Tanzania haipo kati ya nchi masikini duniani

Mtoa mada yuko sahihi,tatizo kundi kubwa zaidi la Wa Tanzania hawafikiri bali hukariri. Nitatoa mifano michache kuthibitisha sisi si maskini ila akili za baadhi ya wenzetu zimejazwa ujinga huo. Tuanze na vyakula. Nenda vijijini;Pima wanakula nini ,mara ngapi kwa siku na gharama ya wanachokula. Vipe thamani vyakula hivyo kwa fedha ya kwetu na watawala wa Dunia. Thibitisha je sisi ni maskini? Usihangaike eneo lako la kupima ukaenda eneo la ukame au mafuriko tu,au ukatumia jamii ya wavivu kutuma. Pima watenda kazi wasiosubiri serikali kuwasimamia . Jamii tunayoiita maskini na inakula mlo mmoja uhalisia ni huu ufuatao. Asubuhi hula matunda embe,ndizi,papai,pera na baadhi hunywa uji au chai. Wapimaji hawamhesabu aliyekula tunda badala ya chai kuwa kapata kifungua kinywa. Kwao bila chai hujapata mlo wa asubuhi. Wapo wa Tanzania asubuhi hula dona la nguvu,mboga za majani na maziwa.Hawanywi chai,kwa kuwa kipimo kilichopo ni chai asubuhi tunawahesabu hawajapata kifungua kinywa. Najiuliza kipi kina faida kubwa kiafya? Umiliki wa mali. Ukiacha " tuliong'ang'ania mjini" ni wapi ukiondoa Kilimanjaro utamkuta Mtanzania hawezi kuipata ekari moja ya ardhi yake? Thamani ya ardhi hiyo nani kaipima? Tuwatawanye wawili wasio na kitu ila wana nguvu na akili. Mmoja apelekwe Kenya mmoja aletwe Tanzania tuwape miezi 6 walete taarifa ya kuipata ardhi. Elimu. Tumetelemka mno. Tuliwahi kufikia 95% ya jiwa Tanzania kujua kusoma na kuandika. Tukadeka tumeharibu hadi tunaudhi chanzo in kusubiri misaada. Sisi si maskini tubadili mtazamo wetu.
Mkuu umesema kweli kabisa.. nakubaliana na wewe 100%. Kuna watu hawajui nini maana ya milo mitatu. ila wanashiba hadi kusaza na hawanunui chakula. wana mihogo, viazi, ndizi, maziwa etc. kisha mtu anakuja eti unaishi chini ya dolla 1? Propaganda mbaya sana hii
 
Ni kweli tunapaswa kubadili mind set zetu kwamba sisi siyo masikini. Hata hiyo reli ya kati ya standard gauge tukiamua kila mtanzania achangie angalau tu. Shs. 1000/ trion 45 zitapatikana ambazo zinatosha kabisa kujenga reli hiyo. Uwezo huo tunao na wapo wengi tu watatoa hata laki moja au zaidi. Wasiwasi wetu ni kuwa michango hii inaweza tafunwa na wachache, mafisadi.
Yap yap!! Hili wazo hua nalipigia sana debe lkn nakosaga wakuniunga mkono.......

Ni kweli kabisa kama kila mtanzania akichangia pesa halisi na si masuala yao wanayoyaita kodi!

Yaani kila kitu tutakifanya kwa muda mfupi sana na tutakua nchi tajiri na yenye kupigiwa mfano ulimwenguni kote
 
TANZANIA HAIPO KATI YA NCHI MASKINI DUNIANI

Kila ninapo soma habari za tanzania nakutana na maelezo kwamba Tanzania ni moja ya nchi maskini sana dunia, miaka nenda rudi bado wanatuita maskini.

Swali ninalo jiuliza kwanini watupangie au kwanini watuite maskini, hii inanikumbusha watu ambao nilikutana nao shuleni ili kuniweka chini yao basi wataniambia sina akili kabisa na mjinga kabisa.

