Tanzania imekwisha??

Lampart

Senior Member
Sep 18, 2009
139
2
Ndugu wana-ukumbi,

Juzi, Sunday, nilipata nafasi kula dinner na rafiki yangu mmoja wa zamani ambae anafuatilia sana mambo ya kwetu na kabla hajapata moja baridi moja moto nikamuuliza “ What’s wrong? Are we the cursed children of Israel? Akacheka sana na huku akinieleza nikae kitako kwanza.
Jamaa akaanza maelezo yake kwa kunieleza kuwa …”Wakulaumika ni JK, kwasababu he underestimated the power of his wapambe. Pili, chaguzi zetu siku hizi zimezidiwa na pesa. Kama huna pesa CCM hutopata kuchaguliwa – mama Sofia Simba anajua hilo pia”, akanieleza.
“JK kawaruhusu watu wachangie hasara zake za uchaguzi bila ya kuweka kiwango (ceiling), na pia wala hakuwa anaulizia pesa anazopata za uchaguzi zilikuwa zikitoka wapi, as a result hawezi hivi sasa kuwafanya lolote hao akina Rostam, Chenge, Lowassa, etc – hata kama kesho wakimuua mtu”. Hapo akafafanua kwakusema kuwa “ Kila nchi leo inakubali private contributions kwaajili ya chaguzi, lakini sio amount kubwa kama alizokuwa akipokea JK. Kama mtu katoa half a billion, je, baada ya uchaguzi utaweza kumuweka jela akifanya kosa mtu huyo?” Aliniuliza.
“JK anajua mambo yote ya rushwa na ufisadi yanayoendelea na yaliyotendeka nchini, but he is powerless. JK anajua nani alokula hela ya Radar. JK anajua kuwa Chenge kakutwa na hela ya Radar, lakini anaogopa kumchukulia hatua za haraka, kwani anaweza kusema mzee zile campaigns zako zilizokuwa zikilipiwa vipi? Je, JK atajibu nini hapo? JK hawezi kumueleza kitu Rostam pia pamoja na hao mafisadi wengine kwasababu wao ndio waliomuweka yeye kitini na sio wananchi. Kosa la JK nikuwa he underestimated the whole situation. Alidhania kuwa akiwa Rais basi atafanya lile atakalotaka yeye. Ile ari yake yote ambayo ilikuwa ikitegemewa imekufa, because he doesn’t hold the real power in CCM. Power in CCM is hold by few who have money – pesa ambazo zimeibiwa kutoka serikalini”.
Jamaa akaendelea kusema kuwa ”Chenge anaposema kuwa ni mwenye vijisenti tu – hio ni kweli kabisa, kwani the bulk of the commission from the purchase of the Radar went to other big guys. Yeye alikuwa akigawa tu na hatujui kama JK nae hakuwahi kumegewa na ndio maana anakaa kimya na hajui amfanye nini Chenge isipokuwa anasema eti kesi nyengine 3 zinakuja. Zinakuja lini wakati ushahidi upo, au anangojea uchaguzi wa 2010 umalizike?”.
Akaendelea kijana kunieleza kuwa nisifikirie kama JK anafurahia haya ya ufisadi and in fact anataka kuachia ngazi hio 2010, lakini wapambe hawataki mpaka amalize. Hili sasa ndio linalomharibia afya yake na japokuwa Daktari wake kasema kuwa hana tatizo lolote – hio sio kweli, kwani hawezi kusema publicly kama ni mwenye tatizo. “Nenda wewe ukayasome maelezo ya Dakatari wake chini ya BP na utaona kuwa besides ya kuwa madaktari wanampima BP yake kila mara, yeye mwenyewe kapewa ile instrument ili ajipime kila siku anapoamka tu. Sasa kama wewe mtu huna BP na madaktari wanasema you are okay, tena sasa ya nini ujipime kila siku?” Aliendelea kudokeza jamaa.
Pia akanieleza kuwa serikali za nyuma ziliharibiwa kidogo na ma-Mama Rais – yaani ile ya Sh. Mwinyi by Mama Mwinyi na ile ya Mkapa by Mama Anna. Alinieleza kuwa yeye anamjua Mkapa vizuri sana tokea Foreign Affairs na lake kubwa mzee ni kupata chupa lake la Whiskey na siku yake imekwisha. “Yeye hakuwa mtu wa tamaa kama inavyotangazwa na wapinzani. Mambo mengi yaliopita yeye hakuwa akiyajua au anapoyajua inakuwa too late na kwahivyo uamuzi wa busara unashindikana. Deal ya Kiwira ni baina ya Yona na Mama Mkapa. Mkapa kaelezwa mwisho tu and NOT in detail. Kampuni ya AnnBen Mkapa wala hakuijua. Hio ilikuwa idea ya Yona kwa mama Mkapa. Ni Yule