Tanzania: Dua ya Kuliombea Bunge...

Tanzania: Dua ya Kuliombea Bunge...

Maamuma

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2008
Posts
848
Reaction score
313
Dua ya kuiombea nchi yetu na kuliombea Bunge - husomwa hivi:

"Ewe MWENYEZI MUNGU Mtukufu, Muumba Mbingu na Dunia, Umeweka katika Dunia Serikali za Wanadamu na Mabunge ya Mataifa ili haki yako itendeke.

Twakuomba, uibariki nchi yetu idumishe uhuru, umoja, haki na amani, Umjalie Rais wetu hekima, afya njema na maisha marefu ili pamoja na wanaomshauri, wadumishe utawala bora.

Utuongezee hekima na busara, sisi Wabunge wa Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na utupe uwezo wa kujadili kwa dhati, mambo yatakayoletwa mbele yetu leo, ili tufanye maamuzi sahihi yenye manufaa kwa watu wote na ustawi wa nchi yetu. Amina."
(Msisitizo ni wangu)

Nimekuwa nikisikiliza kwa makini sana dua ya kuliombea Bunge inaposomwa na Spika au Naibu wake. Siku zote nimekuwa na mashaka kama kweli kinachoombwa ndicho hasa kinachohitajika na Wabunge wetu. Pamoja na upungufu uliomo kwenye dua hii nadhani hili la kuomba kuongezewa hekima na busara kwa wabunge haliombwi ipasavyo.

Nijuavyo ni kwamba mtu huongezewa kitu ambacho anacho tayari ila anahitaji nyongeza. Sidhani kama baadhi ya wabunge wetu wana hekima na busara kiasi cha kuhitaji nyongeza. Matokeo yake aliye na hekima huongezewa (kama inavyoombwa) na asiye nayo hapewi (maana hakuna cha kuongeza). Kwa maana hiyo wale wabunge wachache ambao huongezewa hekima na busara huwa wanapishana kwa mbali sana na wale ambao hawana, na hii huleta mgongano na mabishano makubwa yasiyo na tija.

Nimelazimika kusema haya kutokana na hoja ya hivi karibuni ya wabunge kutaka kuongezewa posho. Hivi kweli wabunge wetu, hayo ndio maamuzi sahihi yenye manufaa kwa watu wote na ustawi wa nchi yetu?

Waheshimiwa wabunge, ombeni mjaliwe hekima na busara kama vile anavyoombewa Rais wetu. Ili yule asiye navyo apewe angalau kidogo.

Wakatabahu,

Maamuma.
 
Serikali haina dini, bunge lina dini gani? Hiyo dua huwa wanamuomba mungu aitwaye nani?

Kama tambueni kuwa mungu wamuombaye anaonekana kuwa ni mkuu wa itikadi ya taaluma ya maji marefu mbunge wa korogwe.
 
"ee Mwenyezi Mungu tusaidie tufanye maamuzi kwa manufaa ya watu wote"

Je maamuzi ya Bunge huwa kwa manufaa ya wote??
 
"Umjalie Rais wetu hekima, afya njema na maisha marefu ili pamoja na wanaomshauri, wadumishe utawala bora"

Hii dua ni ya KULIOMBEA BUNGE (read Bunge), Huyu RAIS na washauri wake wanaingiaje tena kwenye dua ambayo ni SPECIFIC kwa BUNGE na WABUNGE?!
 
mkuu kuna mjumbe mmmoja Bukoba aliwahi mapema kupeleka maoni yake katika tume ya katiba na kusema WIMBO WA TAIFA UFUTWE KWA MAANA WIMBO HUU HUWA OMBEA VIONGOZI LAKINI CHA AJABU VIONGOZI HAO NDIO MAFISADI WAKUBWA TENA WALA HAWA WAHURUMII WAWAOMBEAO kwa mantiki hiyo basi naungana na wewe juu ya dua la kuliombea bunge
 
Siku hizi sala au Swala linachukuliwa ni sheria na wala sio imani na unyenyekevu kwa Mungu wetu, kitu muhimu kama bunge alafu muombeaji ni kiongozi wa bunge ambaye ni mtu wa kawaida (kuombea bunge), kwanini wasitoe ajira kwa viongozi wa dini? Nahisi ndo maana vurugu na matusi hayaaishi, nahisi serikali iliangalie hili
 
Jana Msigwa ameingia bungeni na Biblia, mapepo yamepagawa hadi yakaanza kutaja taja neno 'nguruwe'
 
Nasikia kuna profesa mmoja aliseama neno 'Mungu' liondolewe kwenye sala ya bunge kwa kuwa linawabagua wapagani. Ûnaweza kuona? Wakati wenzao Kenya rais anapiga magoti huku tunasema tusitaje Mungu. Mijitu mingine îmelaaniwa kwa laana. Sasa hii nchi itaendeleaje kama tunamkataa Mungu?

