NAPITA
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 5,077
- 2,249
Katika kikao cha Bunge kinachoendelea mjini Dodoma wakati wa kuchangia bajeti ya ofisi ya Waziri mkuu Mbunge Kangi Lugola aliibua hoja nzito ya kwamba yawezekana kuna baadhi ya Mawaziri wa serikali yake wanajiusisha na vitendo vya madawa ya kulevya maana toka Mkuu wa kitengo cha kuzuia na kupambana na Madawa ya kulevya Bw. Shekiondo kusema anayo majina ya vigogo wanaojiusisha na madawa hayo mpaka leo serikali imekaa kimiya.
Kitendo hicho kilisababisha Waziri Merry Nagu kusimama na kumtaka mh. mbunge kusibitisha kauli yake kwamba amesema kuna baadhi ya Mawaziri wanajiusisha na madawa ya kulevya ama afute kauli yake, maamuzi ya Spika ilikuwa ngoja wakaangalie kumbukumbu za Bunge zimerekodi nini.
Sasa tujiulize inawezekana ni kweli kuna Mawaziri wanausika na madawa haya?.
Na je, kama ikithibitika ni kweli amesema kuna Mawaziri wanajiusisha na madawa haya ya kulevya atakuwa tayari kuwataja kwa manufaa ya Taifa?
Kitendo hicho kilisababisha Waziri Merry Nagu kusimama na kumtaka mh. mbunge kusibitisha kauli yake kwamba amesema kuna baadhi ya Mawaziri wanajiusisha na madawa ya kulevya ama afute kauli yake, maamuzi ya Spika ilikuwa ngoja wakaangalie kumbukumbu za Bunge zimerekodi nini.
Sasa tujiulize inawezekana ni kweli kuna Mawaziri wanausika na madawa haya?.
Na je, kama ikithibitika ni kweli amesema kuna Mawaziri wanajiusisha na madawa haya ya kulevya atakuwa tayari kuwataja kwa manufaa ya Taifa?