mama Anna na wapambe wake walioleta balaa lote hili na mengi mengineo. Mkewe Mkapa Anna ni Mchaga na Mchaga ni kama jirani zako Wapemba wanavyopenda pesa sana. Pia usisahau kuwa Anna kazaa na Mramba na kwahivyo Mramba alikuwa anapo pakutegemea kwa ufisadi wake. Alikuwa akienda Ikulu mara kwa mara kuliko mawaziri wengine, kwasababu ya kisingizio cha huyo motto waliozaa.” – kaendelea jamaa. Alipofikia hapo mimi nikamkatisha kwani niliona kuwa anaanza kuwa too personal na hio haitosaidia kitu. Labda wakati huo ni kwasababu alikuwa anaimaliza beer ya 4.
Kwahivyo, nikamtoa huko na nikamuuliza kama ipo any hope for our country, nae akasema kuwa there is no hope kwasababu JK itabidi aendelee na katika kipindi chapili hatofanya kitu kuhusu ufisadi. In fact jamaa kasema kuwa in the 2nd round ufisadi utashamiri zaidi, kwani hicho ni kipindi cha lala salama. Nikazidi kumbana hapo na nikamueleza hivyo ndio hakuna kweli tamaa kwa sisi walalahoi?
“Labda tuokolewe na Mola”, alinieleza na akasema kwamba …..”ni lazima atokee mwanajeshi kijana mwenye cheo cha chini. Achukue nchi kwa nguvu and in 7 days wafikishwe mahakamni mafisadi wote na watakaoonekana wanazo hatia za ufisadi katika nchi wawe-summarily executed baada ya pesa zetu kurejeshwa nchini, kama vile alivyofanyiwa yule Ceacescu wa Romania. Then, CCM na vyama vya sasa vote viwe-banned na wanasiasa wa sasa wote wa CCM wasiruhusiwe tena kugombea public office na baada ya mwaka mmoja uchaguzi ufanyike tena under new parties. New constitution iwe-formulated na kazi za Rais ziwe re-defined. Rais na mawaziri wasiruhusiwe kujihusisha na mambo ya biashara tena. Adhabu ya rushwa/ufisadi kwenye nchi iwe ni EXECUTION!!!”. I say, at this point I couldn’t stomach what this guy was saying na nilihisi kutaka kutapika, lakini yeye akaendelea kusema kuwa hii idea itakuwa ngumu kufuzu pia kwasababu ya Zanzibar. Nikamuuliza Zanzibar vipi? Akasema mapinduzi ya kijeshi hayatokuwa supported na watu wa Zanzibar kwasababu wao hawajauona ufisadi mkubwa kule kwao kama ule wa Tanganyika. Pia Zanzibar needs CCM to thrive in order for SMZ to exist.
Nikamueleza kuwa kama Zanzibar hawatoiunga mkono serikali ya kijeshi sasa wao sio watatoka tu kwenye Muungano? Akasema ndio, lakini the rate of recovery for Mainland (from the demise of a coup de tat) without Zanzibar itakuwa ni ndogo – kama vile kutambuliwa nje au na majirani. We need Zanzibaris to support us in order to succeed.”
“Kama wao kutoka kwenye Muungano iwe baadae, lakini sio kwasababu ya hayo mapinduzi,” aliropokwa kijana. Pia akanielezea kuwa …”ikiwa Zanzibar haipo kwenye Muungano mapinduzi ya kijeshi Bara yatakuwa milele kama ni uasi tu”.
Hapo nikamuuliza, sasa hii ni maanake nini? Akajibu ….”ni kwamaba hii inamaana maisha ya Taifa lipo kwenye mikono ya JK. Yeye atatufisidi zaidi tu na haya tunayoyaona hivi sasa yataendelea for years to come, kwani we are now caught up in a vicious circle, kwasababu JK nae atahakikisha kuwa atakaemrithi hatompeleka yeye jela au mahakamani na kwahivyo itabidi awe fisadi kama yeye, yaani ataendelea kuficha maudhi na ufisadi wa CCM”
Hapo ikabidi nimueleze jamaa kuwa tuondoke, kwani rate yake ya kunywa beer ikawa inazidi sana na mimi nilisahau kuchukuwa credit card nilipoondoka nyumbani!
NOTE FROM ME!
Wewe mwana_Forum mpenda nchi yako, tafadhali, baada ya kusoma maelezo ya huyu jamaa ya hapa juu toa your sincere comments. Wewe unafikiria nini? Ni kweli leo Tanzania tumekuwa caught up in a vicious circle na hakuna njia ya kutoka isipokuwa kufanyika mapinduzi ya kijeshi???? Please, be sincere for our country’ sake in your comments bila ya kujali kama wewe ni Mpemba, Mchaga, Mkiristo au Muislamu, etc etc.

