Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,268
- 33,040
Tunamwitaji atakayeoteshwa kuhusu dawa ya kumaliza matakataka mijini. Na mwingine aoteshwe dawa ya kuwaondoa wapiga debe mijini. Mwingine aoteshwe dawa ya kuwaondoa wafanyabiashara wanaopanga bidhaa mabarazani na njiani.
Hivyo ndivyo ilikuwa ikisema status update yangu kwenye facebook. Nilisukumwa kuandika huo ujumbe kwa sababu ya
mambo ambayo yamekuwa yakitokea katika nchi yetu kwa siku za karibuni.
Tumekuwa tukisikia kila kukicha juu ya watu ambao wanadai kuwa wameoteshwa na mungu (lower case m) dawa ya magonjwa
sugu yanayowakabili waTZ. Mambo yalianzia Loliondo au kwa Babu kama wengi wetu tunavyopenda kupaita. Ilianza kwa mchungaji mstaafu wa KKKT, Ambilikile Mwaisapile, kuoteshwa dawa ya magonjwa sugu.
Baada ya hapo umefuata utitiri wa watu ambao kila kukicha wamekuwa wakiibuka na kudai kwamba wameoteshwa juu ya dawa ambayo hakuna ugonjwa ambao haitibu ukiamini. Ukiamini nini? Ni swali ambalo watu, hata waliotumia hiyo dawa,
hawawezi kukwambia. Ukimwamini Mungu? Ukiliamini neno la Mungu? Ukiiamini dawa? Ukiamini kwamba dawa ile inaponya? Ukimwamini mtoa dawa? Ukiuamini mrigariga? UKIAMINI NINI?
Nilishasema hapo awali na ninarudia kusema: jamii ya Watanzania inayo magonjwa sugu mengi ukiachilia ya kisukari, UKIMWI, kansa, stroke, shinikizo la damu, presha, vidonda vya tumbo n.k. Tunayo magonjwa ambayo yanahitaji tiba isiyo ya kawaida. Je nani atathubutu kujitokeza akadai kuwa ameoteshwa kuyatibu haya magonjwa?
Ni nani ataoteshwa dawa ya foleni mijini? Nani ataoteshwa dawa ya ukosefu wa maji vijijini? Nani ataoteshwa dawa ya kukatikakatika kwa umeme? Nani ataoteshwa dawa ya uchafu unaozagaa kila kona katika miji na majiji yetu? Nani ataoteshwa dawa ya kupanda bei kwa bidhaa kila kukicha? Nani ataoteshwa dawa ya umaskini? Nani ataoteshwa dawa ya mikataba mibovu? Nani? Nani?
Ila sasa, Je, akijitokeza atakayeoteshwa dawa ya magonjwa haya TUTAMSHABIKIA? Je, tutapanga foleni kumpa sapoti? Je, tutajipanga nyuma yake na kumwambia, tuna imani na wewe? Je, tutaamini?
Rafiki yangu mmoja akaniambia na hapa namnukuu: Magufuli alioteshwa dawa ya kuondoa kero za barabara mbovu. Je, uliona kilichompata? Sote tunajua kilichompata. Hatukumwamini. Hatukuamini!
Hivyo ndivyo ilikuwa ikisema status update yangu kwenye facebook. Nilisukumwa kuandika huo ujumbe kwa sababu ya
mambo ambayo yamekuwa yakitokea katika nchi yetu kwa siku za karibuni.
Tumekuwa tukisikia kila kukicha juu ya watu ambao wanadai kuwa wameoteshwa na mungu (lower case m) dawa ya magonjwa
sugu yanayowakabili waTZ. Mambo yalianzia Loliondo au kwa Babu kama wengi wetu tunavyopenda kupaita. Ilianza kwa mchungaji mstaafu wa KKKT, Ambilikile Mwaisapile, kuoteshwa dawa ya magonjwa sugu.
Baada ya hapo umefuata utitiri wa watu ambao kila kukicha wamekuwa wakiibuka na kudai kwamba wameoteshwa juu ya dawa ambayo hakuna ugonjwa ambao haitibu ukiamini. Ukiamini nini? Ni swali ambalo watu, hata waliotumia hiyo dawa,
hawawezi kukwambia. Ukimwamini Mungu? Ukiliamini neno la Mungu? Ukiiamini dawa? Ukiamini kwamba dawa ile inaponya? Ukimwamini mtoa dawa? Ukiuamini mrigariga? UKIAMINI NINI?
Nilishasema hapo awali na ninarudia kusema: jamii ya Watanzania inayo magonjwa sugu mengi ukiachilia ya kisukari, UKIMWI, kansa, stroke, shinikizo la damu, presha, vidonda vya tumbo n.k. Tunayo magonjwa ambayo yanahitaji tiba isiyo ya kawaida. Je nani atathubutu kujitokeza akadai kuwa ameoteshwa kuyatibu haya magonjwa?
Ni nani ataoteshwa dawa ya foleni mijini? Nani ataoteshwa dawa ya ukosefu wa maji vijijini? Nani ataoteshwa dawa ya kukatikakatika kwa umeme? Nani ataoteshwa dawa ya uchafu unaozagaa kila kona katika miji na majiji yetu? Nani ataoteshwa dawa ya kupanda bei kwa bidhaa kila kukicha? Nani ataoteshwa dawa ya umaskini? Nani ataoteshwa dawa ya mikataba mibovu? Nani? Nani?
Ila sasa, Je, akijitokeza atakayeoteshwa dawa ya magonjwa haya TUTAMSHABIKIA? Je, tutapanga foleni kumpa sapoti? Je, tutajipanga nyuma yake na kumwambia, tuna imani na wewe? Je, tutaamini?
Rafiki yangu mmoja akaniambia na hapa namnukuu: Magufuli alioteshwa dawa ya kuondoa kero za barabara mbovu. Je, uliona kilichompata? Sote tunajua kilichompata. Hatukumwamini. Hatukuamini!