Tanzania tuache kuadhimisha sherehe za Uhuru na Muungano kila mwaka na pia tufute kabisa mbio za mwenge

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,371
Kutokana na ukweli kwamba nchi hii ina matatizo mengi yanayotokana na ukosefu wa fedha na kuwa na vipaumbele vibovu, nashauri tupitishe itakayotamka kuwa sherehe za uhuru na muungano zitakuwa zinafanyika kila baada ya miaka 2 au 3 na wakati huo huo tufute kab iisa mbio za mwenge na huu mwenge ukahifadhiwe makumbusho.

Badala yake utafutwe utaratibu mwingine wa kuadhimisha sherehe hizi kila mwaka tena ikibidi siku husika ziwe siku za kazi kama kawaida isipokuwa kwa mwaka huo wa 2 au 3 ndio iwe public holiday.

Labda tujiulize kuna logic gani ya kutumia mabilioni kudhimisha sherehe za uhuru wakati nchi haina vifaa vya uokozi wakati wa majanga?

Kuna logic gani ya kutenga mabilioni kila mwaka kwa ajili ya mbio za mwenge huku watoto wetu wanasoma katika shule za udongo zilizoezekwa kwa nyasi?

Je, hii ndio maana ya uhuru?

Bajeti ya sherehe za uhuru, muungano na kukimbiza mwenge kwa mwaka mmoja tu wa fedha, haiwezi kugharamia uanzishwaji wa Tanzania Disaster Management Agency?

Tumekosa viongozi wenye vision ya kututoa hapa tulipo na zaidi tumefeli kwa kiasi kikubwa mno katika swala zima la kupanga vipaumbele katika ngazi ya kitaifa, mikoa, wilaya, n.k.

Kwa kifupi tumekosa dira kama Taifa.
 
Unataka Kupokonya Ushindi Wa Chama Kwa Nguvu?
*-Utaweza?-*
Waelimishe Kwaza Wana Giningi (watanzania) Maana Tayari Walishalishwa Unga Wa Ndele.

Kwao Rangi Nyeupe Ni Nyeusi Na Nyeusi Ni Nyeupe!
 
Kutokana na ukweli kwamba nchi hii ina matatizo mengi yanayotokana na ukosefu wa fedha na kuwa na vipaumbele vibovu, nashauri tupitishe itakayotamka kuwa sherehe za uhuru na muungano zitakuwa zinafanyika kila baada ya miaka 2 au 3 na wakati huo huo tufute kab iisa mbio za mwenge na huu mwenge ukahifadhiwe makumbusho.

Badala yake utafutwe utaratibu mwingine wa kuadhimisha sherehe hizi kila mwaka tena ikibidi siku husika ziwe siku za kazi kama kawaida isipokuwa kwa mwaka huo wa 2 au 3 ndio iwe public holiday.

Labda tujiulize kuna logic gani ya kutumia mabilioni kudhimisha sherehe za uhuru wakati nchi haina vifaa vya uokozi wakati wa majanga?

Kuna logic gani ya kutenga mabilioni kila mwaka kwa ajili ya mbio za mwenge huku watoto wetu wanasoma katika shule za udongo zilizoezekwa kwa nyasi?

Je, hii ndio maana ya uhuru?

Bajeri ya sherehe za uhuru, muungano na kukimbiza mwenge kwa mwaka mmoja tu wa fedha, haiwezi kugharamia uanzishwaji wa Tanzania Disaster Management Agency?

Tumekosa viongozi wenye vision katika hi nchi na tumefeli kwa kiasi kikubwa mno katika swala zima la kupanga vipaumbele katika ngazi ya kitaifa, mikoa, wilaya, n.k.

Kwa kifupi tumekosa dira kama Taifa.
Kwakuwa kila mtu ana uhuru wa kujieleza mi naona sawa mawazo yako, ila NO sherehe za uhuru, muungano, mbio za mwenge, n.k ni muhimu na ni kumbukumbu ya urithi wetu wa kitaifa, na sherehe yenyewe ni mara moja kwa mwaka sio kila siku, wewe km hutaki kukumbuka siku uliyokombolewa ni wewe na familia yako, ila kitaifa ni urithi na alama na kumbukumbu kwa taifa la Tanzania.
 
Kwakuwa kila mtu ana uhuru wa kujieleza mi naona sawa mawazo yako, ila NO sherehe za uhuru, muungano, mbio za mwenge, n.k ni muhimu na ni kumbukumbu ya urithi wetu wa kitaifa, na sherehe yenyewe ni mara moja kwa mwaka sio kila siku, wewe km hutaki kukumbuka siku uliyokombolewa ni wewe na familia yako, ila kitaifa ni urithi na alama na kumbukumbu kwa taifa la Tanzania.
Kwani njia pekee ya kuadhimisha siku hizo ni hii ya kutumia mabilioni?
 
Back
Top Bottom