Tanzania ipandishe kodi dhidi ya rwanda-air

isotope is the state of same element to have different atomic masses. Example Polonium210,Polonium220.
 
Last edited by a moderator:
Pia serikali ifukuze Wanyarwanda wote wa Mwese[wa mwaka 1955] -Katavi,na Rukwa,Wanyarwanda hao walipewa urai wa kutamka na baba wa Taifa lakini urai huo hautambuliki kisheria,hivyo ni wakati muafaka warudishwe makwao.Ni wengi na wamewekeza sana huko Sumbawanga,Mpanda na hata mbeya,lakini wote origin yao ni Watusi wa Mwese wa Mwaka 1955.

Hao ni watanganyika wenzetu ndugu. Kama sikosei watu wote waliokuwa ndani ya mipaka ya Tanganyika kabla ya uhuru walipewa uraia baada ya nchi kupata uhuru. Kumbuka kuwa Tanganyika imepata uhuru mwaka 1961 hivyo siyo haki kuwaita hao jamaa kuwa ni wanyarwanda. I stand to be corrected by lawyers.
 
Ndio hapo sasa linapo onysha uwazi kua viongozi wa kiafrika wanachofikiria ni matumbo yao tu. Vita na hasama kila siku. Hakuna kiongozi anayefikiria wananchi Wake. Leo Hii kuna watanzania wengi tu wanamarafiki wa kinyruanda na tunashirikiana vizuri na kuishi pammoja na wanaikemea vita kama hivi. Vita vikitokea ni vita vya viongozi wakiwatuma wanajeshi wao. Waadhirika ni wananchi pammoja na wanajeshi wengi wao wakiwaacha watoto yatima. Ndugu zangu watanzania, tuimarishe amani yetu ya ndani na nje ya nchi. Na Pia tuilinde nchi yetu. Tanzania ni nchi pekee ya Afrika inayosifika duniani kwa amani, tuombeni mungu tupate viongozi waaminifu hakika Tanzania itakuja kujitegemea na itakua rahisi kushirikiana na mataifa mengine yenye amani. Ukabila umezidi katika nchi nyingi za Afrika, tuwekeni pembeni ukabila, udini.
 
Wasukuma wana msemo wao usemao: Kusikia kwa kenge mpaka atoke damu masikioni. Huyo jamaa lugha anayoweza kuielewa ni mtutu tu, hayo mengine ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa.

Siungi mkono vita dhidi ya Rwanda. Hakuna sababu zozote za msingi kuingia vitani na pia nchi yetu kwa sasa haina uwezo kiuchumi wa kugharimia vita. Vita ya Uganda yenyewe imetutoa kamasi mpaka leo tunatambaa na kuishi kwa kutembeza bakuli duniani. Sasa ukileta na hiyo nyingine si ndio utakuwa umeuwa kabisa haka kauchumi matonya ketu ka saidia baba?
 
Breaking News: Siku chache baada ya mgogoro kati ya Tanzania na Rwanda ambao umesabisha "wahamiaji haramu" kufukuzwa nchini, bandari ya DAR inaonesha kila dalili za kuyumba baada ya kususiwa na wafanya biashara wa nchi jirani(insider information).
 
Sio issue ya kupandisha kodi bali anga la Tanzania litangazwe "no-fly zone" kwa Rwandan-Air. Zikionekana tu zidunguliwe haraka iwezekanavyo; rada zote zielekezwe huko bila kusahau maeneo mengine. Huyu kaukau hawezi kutufanyia mchezo namna hiyo.
 
Hivi hakuna magari ya mizigo toka Rwanda kuja kwetu TZ? Why not a fist for a fist! Na sisi tupandishe kwa magari ya Rwanda. sIMPLE!
 
Sasa huu ni utoto. Jiulize tukipandisha kodi kwa Rwandair ni nani atakayeumia zaidi, sisi au wao? Kwa taarifa yako, Tanzania tayari inatoza USD 500 kwa magari ya Rwanda kabla hata ya hii vita ya maneno. I bet ulikuwa hujui. Pili, Rwandair inatumiwa zaidi na wa-Tanzania. Kama huamini kaulize au jaribu kufanya booking ya Ijumaa urudi Jpili Dar-Kigali-Dar uone shughuli yake? Wale jamaa wako vizuri, wana ndege mpya na huduma nzuri. Tusitumie hisia kama ugomvi wa wanawake mitaani.
 
mnahangaika bure....mtaumiza wananchi wa rwanda na wa tanzania bila sababu....dawa ni kumchakaza na kuichukua kigali.... ...... halafu kutangaza uchaguzi huru......
 
Breaking News: Siku chache baada ya mgogoro kati ya Tanzania na Rwanda ambao umesabisha "wahamiaji haramu" kufukuzwa nchini, bandari ya DAR inaonesha kila dalili za kuyumba baada ya kususiwa na wafanya biashara wa nchi jirani(insider information).

ndio maana nasema kuna kila sababu ya kumpiga kagame na kuitisha uchaguzi huru kigali!
 
na Bakhresa nae atapandishiwa kodi kule, kwahiyo atafunga biashara zake rwanda. imekula kwa nani?
 
Kwa vile anaugomvi na magari ya Tanzania, dawa yake tuanzishe bandari ya nchi kavu karibu na mpakani. Magari yote ya Tanzania yakifika pale yanapakuwa mizigo na kuipakia kwenye magari yaliyosajiliwa kwao.
.Good idea.
 
Tanzania ni watu makini hakuna mambo ya kukurupuka tusubiri tuone itakuwaje kama haya mambo nikweli ndio tuchukue action bado mapema sana ku act sisi over

Uwezo wake wa kufikiri ni kama kagame
 
Hizi ni trade embargoes na zimepangwa kwani ukiachia ushuru wa magari kupanda pale mpakani,kukatwa umeme pale Kagera ni vikwazo tayari na nategemea pia Kenya nao wanaandaa la kwao sasa sijuhi ni kustop Flights ama nini ila ngoja tusubiri.
Kuna falsafa moja huwa naiamini kwamba ni bora kijana ukaharibu mbali kuliko kuwaharibia masela wako wa kitaha ama kijiweni make ukikosa huko ukafurumushwa wao watakukinga kama shield yako,leo siye tunaharibu maskani zetu kwa majirani wa bali(US) ...ngoja tuone.
 
Nakubaliana na hili wazo kabisa .It happened the same kati ya Mexico na USA during George Bush helm

hAPA TUNADHANI KUWA SISI HATUHITAJI KUSAFIRI KWA HIZO NDEGE ZA RWANDA. HUTAKI KUONA KUWA TUKIPANDISHA SISI PIA TUTAPANDISHIWA NAULI KWA KUTUMIA NDEGE ZAO?
 
Back
Top Bottom