Tanzania na usafirishaji wa silaha maziwa makuu!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,483
40,008
karibu miaka miwili iliyopita katika kile ambacho kilijulikana kama "Sakata la Mapanki" kati ya vitu ambavyo Rais Kikwete alipinga ni kuhusika kwa Tanzania katika usambazaji wa silaha ndogondogo katika maeneo ya maziwa makuu na hivyo kuchochea vita. Katika hotuba yake ambayo iliungwa mkono baadaye na Bunge la Muungano Rais Kikwete alikataa kabisa kuwa Tanzania haihusiki na mambo hayo.

Ni wakati ule nilipoandika ripoti yangu ya kwanza kuhusu suala la silaha hizi ndogondogo (ripoti hii inapatikana kwenye makasha ya KLH News - Special Reports). Hata hivyo kuna habari mpya ambayo hatimaye inaweza kuwataja tena watu wale wale ambao tumekuwa tukiwasikia tena hasa baada ya mamluki na mfalme wa vita Victor Bout ambaye nilimtaja katika ripoti hiyo kutiwa mbaroni hivi karibuni na hivyo kuwafanya wauza silaha haramu wa eneo letu la maziwa makuu kuwa na matumbo joto.

Je Tanzania imeweza vipi kusimamisha baadhi ya viongozi wake na wananchi wake kujihusisha na udalali wa silaha za moto katika eneo letu la maziwa makuu? Je, hii ni kashfa nyingine ambayo inasubiri kutokea na hivyo kuthibitisha kile ambacho wengine tulikisema miaka miwili iliyopita?
 
Hii ni skendo mpya na itawapa wabunge wetu aibu nyingine ya kuikubaliana na kila hotuba ya kiongozi kama rais na waziri mkuu na kuifanya sehemu yao bila kufanya utafiti juu ya kilichomo kwenye ripoti husika.

Wiki mbili zilizopita nilikutana na watu wawili kutoka visiwa vya Seychelles na kwa kweli walikuwa wanatulaumu waziwazi kuwa tumekuwa sehemu ya kufanya biashara haramu na ama njioa ya kupitisha silaha ili kwenda kudstabilize nchi nyingine kwa faida ya mabwana zetu.

Lets wait and see hili nal;o ni bomu jingine, kuna siku hii serikali itajikuta inaanguka kutokana na hii miskendo ya kila siku kukicha.
 
Back
Top Bottom