa 1980 inawezekana ndiyo umetoa athari kubwa zaidi (nzuri na mbaya) za kisiasa, kiuchumi na kijamii tulizonazo leo hii.

Wahenga embu mtujuze basi.
And i $=5Tz ndiyo sababu kuna kitu naitwa dala dala.

Miaka ya 80 kabla ya vita ya Kagera pamoja na matatizo ya JON uchumi ilikuwa very strong.Kama Taifa ilimiliki viwanda vingi.Wakati Me into anatoa madarakani $=250 of not 100.

Baada ya kuingia Mkapa pamoja n.a. kuu a viwanda na Bank ya BBC $=1200,hivyo majambazi ya Raslimali zetu yalianzia hasa kipindi cha Mkapa ambaye mpaka leo kodi zetu ndizo zinamlisha,zinamnyeshwa na Kumvisha.

Wakati wa tawala ga Mkapa ndipo Watawala lea ulafi walijilimbikizia Mali kupindukia.Ni aibu leo Mkapa kiwatukana wapinzani wakati yeye ndiyo chanzo cha kuuza Raslimali zetu.
 
Majibu yanayotofautiana ninayopata mpaka sasa yanadhihirisha kwamba ni kipindi ambacho ni mystery sana kwenye kumbukumbu zetu. Hivi hii ni kwa makusudi au?

hakukuwa na uongozi, kila mmoja ndo akaanza kujiangalia yeye na familia yake

ni miaka ya akina sokoine kupotezwa

Ni miaka udsm walikuwa fearless

Ni miaka njaa ili strike

mabasi mazuri ya carrier juu yakaingia

miziki ya dansi, kikongo, afrika kusini(kurukun)

watu wakaanza kununua gari kwa wingi, UDA ndio ikawa inajifia na taratibu chai maharage sikaanza kuingia


mystery kwa sababu:TAIFA LIKAANZA KUPOTEA NA KUHAMIA KWA MTU MMOJA MMOJA....dhana ya nchi ilifia miaka hiyo...hakukuwa na kiongozi pale juu....mwinyi hakupaswa kufuata baada ya nyerere alitakiwa awe salim,jumbe..warioba,...msuya....


ukabila ukaanza kushika kasi kimya kimya....katika mashirika mbalimbali


tuendelee
 
Nakumbuka uhaba wa sukari ulipelekea tunywe chai iliyotiwa sukari-guru au wakati mwingine tunatwanga miwa tunakamua juisi inachemshwa hadi inakuwa nzito kama asali badae inatumika kama sukari
 
Kuna watu humu wametoa vitu adimu sana!!
Inaonekana mzimu wa wakati wa wahujumu uchumi imerudi tena na tofauti ya wakati ule na sasa ni kuwa uchumi ulikuwa juu 1$=200shs . Uzalishaji ulikuwa juu, tulikuwa na mashamba makubwa ya mkonge, kahawa,pamba, karafuu n.k

Je kwa sasa na hali hii ya uchumi na uzalishaji umepungua tutafika?
Kwa nyakati kama hizi za miaka ya sasa kilimo ni kelele tu! Hata kilimo cha mazao ya chakula ni shida achilia mbali mazao ya biashara.
Nchi yingi Dunian zilizo pata mabadiliko makubwa ya uchumi yalipitia kwenye kilimo. Ili uwe na viwanda vingi lazima ulime uchakate na kufanya parking.
Nchi ya viwanda malighafi!!!? Kabda tusage kokoto!
Tuangalie America na china! Kilimo ndio kilicho waweka uchumi juu! Alafu technology insfuata yenywe kama uchumi uko powa.
 
Safi sana. Nashukuru kwa michango yenu. Cha kushangaza zaidi ni kwamba kama baadhi walivyosema, ni miaka ya dhana ya ubinafsi (individuality) kuibuka. Hii ni kinyume kabisa na muongo wa nyuma yake, miaka ya 70, ambayo kwa tathmini yangu ndiyo muda ambao Tanzania ilikuwa kileleni kama taifa. Tulikuwa tunapambana pamoja na tunazungumza lugha moja. Ukiangalia sifa nyingi Tanzania tulizokuwa tunapewa, ni jinsi tulivyokuwa kama taifa miaka ya 70.

Naweza hata kuiunganisha miaka ya 80 na uibukaji wa vipaji vya hali ya juu mbalimbali kama baadhi wanavyosema, kuanzia kwenye muziki, ndondi, riadha, mpira wa miguu (kina Kibadeni na Pondamali si ni wa miaka hiyo?). Nadhani ni kwa sababu kila mtu ilibidi aanze kujiangalia mwenyewe ili kusurvive.

Inaonyesha hii dhana ya 'pambana na hali yako' iliibukia miaka ya 80.
 
MiaKa hiyo vyuma vilikaza kuliko Hali ilivyokuwa sasa Mpumbavu wa wakati huo Kichaa chake kikampanda akaanzisha 'Uhujumu uchumi' kutesa na kufilisi Watu Kama afanyavyo Kichaa wa sasa japo juhudi hizo hazukumsaidia chochote 'Mnyonge' aliekuwa anatetea asihujumiwe
We Pohamba ni lini umeinyalandu CCM?...... Lugha yako haieleweki nowdays!!
 
Nakumbuka uhaba wa sukari ulipelekea tunywe chai iliyotiwa sukari-guru au wakati mwingine tunatwanga miwa tunakamua juisi inachemshwa hadi inakuwa nzito kama asali badae inatumika kama sukari
Sabuni za majani ya mpapai, unga wa njano na ule wa mtama ilikuwa kawaida sana!
 
Back
Top Bottom