Wizara ya Madini
Govt Institution
- Apr 12, 2025
- 47
- 19
Leo tarehe 19 Mei, 2025 Ujumbe wa Tanzania kutoka Wizara ya Madini, ukiongozwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini Msafiri Mbibo, umewasili jijini London nchini Uingereza kwa ajili ya kushiriki Jukwaa la Uwekezaji kwa Sekta ya Madini lililobeba agenda ya Uongezaji Thamani Madini (Minerals Beneficiation And Value Addition).
Jukwaa hilo ni fursa kubwa ya kuvutia wawekezaji wa kujenga viwanda nchini Tanzania na kuondokana na utegemezi wa kusafirisha madini ghafi jambo ambalo litasisimua ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira kwa Watanzania.
Ujumbe huo umepokelewa vizuri na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Mhe. Mbelwa Kairuki, ambapo mazungumzo mafupi kuhusiana na vikao vinavyotarajia kuanza tarehe 20.05.2025 hadi 22.05.2025 yamefanyika.
Jukwaa hilo ni fursa kubwa ya kuvutia wawekezaji wa kujenga viwanda nchini Tanzania na kuondokana na utegemezi wa kusafirisha madini ghafi jambo ambalo litasisimua ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira kwa Watanzania.
Ujumbe huo umepokelewa vizuri na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Mhe. Mbelwa Kairuki, ambapo mazungumzo mafupi kuhusiana na vikao vinavyotarajia kuanza tarehe 20.05.2025 hadi 22.05.2025 yamefanyika.