 
Ndugu wana-ukumbi,

.....................Kama mtu katoa half a billion, je, baada ya uchaguzi utaweza kumuweka jela akifanya kosa mtu huyo?” Aliniuliza.


Dear Nd. Lampart,
Tafadhali, niruhusu nimnukuu rafiki yako hapa chini kidogo!!!

"Kama mtu katoa helicopter 2, je, baada ya uchaguzi utaweza kumuweka jela akifanya kosa mtu huyo?”

Naona huyo rafiki yako anaziona hela zinazochangiwa CCM tu, lakini mabilioni zinazotolewa CHADEMA kununua helicopter hakuzitaja!
Anyway, birds of a feather flock together!!!!

 
Do you think the so called wanajeshi are themselves saints? jaribu kufuatilia nchi zilizo tumia njia ya mapinduzi uone zilirudi nyuma hatua ngapi. Besides "Africa need strong institutions not strong individuals" to quote barack obama
 
Dear Nd. Lampart,
Tafadhali, niruhusu nimnukuu rafiki yako hapa chini kidogo!!!

"Kama mtu katoa helicopter 2, je, baada ya uchaguzi utaweza kumuweka jela akifanya kosa mtu huyo?”

Naona huyo rafiki yako anaziona hela zinazochangiwa CCM tu, lakini mabilioni zinazotolewa CHADEMA kununua helicopter hakuzitaja!
Anyway, birds of a feather flock together!!!!

Ngida1
Kwa CHADEMA mtu aliyetoa helikopta kusaidia uchaguzi ni rahisi kumweka jela akifanya kosa kuliko ilivyo kwa CCM leo kwa sababu hawana utamaduni wa kulindana. Wamejikita zaidi katika rule of law.
 
1. Kama unasoma JF, hususan kama unamfuatilia Blu, wala hakuna kipya alichosema huyo jamaa, tushayasema yote hapa.

2. Hiyo habari ya kum-exonerate Mkapa si kweli, Mkapa has a sharp head above his shoulders si mtu wa kupelekwa na mkewe, isitoshe Mkapa mbabe mwenye mfumodume usio kifani, walishagombana na mkewe Nyerere akawapatanisha circa 95 ili isiwe soo kwenye kampeni, lakini bila urais Mkapa na mama Anna walikuwa wanaenda separate ways.Hardly pussy whipped.
Mkapa mwanawe alivyosikia baba yake amekuwa rais alipiga ukelele wa huruma na kusema "mamaaaaa watanzania mmekwisha", nilishangaa kidogo, leo nimeelewa vizuri huyu mwanae mwenyewe anamjua ukomunisti wa Mkapa, huyu mkuda unamuona mtu wa kupelekwa pelekwa na mkewe?

3.Hayo mambo ya wajeshi kuchukua nchi unataka kuwapa watu sababu waifunge JF on treason grounds.What do you think this is, 1-800-GET-INDICTED hotline?
Wanaotaka kupindua hawasemi kwenye internet, wanaosema kwenye internet hawataki na hata wakitaka hawawezi kupindua, kwa hiyo usilete soga linaloweza kutucost bila ya kuwa na tija.
 
Ngida1
Kwa CHADEMA mtu aliyetoa helikopta kusaidia uchaguzi ni rahisi kumweka jela akifanya kosa kuliko ilivyo kwa CCM leo kwa sababu hawana utamaduni wa kulindana. Wamejikita zaidi katika rule of law.