Ukisoma wikipedia kuhusu Tanzania utakutana na sentensi hii (Tanzania is one of the poorest countries in the world)

Baada ya kufanya utafiti nikagundua kutoka ktk kundi hili au kutoka ktk dimbwi la kuitwa maskini ni jukumu letu watanzania, lazima tufike mahali tukatae kwa vitendio na kujua wapi tunatakiwa kuwa.

Nimejaribu kutafuta baadhi ya source nikaona tanzania haipo kati ya nchi kumi za mwisho maskini. Mfano unaweza soma hapa. Top 10 Most Poorest Countries In The World 2015

Lakini pamoja na kuona baadhi ya source zinaitoa Tanzania ktk listi ya nchi maskini nimepata maswali yakujiuliza kama ifutavyo

1. Nani atapigania haki ya tanzania kufutwa kwenye listi ya nchi maskini kama walivyo fanya kenya

2. Kwa nini na sisi wenyewe watanzania tusikatae kuitwa maskini, fikra ambayo inatufanya tufanye mambo kimaskini, wote mmemsikia waziri wa fedha siku chache zilizo pita akisema eti haiwezekani kujenga reli kwa fedha zetu za ndani, hayo ni mawazo ya kimaskini kabisa.

3. Je serikali ina mpango gani wa kujipima yenyewe badala ya kutegemea mashirika ya nje kutupimia vitu kama GDP , etc.

hii vita ya kuukata umaskini inabidi ifanywe kwa umoja na umahili mkubwa , kwa kutangaza Tanzania kama nchi ambayo si maskini kwa kutumia vyombo vyote vya habari kama Internet, forums etc, Kila tunapo taja tanzania lazima tueleze kuwa tanzania si nchi maskini, nchi yenye utajiri mwingi, yenye amani etc

Kwanini turuhusu watu wengine kututangaza kwa ubaya?

Tanzania si nchi maskini wala moja ya nchi maskini.

Nawasilisha
Sisi ni maskini ingawa hatukutakiwa kuwa maskini. Hayo mambo ya orodha yanategemea vigezo vinavyotumika na data wanazopelekewa. Naona watanzania ni maskini kwa sababu zifuatazo:
- asilimia kubwa ya wananchi wa kijijini hawaishi kwenye nyumba bora.
- asilimia kubwa ya watanzania wote wanaishi kwenye slums na wala hawaoni ni ajabu. Vyoo bado ni vya shimo ingawa sasa hivi kuna maboresho kidogo mijini (Blair toilets).
- asilimia kubwa hawana vyombo binafsi vya usafiri kama gari, boda boda au bajaji. Wakazi wengi wa vijijini hutumia baiskeli.
- asilimia kubwa ya watoto wanasoma wakiwa wamekaa chini, wengine hata madarasa hawana.
- asilimia kubwa ya watanzania hawana access ya kupata matibabu mazuri. Madaktari wengi hutumia sio zaidi ya dakika 10 kuona mgonjwa, matokeo yake huyu mgonjwa anaweza kuwa misdiagonized. Wengi pia hawana hata hiyo hela ya kumuona daktari au ya vipimo kwa hiyo wengi wetu tunanunua dawa kwenye Maduka ya dawa au tiba mbadala.
- asilimia kubwa hawapati lishe kutokana na umaskini. Kwa baadhi yetu milo mitatu kwa siku tunaisikia kwenye bomba. Kunawanaokosa vyakula vyenye protini kwa vile kundi hili la chakula ni ghali, ukilinganisha na mboga za majani. Maharage yamesaidia sana.
- asilimia kubwa tunategemea mitumba, ikipigwa marufuku tutaumbuka.
- magari pia ni ya mtumba. Wachache sana wananunua magari mapya.
- asilimia kubwa hatuna akiba benki. Vijijini huwa wanaweka akiba ya chakula ndani endapo watavuna vizuri.
- kilimo bado ni cha kizamani. Kazi kubwa mavuno kidogo au kukosa kabisa.
 
