Tanzania ya miaka ya 1980

Tanzania ya miaka ya 1980

Ukisema miaka ya 80 ndio Turn point ya Tanzania ilipoanza
Kuteka ndege ya ATC na akina Member Lee kutoka Mwanza hadi Uingereza wakidai Nyerere ajiuzuru
Vita ya hujumu uchumi kuna wahindi walimwaga pesa barabarani.
Kufukuzwa kazi makamu wa kwanza wa raisi Jumbe na kuvuliwa hadhi zote hadi akawekwa under house arrest.
Kifo cha Waziri Mkuu Sokoine kilishtua umma,ili kupoza hasira za wananchi Nyerere akamteua Salim Mohamed Salim kuwa Waziri Mkuu.
Uncle Tom alikula njama na maofisa wa jeshi kumpindua raisi Nyerere,lakini jaribio lilizimwa na watu kadhaa kukamatwa,Commando Tamimu aliepanga kumua Nyerere alipigwa risasi na kachero Mabele Marando.
Nyerere alingatuka chini ya shindikizo za nje na ndani mwaka 1985.Mwinyi akachguuliwa raisi wa Tanzania.
Wimbi la vijana kwenda ng'ambo lilishamiri katika kipindi hiki.
 
Ukisema miaka ya 80 ndio Turn point ya Tanzania ilipoanza
Kuteka ndege ya ATC na akina Member Lee kutoka Mwanza hadi Uingereza wakidai Nyerere ajiuzuru
Vita ya hujumu uchumi kuna wahindi walimwaga pesa barabarani.
Kufukuzwa kazi makamu wa kwanza wa raisi Jumbe na kuvuliwa hadhi zote hadi akawekwa under house arrest.
Kifo cha Waziri Mkuu Sokoine kilishtua umma,ili kupoza hasira za wananchi Nyerere akamteua Salim Mohamed Salim kuwa Waziri Mkuu.
Uncle Tom alikula njama na maofisa wa jeshi kumpindua raisi Nyerere,lakini jaribio lilizimwa na watu kadhaa kukamatwa,Commando Tamimu aliepanga kumua Nyerere alipigwa risasi na kachero Mabele Marando.
Nyerere alingatuka chini ya shindikizo za nje na ndani mwaka 1985.Mwinyi akachguuliwa raisi wa Tanzania.
Mabere Malando na shahidi X pia alitoa ushahidi
 
Wimbi la vijana kwenda ng'ambo lilishamiri katika kipindi hiki.
'Stole away'.
Nna jamaa zangu wawili walikwenda kudandia meli Maputo, mmoja alidakwa mpakani (Mtwara) akarudishwa na mwingine alienda mpaka Italy lakini na yeye wakamrudisha.
 
Mungu atuweke hai na sisi tutakuja kusimulia enzi hii kwa kwa wajukuu maana huyu Makufuli sio wa kusahau
 
Miaka ya 80 filamu za Kihindi zilikuwa maarufu sana.

Baadhi ya wacheza filamu nyota wa kipindi hicho, kama Mithun Chakraborty, kwa mfano, walikuwa wanakuja hadi Tanzania.

Pia ni miaka ambayo mitindo ya nywele kama 'shegi' na 'panki' ilivuma sana.

Na kama sijakosea, madawa ya kubadilisha nywele [kali kiti - curl kit] ndo yaliingia nchini.
Miaka ya 80 mazao yalikuwa yanaota kwa lengo la kulisha watu, lakini baada ya laana ya watawala sasa mazao yanaota kwa ajiri ya mbegu ili ihifadhi kizazi chake.
 
80s pamoja na kuwa tulitoka Vitani Tukakaza Mikanda,maduka ya Kaya,Uhujumu uchumi nk.
Tanzania ndio tulikuwa tumefika mahali pazuri Kiviwanda kwani Mashirika mengi ya Umma yalikuwa yako imara na viwanda alivyojenga Mwl ndio vilikuwa kwenye pick!

Miaka hiyo watumishi waliofanya kazi kwenye Mashirika ya Umma(SU) na vyama vya Ushirika ndio waliokuwa wanaheshimika kwa kuwa na kupato kikubwa wafatie watumishi wa Chama na Serikali..

Ajira kama Ualimu,Police,Jeshi,Mahakama zilidharauliwa sana na ndilo lililopelekea mwanzoni mwa 90s, baadhi ya idara kama Police,Mahakama na Magereza, na Mamlaka ya Kodi(TRA) kuwa na baadhi ya watumishi walioingia kwenye rushwa wakirubuniwa na hao wengine na wafanyabiashara hasa wale wa Kiasia na waarabu walioshika biashara wakati ule.

Mwl. Alipigia kelele sana hali akisisitiza kuwa "Rushwa ni hatari sana kwani ikishaingia ni vugumu kutoka"

Miaka ya 90s baada ya rushwa kuingia na kuwa na watumishi wa Mashirika ya Umma walioshirikiana na wafanyabiashara na baadhi ya Viongozi wasio waaminifu, ndipo ilipotokea muanguko wa Mashirika mengi sana na baadaye tulipolazimishwa kuingia kwenye privatization ndip ikapelekea kuua viwanda vyetu vingi.

Anachokifanya Raisi wetu Magufuli, wengi wanakielewa ama wanakataa kukubali kukielewa.
Huyu anavunja na kuondoa biashara zinazotoka nje ambazo malighafi zake au rasilimali zake tunazo, na kualika wawejezaji wa ndani na nje kuwekeza katika kuganya production ya bidhaa hizo hapa nchini ili hatimaye na sisi tuzipate hapanhapa kwa bei nafuu na pia Wafanya biashara wa ndani na nje wazichukue na kufanya exports.

Haya hayaji miraculous kwamba leo kesho tayari, ni lazima kuharibike kitu, halafu kujengwe kitu ndio mavuno yaje. Hivyo tuchangamkie na kutafuta mapya ya fursa zijazo na tusipayuke tukiacha wajanja wanakamata hizo fursa zilizopo na zijazo huku wakiturubuni na kutupotosha tubaki watumwa wao baadaye.


Mradi wa trilioni 3 wasajiliwa nchini, kutoa ajira 4500
Vitu kama hivi alichoppst Trump2 ndivyo tungekuwa tunachangamkia kutafuta kujua mbali ya ajira vina fursa gani zingine , na kisha mchanhamkie au muwapeleke ndugu wasio na ajira au wenye mitaji wafanye biashara nk. badala ya kukaa na kuponda .

Angalieni wenzetu wa Jukwaa la Kenya humu JF , mbali ya Politics zaidi wanalitumia kuhabarishana fursa za biashara na uchumi na nyingi zikiwa ni za hapa kwetu. Sisi habari hiyo hiyo tutangoja kina Zito waseme na wasiposema inakuwa sio habari, kibaya ikiletwa kwenye mjadala itapondwa na kupuuziwa huku wapuuzaji wengi ni wale hohehahe wasio na lolote.
Vijana amkeni
 
Aisee umenikumbusha enzi zile unaenda na kitabu chako cha ration dukani kila baada ya wiki mbili kununua sukari .
Operesheni Nguvu kazi...nakumbuka polisi walikuwa wanakuja wamevaa kiraia na kama wanapiga tizi (jogging) ..halafu inapigwa filimbi wanatawanyika na wanaanza kamata watu...
Bila ya kusahau jamaa wa mali ya sili Walikuwa wanakuja na migobole mijini hasa Dodoma na kuwapiga risasi mbwa wazuzuraji.
 
Dah....umenikumbusha mbali sana...chozi limenidondoka
 
Back
Top Bottom