Dear Nd. Jasusi,
I wish I could believe you, but tungojee kwanza CHADEMA waipate hio serikali na halafu tuone kama hawana utamaduni wa kulindana. Leo hawana kitu watalindana nini? Watalindana na huo umaskini wao? Ngojea wapate na wao na hapo tena ndio tutajua kama wanao utamaduni huu au vipi.
Kwa kweli binafsi nilivunjika moyo sana nilivyoona kuwa mtu mmoja anachangia chama kama hivi. Hii ni hatari. Hatukatai kuchangia, lakini ni lazima iwepo ceiling, else our parties will be hijacked by the super rich!
 
Do you think the so called wanajeshi are themselves saints? jaribu kufuatilia nchi zilizo tumia njia ya mapinduzi uone zilirudi nyuma hatua ngapi. Besides "Africa need strong institutions not strong individuals" to quote barack obama

Eagle,
We are not looking for saints. We already have one - Nyerere!
We are looking for a way out of this vicious circle. Sasa tutatoka vipi? JK atakuja kumchagua mtu ambae anajua hatokuja kumtia jela yeye kwa makosa haya anayoyafanya hivi sasa, na huyo atakaekuja nae atafanya hivyo hivyo, sasa tutakuwa tunaelekea wapi?
Please, don't talk of kurudi nyuma. What are we doing now? Hivyo kweli hivi sasa tunakuenda mbele wakati watoto wetu wanasoma chini kwenye mchanga, wakati watoto wetu wanauza kuni, wakati watoto wetu wanateka maji. Watoto wetu have today become the hewers of wood and drawers of water! Hivi kweli huku ndio kuenda mbele????
 
Braza Lampart,
Ingawa umeomba comment zetu bila ya kujali itikadi za kidini, lakini huwezi kujizuia bila kutia dini kidogo. Kwani ukiangalia Mkapa ndio alioiyua hii nchi japo kua Kikwete kaja kuimaliza, lakini kelele hizi hatuzisikia wakati wake na hata baada ya kuondoka madarakani. Kwa mujibu wa kanisa , Kikwete ni chaguo la Mungu, Jee Mungu wa kanisa hufanya makosa?. Hayo unayoyasema kua atokee mwanajeshi apindue, hilo sahau kwa sababu CCM imeshainywesha damu ya bendera yake vyombo vya dola vyote kua Jeshi, Polisi na Usalama ni vyombo vya CCM sio vyombo vya dola, hilo kaa ukijua. In my opinion the only way ya kuaamka Wa-Bara ni kwanza kufanya majaribio ya kuiwaacha Znz kujitawala wenyewe ( mind you sisemi kuvunjika muungano hapa) ili ichague serikali na liongozi wamtakae ( hapa pia sisemi lazima CUF au chama kingiine) kwani hata huyo kiongozi wa CCM waachiliwe wamchague wao wa-znz wenyewe, wamechoka kuchaguliwa Dodoma. maendeleo yatakapo-onekana znz hapo ndipo bara wata-amka.
Penginevyo ni kama mwenzangu alivyouliza "kwani hao majeshi sio corrupted?" si tunaona Nigeria wakati wa marshal law na Sudan etc. Tz is very very rich country, people are strugling for one meal a day. It's shame, Ukiona nchi nyengine kubwa kwa eneo na watu na ni ndogo kwa rasilimali lakini watu wanaishi maisha bora.
Take the example moja ndogo tu, Unatoka Mombasa kwa basi mpaka mpakani Horo-horo njia safi ya lami about 120km, lakini another 65km mpaka Tanga ni Adhabu tupu, sasa hapo hapo mtalii anajua kua nakwenda nchi ya tabu,especcially kuwe na mvua, you will be lucky kufika Tanga. Tupeane pole.
 
1. Kama unasoma JF, hususan kama unamfuatilia Blu, wala hakuna kipya alichosema huyo jamaa, tushayasema yote hapa.

2. Hiyo habari ya kum-exonerate Mkapa si kweli, Mkapa has a sharp head above his shoulders si mtu wa kupelekwa na mkewe, isitoshe Mkapa mbabe mwenye mfumodume usio kifani, walishagombana na mkewe Nyerere akawapatanisha circa 95 ili isiwe soo kwenye kampeni, lakini bila urais Mkapa na mama Anna walikuwa wanaenda separate ways.Hardly pussy whipped.
Mkapa mwanawe alivyosikia baba yake amekuwa rais alipiga ukelele wa huruma na kusema "mamaaaaa watanzania mmekwisha", nilishangaa kidogo, leo nimeelewa vizuri huyu mwanae mwenyewe anamjua ukomunisti wa Mkapa, huyu mkuda unamuona mtu wa kupelekwa pelekwa na mkewe?