Mkuu .. tunaaminishwa tuu kwamba sisi ji maskimi ili tuwe na fikra za kimaskini. lakini sisi sio maskini

Wanaotuita masikini wanatumia vigezo vya uchumi kutupima: GDP, GNP, income per capita, upatikanaji wa hujuma za kijamii na ubora wake, n.k. Sio suala la kutuaminisha tu. Na ukweli uko dhahiri kwamba Watanzania wengi sana tu masikini. Tunaishi katika mazingira duni sana.

Inawezekana viongozi wetu kwa muda mrefu ndio wametuaminisha kuwa nchi yetu ni masikini sana ili wasibanwe kuhusu utendaji wao huku wakiratibu ufisadi wa mapato na rasilimali kibao za taifa bila kuhojiwa.
 
Tanzania ipo katika Nchi masikini,tatizo kutokua na umakini katika mambo ya Msingi kwanza..Tanzania yoote hawawezi kulima kama kuna eneo ni kame ilitakiwa kuwe na ghara kubwa la chakula la Taifa kwa wakazi hao..unaenda Sumbawanga mahindi hadi yanaharibika,ndizi Rombo zinaharibika kwa ajili ya kukosa usafiri mpaka maeneo husika na hasa inazingatiwa biashara ni Dar na Nairobi wakati singida,dodoma,Tabora ni shiida kabisa..Elimu haithaminiwi hakuna madawati majengo yanajengwa kwa sanaa tuu mara halilingani na fedha iliyotolewa ? Magari ambayo yabnatakiwa yabebe abiria au mizigo kodi haikamatiki watakaoleta ni wachache na gharama za kila kitakachobebwa kitakua juu..kodi ya pick up nissan Navara zambia waliishusha baada ya kugundua ni gari ya kazi na inasaidia jamii na haisumbui sumbui..hatuzungumzii Madini tulionayo,mbuga za wanyama,gesi na vyanzo vingine vya mapato ili kulikomboa Taifa katika hili janga la umasikini ndio tupo kupanga kupandisha kodi ya vifaa vya ujenzi ili wananchi waendelee kujenga vibanda tuu na si Nyumba Bora..
 
Sisi ni maskini ingawa hatukutakiwa kuwa maskini. Hayo mambo ya orodha yanategemea vigezo vinavyotumika na data wanazopelekewa. Naona watanzania ni maskini kwa sababu zifuatazo:
- asilimia kubwa ya wananchi wa kijijini hawaishi kwenye nyumba bora.
- asilimia kubwa ya watanzania wote wanaishi kwenye slums na wala hawaoni ni ajabu. Vyoo bado ni vya shimo ingawa sasa hivi kuna maboresho kidogo mijini (Blair toilets).
- asilimia kubwa hawana vyombo binafsi vya usafiri kama gari, boda boda au bajaji. Wakazi wengi wa vijijini hutumia baiskeli.
- asilimia kubwa ya watoto wanasoma wakiwa wamekaa chini, wengine hata madarasa hawana.
- asilimia kubwa ya watanzania hawana access ya kupata matibabu mazuri. Madaktari wengi hutumia sio zaidi ya dakika 10 kuona mgonjwa, matokeo yake huyu mgonjwa anaweza kuwa misdiagonized. Wengi pia hawana hata hiyo hela ya kumuona daktari au ya vipimo kwa hiyo wengi wetu tunanunua dawa kwenye Maduka ya dawa au tiba mbadala.
- asilimia kubwa hawapati lishe kutokana na umaskini. Kwa baadhi yetu milo mitatu kwa siku tunaisikia kwenye bomba. Kunawanaokosa vyakula vyenye protini kwa vile kundi hili la chakula ni ghali, ukilinganisha na mboga za majani. Maharage yamesaidia sana.
- asilimia kubwa tunategemea mitumba, ikipigwa marufuku tutaumbuka.
- magari pia ni ya mtumba. Wachache sana wananunua magari mapya.
- asilimia kubwa hatuna akiba benki. Vijijini huwa wanaweka akiba ya chakula ndani endapo watavuna vizuri.
- kilimo bado ni cha kizamani. Kazi kubwa mavuno kidogo au kukosa kabisa.
Umeandika vitu ambavyo umeaminishwa kwamba ukiwa navyo basi wewe ni maskini.
Mahoteli mangapi yamejengwa kwa makuti ambayo mwananchi wa kawaida akiwa na nyumba ya makuti unamwita maskini.
matajiri wangapi wanamiliki magari chakavu lakini mwana tabora akimiliki gari chakavu unamwita maskini
Lazima tujikubali wenyewe la sivyo ipo siku tutaitwa wachawi na tutakubali
 
Umeandika vitu ambavyo umeaminishwa kwamba ukiwa navyo basi wewe ni maskini.
Mahoteli mangapi yamejengwa kwa makuti ambayo mwananchi wa kawaida akiwa na nyumba ya makuti unamwita maskini.
matajiri wangapi wanamiliki magari chakavu lakini mwana tabora akimiliki gari chakavu unamwita maskini
Lazima tujikubali wenyewe la sivyo ipo siku tutaitwa wachawi na tutakubali
Sikusemea makuti, nimeongelea nyumba ambazo udongo unamomonyoka.

Sijaongelea magari chakavu. Nimeongelea uwezo wa kununua (spending power) magari mapya.

Hivi mtanzania hana akili ya kuona na kupambanua kitu? Mpaka aaminishwe na mtu. Hivi ninavyovisema hujaviona? Unaishi ulimwengu gani? Au umeamua kufumbia macho.
 
Wakati mwingine kutiana hamasa ni njia mojawapo ya kujisahaulisha umaskini. Inawezekana mleta mada anaishi mjini, kwa hiyo anafikiri watanzania wote wana viwango vya maisha kama vya watu wa mijini (hata umaskini unaonekana mijini pia). Tusijidanganye, ni kweli kabisa kwamba TANZANIA NI MOJA YA NCHI MASKINI DUNIANI kama huamini funga safari leo nenda vijijini waliko watanzania wengi ukajionee mwenyewe.
 
Ukweli ni kwamba Tanzania ni miongoni mwa nchi masikini Dunia, kusema kuwa hatupo katika nchi 10 masikini zaidi duniani siyo sababu ya sisi kutokuwa masikini,

Kwa kuangalia tuu kwa kawaida sisi tupo nyuma sana kwa maendeleo ya nyaja zote, kiuchumi, kijamii na kisiasa, ebu jaribu kuangalia Huduma za kijamii zinazotolewa Tanzania ni za hali ya chini sana, ukienda mashuleni hapafai, hospitalini huko ndipo usiseme mashrika na taasisi za serikali zimechoka kila idara.

Nikiwa nasafiri kwa Basi kutoka dar to mwanza nikifka mikoa ya kati singda tabora na baadhi ya sehemu za mwanza na shinyanga nikiona watu walivyochoka na maisha nawaza sana
Mimi sio mpenzi wa kusafiri ila mwaka jana nilienda dodoma, daaaaah nilisikitika sana mkuu!
 
Mpaka mwishoni mwaka miaka ya 90 China ilikuwa ikihesabiwa kama nchi maskini na iliwekwa ktk kundi la nchi zinazostahili kusaidiwa,mfadhili mkuu wa China alikuwa Germany. Leo hii China ni nchi tajiri sana duniani.Siri no nini?they didn't cry out complaining why they're called the poor country? They worked hard instead,with the goals they set and ambitions for higher success they had they finally got there where they are today,the economic giant. Let's keep crying and complaining while doing nothing to improve our people's lives and country's economic wellbeing in general.
Raia yoyote wa China ambae anagharimu taifa lake kimaendeleo huwa wanaua, wana sheria kubwa sana juu ya watu namna hiyo.
Kwa kifupi ni kwamba, jamaa wapo seious, Tanzania ni drama tuu. Leo hii mtu kama jk kamaliza muhula wake nchi ikidaiwa 49 trilionz, hakuna aliyehoji. Aliyekaa sasa madarakani Idara aliyosimamia ina deni la 1Trilion, 900 Bilionz zilikuwa ni Penalty, leo hii na yeye ni Rais.
Aliyeaminishwa kuwa ni fisadi mkuu leo hii kaamia upinzani, na hapo hapo kapewa ruhusa ya kugombea Urais.
Tanzania hatupo serious kwa kila ktu, ni dramas tuu.
 
Nina kubariana na Wewe kwa 100% nimejaribu kutembelea nchi nyingi lakini nikagudua Tanzania ni nchi tajiri sana mpaka sasa sijaona umasikini Hata kidogo wa mali, ila nimegundua umadikini wetu nj kubweteka kutopenda kufanyakazi, na watu kutowajibika ipasavyo. Tanzania ni nchi ya neema iliyojaa maziwa na asali,
-Unadhani deni la 49Trilionz limetokana na wananchi kutofanya kazi?
-Kama watu hawafanyi kazi hizo pesa za ESCROW, MEREMETA, EPA zimetoka wapi?
 
Yap yap!! Hili wazo hua nalipigia sana debe lkn nakosaga wakuniunga mkono.......

Ni kweli kabisa kama kila mtanzania akichangia pesa halisi na si masuala yao wanayoyaita kodi!

Yaani kila kitu tutakifanya kwa muda mfupi sana na tutakua nchi tajiri na yenye kupigiwa mfano ulimwenguni kote
Kwa jinsi wanavyoramba pesa zetu na kujibinafsisha mali zetu leo hii upite mchango harafu nitoe pesa yangu?
Thubutuuu!!!!! Hii nchi huko juu kila mtu ni mwizi.
 
Sisi ni maskini ingawa hatukutakiwa kuwa maskini. Hayo mambo ya orodha yanategemea vigezo vinavyotumika na data wanazopelekewa. Naona watanzania ni maskini kwa sababu zifuatazo:
- asilimia kubwa ya wananchi wa kijijini hawaishi kwenye nyumba bora.
- asilimia kubwa ya watanzania wote wanaishi kwenye slums na wala hawaoni ni ajabu. Vyoo bado ni vya shimo ingawa sasa hivi kuna maboresho kidogo mijini (Blair toilets).
- asilimia kubwa hawana vyombo binafsi vya usafiri kama gari, boda boda au bajaji. Wakazi wengi wa vijijini hutumia baiskeli.
- asilimia kubwa ya watoto wanasoma wakiwa wamekaa chini, wengine hata madarasa hawana.
- asilimia kubwa ya watanzania hawana access ya kupata matibabu mazuri. Madaktari wengi hutumia sio zaidi ya dakika 10 kuona mgonjwa, matokeo yake huyu mgonjwa anaweza kuwa misdiagonized. Wengi pia hawana hata hiyo hela ya kumuona daktari au ya vipimo kwa hiyo wengi wetu tunanunua dawa kwenye Maduka ya dawa au tiba mbadala.
- asilimia kubwa hawapati lishe kutokana na umaskini. Kwa baadhi yetu milo mitatu kwa siku tunaisikia kwenye bomba. Kunawanaokosa vyakula vyenye protini kwa vile kundi hili la chakula ni ghali, ukilinganisha na mboga za majani. Maharage yamesaidia sana.
- asilimia kubwa tunategemea mitumba, ikipigwa marufuku tutaumbuka.
- magari pia ni ya mtumba. Wachache sana wananunua magari mapya.
- asilimia kubwa hatuna akiba benki. Vijijini huwa wanaweka akiba ya chakula ndani endapo watavuna vizuri.
- kilimo bado ni cha kizamani. Kazi kubwa mavuno kidogo au kukosa kabisa.
Anayesema hii nchi sio masikini bila shaka hajasoma Development Studies chuoni kwao, hii nchi ina kila dalili za umasikini.
1. Elimu, Tanzania elimu ni ndogo sana. Mwaka 2014 kama sikosei, nilienda pale Ubungo Plaza, alikuwepo Dkt Kitila Mkumbo na mmama flani hivi. Walisema Tanzania ina jumla ya watu milioni 46+ ila wenye degree ni Milion 2 tuu.
2. Afya, hapa sitaki kuzungumzia sana maana kila mmoja anajua ni nini kinaendelea. Magufuli kaenda Muhimbili na kila mtu alisikia kilichotokea, na hii ndo Hospital kuu ya Taifa.
3. Matumizi mabaya ya Rasilimali, angalia meno ya tembo, twiga kupanda ndege n.k
Sitaki hata kuendelea.....
 