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Siku hizi sala au Swala linachukuliwa ni sheria na wala sio imani na unyenyekevu kwa Mungu wetu, kitu muhimu kama bunge alafu muombeaji ni kiongozi wa bunge ambaye ni mtu wa kawaida (kuombea bunge), kwanini wasitoe ajira kwa viongozi wa dini? Nahisi ndo maana vurugu na matusi hayaaishi, nahisi serikali iliangalie hili


Duh mkuu naona una kahoja. Hii kitu inabidi iangaliwe upya lakini sasa kwa kuwa tuna imani nyingi hapa nchini itabidi waajiriwe viongozi wa Budha, Katoliki, Sabato, Islamu, Bahai, nk. Kwa jinsi hiyo huenda suala la sala/swala likachukua nusu saa nzima manake kuna wenzetu wakianza kuomba inabidi wekemee hasa wakiingiwa na roho na kuzanza kunena!
 
MUNGU mwenye rehema tunakuomba utujalie amani na tuishi kwa amani na kila mtu bila ubaguzi
 
Pale bungeni ni unafiki mtupu na ndo maana Mungu amewalaani sasa bunge linaonekana kituko!
 
Sasa wabunge wanataka kuwe na vyuo vya kutongozea, na kuhalalisha Bangi mmmhhh mwisho watakuja kuthibitisha ndoa za jinsia Moja
 
Waajiri wa dini gani?
Na watatumia muda gani wote kuomba?
Na wapagani je? Wakatambike?
 
Kwa tanzania hii ambayo leo hii udini umeota mizizi sijui kama sala hizo zitafanya kazi!! Hiki ndicho kitakachotokea:
  • Wakati Sheikh anasoma dua, wabunge Wakristo watakuwa wanakemea kimya kimya Sheikh ashindwe kwa jina la YESU!
  • Wakati Mchungaji anasoma dua, Waislamu watakuwa wanasema kimya kimya "astaghfurall! astaghfurall!!"
Sasa unazani dua hizo zitapokelewa kweli?
Waacheni hivyo hivyo, wachanane kavu kavu na ikibidi ifike siku hat watiane mikono hadi waheshimiane!
 
:Wasomi wa kiislamu wanasema ni sala ya kikristo....!
 
Dua ya kuiombea nchi yetu na kuliombea Bunge - husomwa hivi:

(Msisitizo ni wangu)

Nimekuwa nikisikiliza kwa makini sana dua ya kuliombea Bunge inaposomwa na Spika au Naibu wake. Siku zote nimekuwa na mashaka kama kweli kinachoombwa ndicho hasa kinachohitajika na Wabunge wetu. Pamoja na upungufu uliomo kwenye dua hii nadhani hili la kuomba kuongezewa hekima na busara kwa wabunge haliombwi ipasavyo.

Nijuavyo ni kwamba mtu huongezewa kitu ambacho anacho tayari ila anahitaji nyongeza. Sidhani kama baadhi ya wabunge wetu wana hekima na busara kiasi cha kuhitaji nyongeza. Matokeo yake aliye na hekima huongezewa (kama inavyoombwa) na asiye nayo hapewi (maana hakuna cha kuongeza). Kwa maana hiyo wale wabunge wachache ambao huongezewa hekima na busara huwa wanapishana kwa mbali sana na wale ambao hawana, na hii huleta mgongano na mabishano makubwa yasiyo na tija.

Nimelazimika kusema haya kutokana na hoja ya hivi karibuni ya wabunge kutaka kuongezewa posho. Hivi kweli wabunge wetu, hayo ndio maamuzi sahihi yenye manufaa kwa watu wote na ustawi wa nchi yetu?

Waheshimiwa wabunge, ombeni mjaliwe hekima na busara kama vile anavyoombewa Rais wetu. Ili yule asiye navyo apewe angalau kidogo.

Wakatabahu,

Maamuma.

chunga sana kitu kinachoitwa kiapo,wabunge wetu wakiapishwa wanashika biblia au quran kama comitment,lakini wanayoyafanya ni kinyume kabisa,unategemea nini hapo kama si "kudata"
 
Tatizo siyo DUA, tatizo liko kwa hao wanaoombewa hiyo DUA maana hata kwenye viapo vyao wanaapa vizuri ila wakisha apa wanasahau kama walisha apa
 
Waajiri wa dini gani?
Na watatumia muda gani wote kuomba?
Na wapagani je? Wakatambike?
Hawa wapagani hawajajiandikisha serekalini,wangejisajili,wakajulikana,ingekwa wepesi kujulikana ni kina nani na wako wapi na wanafanya nini
 
"Ewe MWENYEZI MUNGU Mtukufu, Muumba Mbingu na Dunia, Umeweka katika Dunia Serikali za Wanadamu na Mabunge ya Mataifa ili haki yako itendeke.

Twakuomba, uibariki nchi yetu idumishe uhuru, umoja, haki na amani, Umjalie Rais wetu hekima, afya njema na maisha marefu ili pamoja na wanaomshauri, wadumishe utawala bora.

Utuongezee hekima na busara, sisi Wabunge wa Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na utupe uwezo wa kujadili kwa dhati, mambo yatakayoletwa mbele yetu leo, ili tufanye maamuzi sahihi yenye manufaa kwa watu wote na ustawi wa nchi yetu. Amina."

Kwa tabia wanazofanya Wabunge wetu Dua hizi hupokelewa na Mungu kweli??!!!
 
Back
Top Bottom