3.Hayo mambo ya wajeshi kuchukua nchi unataka kuwapa watu sababu waifunge JF on treason grounds.What do you think this is, 1-800-GET-INDICTED hotline?
Wanaotaka kupindua hawasemi kwenye internet, wanaosema kwenye internet hawataki na hata wakitaka hawawezi kupindua, kwa hiyo usilete soga linaloweza kutucost bila ya kuwa na tija.

Nd. Bluray,
Thabit Kombo alivyoelezwa na Karume juu ya Mapinduzi baada ya ghasia za June 1961 alisema zaidi ya hayo unayoyasema wewe. Yeye alisema kuwa "Sultani atatunyonga Karume!"
Karume angelimfuata Thabit Kombo, basi Unguja mpaka leo Sultani angelikuwa anatawala.
Waache watufungie. Tutafungua nyengine. Watatufungia ngapi na mpaka lini?????
Mwisho watakuja kujua kuwa kufungia haisaidii kitu.
Sisi Watanzania jamani ni watu waoga sana. Hata kuzungumza tu tunaogopa!!!!
Huyo jamaa wala sio jeshi, yeye mwenyewe kafurahi tu na wewe ushaingia terror!
Hivyo ndio ushaona kuwa hapa JF tunapanga mapinduzi?????
Kama ni hivyo basi bora tufungeni midomo yetu na tumuachie JK afanye analotaka. Ya nini sasa sisi kila siku kusemasema kama ni waoga hivyo?????
Kwani hayo tunayoyaandika kila siku kuichambua serikali na huyo JF ni mazuri?
 
1. Kama unasoma JF, hususan kama unamfuatilia Blu, wala hakuna kipya alichosema huyo jamaa, tushayasema yote hapa.

Dear Nd. Bluray,
Kuuliza sio ujinga. Huyo blu ni nani, kwani nasi pia tunataka kumfuatilia.
Yeye yupo hapa ukumbini?
 
Dear Nd. Jasusi,
I wish I could believe you, but tungojee kwanza CHADEMA waipate hio serikali na halafu tuone kama hawana utamaduni wa kulindana. Leo hawana kitu watalindana nini? Watalindana na huo umaskini wao? Ngojea wapate na wao na hapo tena ndio tutajua kama wanao utamaduni huu au vipi.
Kwa kweli binafsi nilivunjika moyo sana nilivyoona kuwa mtu mmoja anachangia chama kama hivi. Hii ni hatari. Hatukatai kuchangia, lakini ni lazima iwepo ceiling, else our parties will be hijacked by the super rich!
Ndugu Ngida1,
Hata enzi za TANU ni watu wamoja wamoja waliochangia. Lakini Mzee Rupia
hakulindwa na Nyerere ati kwa sababu tu alisaidia kuchangia TANU. Ni spirit hiyo hiyo inayowaongoza wana CHADEMA.
 
Jamani nani anaweza kutuambia siri ya MSUMBIJI na RWANDA kupaa katika maendeleo?MALAWI kuwa big exporter wa mazao ya biashara kama mbao,pamba,chai,tumbaku,karanga kutushinda sisi?
 
Jamani nani anaweza kutuambia siri ya MSUMBIJI na RWANDA kupaa katika maendeleo?MALAWI kuwa big exporter wa mazao ya biashara kama mbao,pamba,chai,tumbaku,karanga kutushinda sisi?
Siri ni moja tu. Hawajaghubikwa na ufisadi. Tanzania bila ufisadi inawezekana.
Tanzania ya ufisadi katu haitasonga mbele.
 
Do you think the so called wanajeshi are themselves saints? jaribu kufuatilia nchi zilizo tumia njia ya mapinduzi uone zilirudi nyuma hatua ngapi. Besides "Africa need strong institutions not strong individuals" to quote barack obama

Na wameenda mbele hatua ngapi!, nakubaliana na issue ya wanajeshi ila sio hawa wa style hii Tanzania, wanapiga raia bila sababu wakipewa nchi watatupora wake zetu na kulala na watoto wetu kinguvu, God forbid!
 
