Wanashangaza zaidi wananchi wanaowashabikia wakijua fika hakuna nchi hawa wamarekani wameivamia ikafanikiwa
Haifanikiwi Leo lakini miaka 50 ijayo watakua sio wenzetu wakati huo sisi ndio tutavurugana.
Mana Watu watakavyozidi kupata elimu na maarifa hawatakubali kutawaliwa kimaajabu badala ya sheria.
Hivi palikua na sababu gani ya kuwabeba na kuwavumilia Wakurugenzi na wasimamizi wa uchaguzi waliolalamikiwa tangu mwanzo kuwa wanakiuka sheria wazi za uchaguzi?
Tangu lini vyombo vya dola vikaingia kwenye chumba cha kupiga kura?
Wamarekani na wazungu wanatuona kuwa sisi wa Afrika ni watu waajabu sana kwa uovu ,ukatili ,ushenzi na hujuma tunazofanyiana kwa kugombania madaraka kwa sababu tu ya ubinafsia wa kugombania raisilimali zetu wenyewe.
Uchaguzi wa Marekani uko wazi dunia nzima na Lile ni Taifa kubwa sana lililoundwa na nchi 52 lakini limeendelea kuwa Taifa moja kwa sababu ya Uhuru na demokrasia.
Hata kama uchaguzi wao unakua na kasoro lakini hawakataniapanga ili kulazimisha MTU wa chama fulani ashinde.
Inajulikana wazi kuwa kuna ngome za Chama Fulani sehemu Fulani na hakuna siku serikali wanapeleka Majeshi huko ili chama kingine kishinde kwa nguvu.
Wanaacha upepo ubadilishwe na wapiga kura wenyewe. Hutasikia wakitisha watu kuwa msipomchagua Huyu tutawakatia umeme ,hatutawapa madawa hospitalini, hatutatoa fedha za kodi zenu kwa maendeleo yenu.
Huwezi kusikia mambo ya ajabu kama hayo yanayokiuka haki na Uhuru wa watu.
Sasa kwetu uchaguzi Mkuu wa Wilaya ambaye ni mwenyekiti wa Ulinzi na usalama wa Walaya anasimama hadharani na kusema Mimi sio Neutral ni lazima Chama changu kishinde.
Wasimamizi wa uchaguzi wanafanya mambo ya ajabu wazi kabisa ili auonekani kuwa anapigania CCM halafu Tume yenye watu weledi kabisa inaibuka na kuukaripia ubalozi wa Marekani.
Mambo mengine tuyafanye tukijua kuwa tunawafanyia binadamu wenzetu ambao hata wao wanataka kutendewa haki.
Watu wote wanalipa Kodi zao lakini wanapotaka kumchagua mwakilishi wao wa kwenda kutumikia kodi zao kwa ujira wa Ubunge au udiwani wanajitokeza watu wachache wanalazimisha kundi la chama chao na marafiki zao ndio pekee wafaidi kodi za wananchi.
Tume Tendeni haki hamutaiona Marekani ikiwasema.
Mmeapa kutenda Haki lakini mnakiuka kiapo chenu. Kumbukeni mnalipwa kwa jasho la wote sio la CCM pekee.Tena hao CCM mnao watetea ndio wenye uwezo wa hata kusamee kodi na kuwakosesha pesa za mishahara.
Watendeeni wengine haki.
Dunia haijawahi kuwaenzi watu wasiotenda haki