TANZANIA HAIPO KATI YA NCHI MASKINI DUNIANI

Kila ninapo soma habari za tanzania nakutana na maelezo kwamba Tanzania ni moja ya nchi maskini sana dunia, miaka nenda rudi bado wanatuita maskini.

Swali ninalo jiuliza kwanini watupangie au kwanini watuite maskini, hii inanikumbusha watu ambao nilikutana nao shuleni ili kuniweka chini yao basi wataniambia sina akili kabisa na mjinga kabisa.

Ukisoma wikipedia kuhusu Tanzania utakutana na sentensi hii (Tanzania is one of the poorest countries in the world)

Baada ya kufanya utafiti nikagundua kutoka ktk kundi hili au kutoka ktk dimbwi la kuitwa maskini ni jukumu letu watanzania, lazima tufike mahali tukatae kwa vitendio na kujua wapi tunatakiwa kuwa.

Nimejaribu kutafuta baadhi ya source nikaona tanzania haipo kati ya nchi kumi za mwisho maskini. Mfano unaweza soma hapa. Top 10 Most Poorest Countries In The World 2015

Lakini pamoja na kuona baadhi ya source zinaitoa Tanzania ktk listi ya nchi maskini nimepata maswali yakujiuliza kama ifutavyo

1. Nani atapigania haki ya tanzania kufutwa kwenye listi ya nchi maskini kama walivyo fanya kenya

2. Kwa nini na sisi wenyewe watanzania tusikatae kuitwa maskini, fikra ambayo inatufanya tufanye mambo kimaskini, wote mmemsikia waziri wa fedha siku chache zilizo pita akisema eti haiwezekani kujenga reli kwa fedha zetu za ndani, hayo ni mawazo ya kimaskini kabisa.

3. Je serikali ina mpango gani wa kujipima yenyewe badala ya kutegemea mashirika ya nje kutupimia vitu kama GDP , etc.

hii vita ya kuukata umaskini inabidi ifanywe kwa umoja na umahili mkubwa , kwa kutangaza Tanzania kama nchi ambayo si maskini kwa kutumia vyombo vyote vya habari kama Internet, forums etc, Kila tunapo taja tanzania lazima tueleze kuwa tanzania si nchi maskini, nchi yenye utajiri mwingi, yenye amani etc

Kwanini turuhusu watu wengine kututangaza kwa ubaya?

Tanzania si nchi maskini wala moja ya nchi maskini.

Nawasilisha
Mkuu nimekusoma hasa masikitiko yako.
Nami nachangia kidogo.
Nataka nikuhakikishie kuwa kuna kila sababu ya kuitwa watu maskini kwa sababu hizi;
Kipato kidogo sana cha watz, elimu duni, miundo mbinu dhaifu, siasa chafu na mengine mengi.
Nataka ni kwambie kuwa ufike wakati tuukubali ukweli huu kuwa sisi ni maskini na ndipo tukae chini tufikiri jinsi ya kujikwamua.
Nimefanikiwa kutembea karibu kila wilaya ya nchi hii, nimeona mengi, watu wana hali mbaya sana, maisha yetu ni duni mno ( nasema yetu coz mm ni mtz ). Mara nyingi hutokwa machozi sana, nimewahi kufika wanakoishi wasonjo na kushuhudia vijana wa miaka 18 wanatembelea kaptula tu bila shati, mabinti wanatembea kifua waz nyonyo nje nje kwa kukosa mavazi, hawajui shule.
Sio hao tu, maisha karibu vijiji vyote tz hali inatisha, sio vijiji pekee hata mijin wengi wanaishi kisanii na kidalali zaidi, kwanini tusiitwe maskini?
 