1. Kama unasoma JF, hususan kama unamfuatilia Blu, wala hakuna kipya alichosema huyo jamaa, tushayasema yote hapa.

2. Hiyo habari ya kum-exonerate Mkapa si kweli, Mkapa has a sharp head above his shoulders si mtu wa kupelekwa na mkewe, isitoshe Mkapa mbabe mwenye mfumodume usio kifani, walishagombana na mkewe Nyerere akawapatanisha circa 95 ili isiwe soo kwenye kampeni, lakini bila urais Mkapa na mama Anna walikuwa wanaenda separate ways.Hardly pussy whipped.
Mkapa mwanawe alivyosikia baba yake amekuwa rais alipiga ukelele wa huruma na kusema "mamaaaaa watanzania mmekwisha", nilishangaa kidogo, leo nimeelewa vizuri huyu mwanae mwenyewe anamjua ukomunisti wa Mkapa, huyu mkuda unamuona mtu wa kupelekwa pelekwa na mkewe?

3.Hayo mambo ya wajeshi kuchukua nchi unataka kuwapa watu sababu waifunge JF on treason grounds.What do you think this is, 1-800-GET-INDICTED hotline?
Wanaotaka kupindua hawasemi kwenye internet, wanaosema kwenye internet hawataki na hata wakitaka hawawezi kupindua, kwa hiyo usilete soga linaloweza kutucost bila ya kuwa na tija.


I simply like your views in many things!
 
Ndugu Ngida1,
Hata enzi za TANU ni watu wamoja wamoja waliochangia. Lakini Mzee Rupia
hakulindwa na Nyerere ati kwa sababu tu alisaidia kuchangia TANU. Ni spirit hiyo hiyo inayowaongoza wana CHADEMA.


Dear Nd. Jasusi,
Mzee Rupia alichangia pesa zenye thamani ya bei ya helicopter mbili
kwa wakati mmoja?
Hakuna anaekataa michango katika sisi wanachama wa Chadema, lakini michango mikubwa kama hii inazo hatari zake. JK anashindwa kuiendesha nchi kwa sababu ya michango kama hii na sisi leo tena kwenye Chadema yetu tunaikaribisha? Tunawasema CCM nini na sisi tunafanya nini?
Kama Chadema ilikuwa haina uwezo wa kununua helicopters 2, basi pia itakuwa haina uwezo wa kuzi-maintain hizo helicopter na mchangiaji ataendelea kuchangia kila siku, else hizo helicopters zitakufa. Sasa hii ni sawa????
 
Dear Nd. Lampart,
Mimi moyoni mwangu ninakubali kuwa ipo haja ya mapinduzi hapa Tanzania - iwe leo na sio kesho, else hatutoweza kutoka kwenye hii vicious circle that has been created by CCM and in which we are now all caught up!
Hata Mwalimu Nyerere angelikuwa hai leo, basi angeyaunga mkono mapinduzi kama hayo.
Jambo moja tu ambalo silikubali ni kuwa kama hayo mapinduzi yatafanywa na majeshi. Mapinduzi kama hayo tunataka yafanywe na raia wenyewe, kama walivyofanya kule Philippines siku zile walivyomuondoa Marcos. Nasi inatakiwa tufanye mapinduzi kama yale ili kumuondoa JK, kwani kwa kura CCM haitoondoka ng'o!!!
Katika moja ya sherehe za Mapinduzi ya ZNZ za huko nyuma nilizohudhuria Mwalimu Nyerere mwenyewe alisimama na kusema mbele ya wananchi kuwa....." where all ways fail, a people's insurrection becomes the only alternative for an oppressed people to redeem themselves from their oppressors". Oppressors hapo Mwalimu akimaanisha Sultani na ma-henchmen wake. So, if what Mwalimu said was true against the Sultan it should also be true today against JF and his mafisadi (CCM).
Mwalimu alipokuwa akiyasema hayo hakuwa ana-commit treason. Sasa itakuwaje sisi leo tuyaseme hayo hayo ya Mwalimu na watu waseme kwamba tuna-commit treason???
Mkuki kwa nguruwe kwa binaadamu mchungu???
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom