Tanzania excluded from EAC joint communique

Tanzania excluded from EAC joint communique

Tanzanzaia ifanye kama Switzerland ijitoe na ishughulike na mambo yake yenyewe maana hapa nachoona cycle of repetiton is on the making kama Kenyatta sr alivyofanya kwa Nyerere na Kenyatta jr anarudia yale yale.

Tanzania haijasahau. Lazima kuwa makini na hii project ya EAC
 
kwa sasa nguvu kubwa ni kuikomboa congo na ukoloni wa kagame hawa wengine tutawaangalia baadaye tuwafanye nini.
 
Hatari lakini salama. Ina maana tz haikualikwa au haihusiki na hii miradi?
 
Federation Africa wapi na wapi? Waacheni waende tuone watafika wapi, haina muda mrefu hiyo lazma ivunjike. Ile EAC iliyovunjika Tanzania ndo iliyofanya ikawepo na kilichofanya ivunjike ni Kenya na Uganda. Hao waliojiunga nao watajajutia maamuzi yao baadae. Sisi yetu macho...
 
It is time for our leaders to be real .Time to pull out na Wakenya waje kwa passort na kuomba vibali vya kazi .Sisi hatuna mengi Kenya ila wao wana hata ma Bank hapa .Time for Watanzania kuacha kutumia KBC na bank zingine .JK mimi si mfuasi wa CCM lakini kwenye hili tangaza tuko wote bwana .Hatuwezi kuendeshwa na hawa watu .Wakenya wamezagaa kila kona huku wanapata maisha na investments zao kama Uchumi nk waondoe au walipe kodi haswa maana hatuko katika shirikisho .Wameanza wenyewe tumalizie kwa kishindo .
 
Tuko SADEKI, Sida Hamuna.

Yaani hii inji tungekuwa na akili tungeachana nao kabisa, tujiimarishe na SADC yetu period! Nchi zenyewe njaa tupu watatuambia nini hawa Mburula? Mi nashangaa sana hiui ni mfanyabiashara gani wa Rwanda au Burundi atakubali kupitisha mzigo wake maili zote zile wakati kuna uwezekano wa kupakia Dar na kesho yake yuko KGL AU BUJA? Hapa kikubwa TZ tuboreshe bandari na reli yetu hakika watakuja tu! Ile ya kwao itabaki ya kusafirishia mizigo ya serikali! Mwakyembe umejiandaa?
 
ndio tutie akili, badala ya kukaa kujiibia kila siku tujenge nchi. ili hata tukitengwa tuwe tuweze kujimudu.
 
Hivi si tujitoe tu eac tunapoteza nini mbona ilikuwa haipo hii jumuiya tangu 1977 na tulipeta tu
 
Kama umewahi kuishi na Watutsi hii move ya PK hutaishangaa....Watutsi wafitini sana,kaja mikono nyuma E.A tumempokea,tukampa hifadhi ya wakimbizi,tukamsomeshea vijana wake..sasa kaanza chokochoko...katuulia Profesa wetu Mwaikusa sasa anatuingiza vidole machoni.....
 
Tutasema sana tu, lakini kuumia ndio huko. Kutengwa na jirani yako kuna madhara makubwa tusijifariji. Tutafute sababu na kujisafisha. Tumebweteka kwa kulewa misifa kwa kukalia raslimali na kuwauzia wazungu. Ni laana tuliyoitafuta siku zote. CCM hoyeeeeeee! utuzike salama, maana unaendelea kutujaza ujinga ati bora tule nyasi na kubeba msalaba wake. Tunashikishwa adabu, ina maana hata misimamo ya nchi hii haingwi mkono na majirani zake wote.
 
Kwa hili nemkubali kwamba upeo wa waafrika unashuka kila kukicha. Kama wale watu wanaofikiriwa kuwa Great Thinkers kwa level ya Uraisi wanafanya vitu vya ovyo ovyo kama hivi, vipi watu wa kawaida wanaowachagua. Ninawasiwasi na uwezo wa Kenyatta katika kupambanua mambo ingawaje anaweza kuwa business opportunist lakini kwa muda mfupi tu. Kwani Kagame na Museveni wamemuingiza kingi mapema sana.
 
Kumekucha! TZ yatengwa EAC

Hivi kuna nchi gani East Africa iliyojaza raia wa nchi nyingine Kama TZ. Ukija makanisani wamejaaa tena very manipulative kutwa wanatuchongnisha na wachungaji wetu kwa kujidai wako very loyal to the pastors kuliko mshirika mwingine yoyote hata wamekuwa washauri wakuu makanisani, hasa wakenya (what is the agenda behind!!!). Misikitini ndio usiseme wamejaa tele. Serikalini ndio hivyo, makampuni binafsi na wafanyabiashara. Bidhaa za Kenya zinazouzwa TZ zimejaa nk. Hebu tufanye utafiti ratio ya waTZ walioko kwenye nchi za wenzetu na waliojazana kwetu tuone nani hasa anafaidika na huu umoja.

hawa viongozi wanahitaji Hekima. Moto wanaouwasha sijui Kama ukikolea wataweza kuuzima. Uongozi ni Hekima. Tuwaombee Hekima viongozi wote wa East Africa. Jazba zisitumike ktk kufanya maamuzi. Waathirika ni wananchi na sio viongozi.

TZ ni nchi iliyobarikiwa ina mito, maziwa, madini na mabonde yenye rutuba. Ni waTZ tu kuamka kufanya kazi kwa bidii, kuondokana na ufisadi na ubinafsi nk. Aidha kikubwa kuliko vyote ni kumcha Mungu kwani ndicho chanzo cha maarifa. Then tutakuwa mbali. The only thing we need is the favour of GOD not a man. If God be for us who can be against us. Adui wa nchi yetu ni adui wa MUNGU.

ni wakati wa waTZ kujitambua, kupendana, kuamka na kuwa WAZALENDO ili tuijenge nchi yetu. Kuta zilizobomoka na zijengweeeeee.

Kwa mkono wa BWANA tutatenda MAKUU.

Queen Esther
 
Kenya inajua kuzichezesha kamari hizi nchi aisee.....inawaburuza kama ng'ombe. Mzigo utoke Mombasa hadi Bujumbura, transit of 3 countries???
 
Back
Top Bottom