Wakati mwingine kutiana hamasa ni njia mojawapo ya kujisahaulisha umaskini. Inawezekana mleta mada anaishi mjini, kwa hiyo anafikiri watanzania wote wana viwango vya maisha kama vya watu wa mijini (hata umaskini unaonekana mijini pia). Tusijidanganye, ni kweli kabisa kwamba TANZANIA NI MOJA YA NCHI MASKINI DUNIANI kama huamini funga safari leo nenda vijijini waliko watanzania wengi ukajionee mwenyewe.
Ajahahahahahahahahahaha huku tunaita kutiana moyo.
 
Anayesema hii nchi sio masikini bila shaka hajasoma Development Studies chuoni kwao, hii nchi ina kila dalili za umasikini.
1. Elimu, Tanzania elimu ni ndogo sana. Mwaka 2014 kama sikosei, nilienda pale Ubungo Plaza, alikuwepo Dkt Kitila Mkumbo na mmama flani hivi. Walisema Tanzania ina jumla ya watu milioni 46+ ila wenye degree ni Milion 2 tuu.
2. Afya, hapa sitaki kuzungumzia sana maana kila mmoja anajua ni nini kinaendelea. Magufuli kaenda Muhimbili na kila mtu alisikia kilichotokea, na hii ndo Hospital kuu ya Taifa.
3. Matumizi mabaya ya Rasilimali, angalia meno ya tembo, twiga kupanda ndege n.k
Sitaki hata kuendelea.....
Vitabu mnavyo soma vina matatizo hayo hayo na fikra za kutufanya sisi tuonekane maskini.. mbona wao hawasomi mambo yetu?
 
TANZANIA HAIPO KATI YA NCHI MASKINI DUNIANI

Kila ninapo soma habari za tanzania nakutana na maelezo kwamba Tanzania ni moja ya nchi maskini sana dunia, miaka nenda rudi bado wanatuita maskini.

Swali ninalo jiuliza kwanini watupangie au kwanini watuite maskini, hii inanikumbusha watu ambao nilikutana nao shuleni ili kuniweka chini yao basi wataniambia sina akili kabisa na mjinga kabisa.

Ukisoma wikipedia kuhusu Tanzania utakutana na sentensi hii (Tanzania is one of the poorest countries in the world)

Baada ya kufanya utafiti nikagundua kutoka ktk kundi hili au kutoka ktk dimbwi la kuitwa maskini ni jukumu letu watanzania, lazima tufike mahali tukatae kwa vitendio na kujua wapi tunatakiwa kuwa.

Nimejaribu kutafuta baadhi ya source nikaona tanzania haipo kati ya nchi kumi za mwisho maskini. Mfano unaweza soma hapa. Top 10 Most Poorest Countries In The World 2015

Lakini pamoja na kuona baadhi ya source zinaitoa Tanzania ktk listi ya nchi maskini nimepata maswali yakujiuliza kama ifutavyo

1. Nani atapigania haki ya tanzania kufutwa kwenye listi ya nchi maskini kama walivyo fanya kenya

2. Kwa nini na sisi wenyewe watanzania tusikatae kuitwa maskini, fikra ambayo inatufanya tufanye mambo kimaskini, wote mmemsikia waziri wa fedha siku chache zilizo pita akisema eti haiwezekani kujenga reli kwa fedha zetu za ndani, hayo ni mawazo ya kimaskini kabisa.

3. Je serikali ina mpango gani wa kujipima yenyewe badala ya kutegemea mashirika ya nje kutupimia vitu kama GDP , etc.

hii vita ya kuukata umaskini inabidi ifanywe kwa umoja na umahili mkubwa , kwa kutangaza Tanzania kama nchi ambayo si maskini kwa kutumia vyombo vyote vya habari kama Internet, forums etc, Kila tunapo taja tanzania lazima tueleze kuwa tanzania si nchi maskini, nchi yenye utajiri mwingi, yenye amani etc

Kwanini turuhusu watu wengine kututangaza kwa ubaya?

Tanzania si nchi maskini wala moja ya nchi maskini.

Nawasilisha
"...Tanzania sio nchi fukara ila, kuwa mtu mweusi duniani ni moja ya ufukara wa kudumu"
 
Back
Top Bottom