Tanzania kufundisha marubani...

Tanzania kufundisha marubani...

Hossam

JF-Expert Member
Joined
Feb 10, 2011
Posts
3,548
Reaction score
2,180
Mbavu zangu zimetaka kuvunjika niliposoma kwenye gazeti kuwa NIT soon wataanza kufundisha watu urubani ili kuongeza idadi yao.

Source: Tanzania Daima la leo uk. 3

My take: mwendawazimu sio lazima avue nguo.
 
Unamaanisha Tanzania hakuna kabisa chuo cha kufundisha urubani? Vipo sana kimoja wapo kikiwa cha mzee Omary pale JNIA Terminal One Dar na ndo mmiliki wa ndege za Tropical air. Kinaitwa Tropical Flying School. Sijalisoma hilo gazeti lakini sijaona ambacho kilikuwa kinakuchekesha mpaka uvunjike mbavu. Chuo kimojawapo kingine kipo kule Zanzibar kinamilikiwa na kampuni ya ZENITH AVIATION. Kwani unadhani nini kinaweza kuwashinda NIT? Bado sijaona point yako. Sijui kama unajua kuwa marubani wa JWTZ kwa asilimia kubwa wanajifunzia hapahapa nchini? Pengine pia hujui kuwa marubani wapo wengi tuu waliojifunzia hapahapa nchini na wanarusha ndege hizihizi tunazopanda? Wakiwemo ninaowafahamu mimi na walimu wa urubani pia. Pengine hujui kuwa leseni za urubani ni nani anazitoa? Kuna mamlaka ya usafiri wa Anga ndo wahusika (TCAA).
 
Nimtetee mleta uzi, kilichomvunja mbavu ni TZ kutokuwa na ndege hivyo marubani wakihitimu mpaka wapate ndege wanaweza kusahau urubani, au siyo mpwa?
 
@ cabhati.. Heshima mbele..mkuu unauelewa mkubwa sana. Si hicho tu ulichoona kuna mitaala...practicals...standard...!!! Hovyo kabisa wazo hili...yaani matreni yamewadodea halafu wanataka ndege kweli Tz ni comedians...
 
Kwa hizi ndege zetu mbovu, hawa wanataka kuua tu...
 
Angalia vizuri nembo ya NIT
Utaona hata ndege ipo kwa
kifupi wanaweza tatizo ni
ndege hapa Nchini hakuna.
 
Mbavu zangu zimetaka kuvunjika niliposoma kwenye gazeti kuwa NIT soon wataanza kufundisha watu urubani ili kuongeza idadi yao.

Source: Tanzania Daima la leo uk. 3

My take: mwendawazimu sio lazima avue nguo.

Mkuu umenena kweli,

Tunao marubani kebekebe waliokuwepo tangu enzi za Air Tanzania wako benchi hawaruki. Wengi walioanza na East African Airways wameshastaafu, ila wa ATC bado wapo. Kuna walioondoka nchini wanafanya kazi nje ya nchi kama marubani. Walisomeshwa kwa pesa za walipa kodi, na wengine walisomeshwa nje ya nchi hususan Uholanzi (Fokker), Marekani (Boeing) na Ufaransa (Airbus) Sina hakika marubani waliokuwa wanarusha Twin Otter za ATC na wanaorusha hizi Dash-8 wamejifunzia wapi. Ila kwa kweli wako wengi sana kuliko idadi ya ndege tulizo nazo.

Hivi kweli hatuoni aibu kufundisha marubani wapya wakati wale waliopo tumeshindwa kuwapatia ajira inayofanana na taaluma yao?

Nakubaliana nawe asilimia mia moja na kumi, viongozi hatuna ila wendawazimu kwenye serikali yetu tunao mpaka wa ziada...
 
tatizo mojawapo la Watanzania ni kuamini kuwa Tanzania hatuwezi mambo ya maana kama haya ya kuwafunza marubani. Sana sana mleta mada angesikia kuna chuo cha uganga wa kienyeji bila shaka asingevunjika mbavu!!!
 
inawezekana sana....kwani watanzania tukoje.........?

Capt Preta
HP...7
 
Sioni tatizo lolote katika kufundisha huo urubani, tatizo linakuja kwenye ajira.
 
Watu wengine bwana sasa mnadhani masomo ya urubani ni special kihiiivyo
 
Uganda wanaenda mbio sana na chuo chao kile Soroti!kiko vizuri sana sana kwa sasa!
 
Sioni tatizo kabisa kwa vile urubani una daraja zake. Kumfundisha mtu kurusha ndege ni kitu kimoja ila kumufundisha awe na leseni ya kurusha ndege yenye abiria ni kitu kingine. Mimi nilifanya kozi fupi sana ya kama mwezi mmoja tu nikapata leseni yangu ya kurusha ndege, na ninaruhusiwa kurusha ndege yoyote inayotumia VFR bila kuwa na abiria yoyote. NIT hawashindwi kutoa mafunzo ya aina hiyo!!
 
Inaweekana tena sana nafikiri tunao walimu walio wazuri tu tatizo tunathamini marubani wa kigeni zaidi kuliko wa kwetu,
Nchi nyingi kama Misri kufanya conversion ya leseni lazima ulipe $ 10,000. kwa rubani wa kigeni kuruka kama rubani wa kawaida ili kulinda ajira ya marubani wao tatizo la hapa kwetu rubani wa kigeni anapewa kipaumbele zaidi,
Huo ni mtazamo wangu ninavyowasikia baadhi ya marubani pale terminal 1
Mbavu zangu zimetaka kuvunjika niliposoma kwenye gazeti kuwa NIT soon wataanza kufundisha watu urubani ili kuongeza idadi yao.

Source: Tanzania Daima la leo uk. 3

My take: mwendawazimu sio lazima avue nguo.
 
Hello Capt preta
hivi ile ndege uliyokuwa unaendesha ikavunjika kioo ikiwa angani ishatengema

yah......nilishaweka kioo.....juzi nilikuwa naruka kuelekea Loitoktok.....nikaona skurubu ya bawa inadondoka.......khaa......niliongezaje speed ili nifike nikaikaze......
 
Mbavu zangu zimetaka kuvunjika niliposoma kwenye gazeti kuwa NIT soon wataanza kufundisha watu urubani ili kuongeza idadi yao.

Source: Tanzania Daima la leo uk. 3

My take: mwendawazimu sio lazima avue nguo.

Marubani wa MALORI au wa maguta?? Tuna utani kweli Tanzania!!! Hao NIT wakamilishe kwanza mahitaji ya vitendea kazi kufundishia madereva
 
Back
Top Bottom