Cicero
JF-Expert Member
- Jan 20, 2016
- 2,924
- 3,072
MWEEEH! Kama uongo vile. Mbona siiamini hii ripoti. Ngoja niwashushie data ntarudi baadae.
======
Inakadiriwa kuwa Mamilionea 499 kwa kiwango cha dola wamepungua nchini Kenya kutoka mwaka jana.
Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2020 shirika linalofuatilia kiwango cha utajiri binafsi wa watu (HNWI) , Wakenya sita pia walishuka kutoka kwenye kikundi cha watu matajiri sana wanaofahamika kama Ultra High Net- Super (YHBW1) wakiwa na zaidi ya shilingi bilioni 3, na hivyo kupunguza idadi yao na kufikia 42.
Ripoti hiyo imeeeleza kuwa jinsi uchumi wa Kenya ulivyo waumiza watu binafsi matajiri ambao kila mmoja wao alikua na zaidi ya shilingi milioni 100.
Mabadiliko haya yametokea katika mwaka ambao Kenya imepitia kipindi kigumu cha uchumi, ambacho kilisababisha kushuka kwa faida katika kampuni na hivyo watu maelfu ya watu walipoteza ajira.
Mwaka jana wakenya 2,900 waliorothseshwa na HNWI kama watu binafsi wenye kipato cha juu zaidi mwaka jana ambacho kilipungua kwa asilimia 14.6 ikilinganishwa na mwaka 2017.
Zaidi ya miaka mitatu, Kenya ilikabiliwa na sintofahamu ya kisiasa kufuatia uchaguzi wa mwaka 2017, jambo ambalo liliwafanya wawekezaji kuwekeza nchini humo.
Hali mbaya ya hewa pia ambayo iliathiri kilimo- ambacho huchangia ukuaji wa pato la ndani la taifa.
Kushuka kwa idadi ya mamilionea yalikua ni matokeo ya kudorora kwa uchumi, kwa mujibu wa Bw Andrew, mmoja wa watafiti wa ripoti ya utajiri binafsi.
Afrika Kusini iliongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya matajiri binafsi ikiwa na idadi ya watu wenye utajiri wa kupindukia 1,033, ikifuatiwa na Misri ( 764), Nigeria (724) Morocco na Tanzania (114).
Source: BBC
======
Inakadiriwa kuwa Mamilionea 499 kwa kiwango cha dola wamepungua nchini Kenya kutoka mwaka jana.
Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2020 shirika linalofuatilia kiwango cha utajiri binafsi wa watu (HNWI) , Wakenya sita pia walishuka kutoka kwenye kikundi cha watu matajiri sana wanaofahamika kama Ultra High Net- Super (YHBW1) wakiwa na zaidi ya shilingi bilioni 3, na hivyo kupunguza idadi yao na kufikia 42.
Ripoti hiyo imeeeleza kuwa jinsi uchumi wa Kenya ulivyo waumiza watu binafsi matajiri ambao kila mmoja wao alikua na zaidi ya shilingi milioni 100.
Mabadiliko haya yametokea katika mwaka ambao Kenya imepitia kipindi kigumu cha uchumi, ambacho kilisababisha kushuka kwa faida katika kampuni na hivyo watu maelfu ya watu walipoteza ajira.
Mwaka jana wakenya 2,900 waliorothseshwa na HNWI kama watu binafsi wenye kipato cha juu zaidi mwaka jana ambacho kilipungua kwa asilimia 14.6 ikilinganishwa na mwaka 2017.
Zaidi ya miaka mitatu, Kenya ilikabiliwa na sintofahamu ya kisiasa kufuatia uchaguzi wa mwaka 2017, jambo ambalo liliwafanya wawekezaji kuwekeza nchini humo.
Hali mbaya ya hewa pia ambayo iliathiri kilimo- ambacho huchangia ukuaji wa pato la ndani la taifa.
Kushuka kwa idadi ya mamilionea yalikua ni matokeo ya kudorora kwa uchumi, kwa mujibu wa Bw Andrew, mmoja wa watafiti wa ripoti ya utajiri binafsi.
Afrika Kusini iliongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya matajiri binafsi ikiwa na idadi ya watu wenye utajiri wa kupindukia 1,033, ikifuatiwa na Misri ( 764), Nigeria (724) Morocco na Tanzania (114).
Source: BBC