Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 123,593
- 234,219
Nimesikitishwa sana na mavazi (sare) ya viongozi mbalimbali waliohudhuria Uzinduzi wa kinachoitwa Mbio za Mwenge, kwa nchi masikini kama hii inayoomba omba kila mara kutumia hela za umma ili kushona sare za mwenge, ni jambo ambalo ni sawa na kituko, bad enough sasa sare zenyewe badala ya kuwekwa vivutio vya Nchi inawekwa picha ya Rais Samia!
Sasa ni hivi, ni lazima Wananchi waelezwe hizo sare ni za kazi gani na ziko ngapi na bei yake ni ipi na zimegharamiwa na nani? Na kama hamtaki kusema ukweli basi tutaingia kazini sisi wenyewe kuutafuta ukweli na kuuanika hadharani , Tusilaumiane !