Tanzania: Deni la Taifa lafikia trilion 116

Tanzania: Deni la Taifa lafikia trilion 116

Umekopa kwa dollar utalipa kwa dollar,unapochelewa ndivyo deni linaendelea flactuate
Duh bas tutakua sana watumwa wa hili deni provided shilingi yetu inaendelea kufanya vbaya(kuporomoka) dhidi ya dola
 
Tanzania imefikia deni la taifa la trilioni 116 (dola za Marekani bilioni 46.6) hadi Juni 2025, likiongezeka kwa asilimia 1 ukilinganisha na Mei. Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ilieleza kuwa deni la nje linachangia asilimia 70.7 ya jumla, huku deni la umma likiwa sehemu kubwa zaidi kwa asilimia 85.4. Malipo ya huduma ya deni la nje mwezi Juni yalifikia dola milioni 234.4, yakihusisha marejesho ya mkopo na riba.

Kwa upande wa ndani, deni lilikuwa trilioni 35.5, likiongezeka kwa asilimia 0.9 kutokana na hati mpya za dhamana. Uchambuzi wa IMF unaonyesha deni la umma ni asilimia 35 ya Pato la Taifa, chini ya kiwango cha hatari, ingawa kushuka kwa thamani ya shilingi dhidi ya dola kumeongeza mashaka juu ya mzigo wa deni.

Wachambuzi wanasema ingawa deni ni kubwa, bado linaweza kudhibitiwa iwapo mazingira ya sasa ya kiuchumi yataendelea.

Saidia fundi

View attachment 3452298
Achana na kauli ya wachambuzi(Madalali) kudai eti linadhibitika, siyo kweli maana hatuoni mpango wowote wa deni kulipika.Kilicho dhahiri ni kuwa deni linaongezeka kwa sababu tunaendelea kukopa kwa matumizi ya kawaida.
Zingatia walichosema IMF kwamba mzigo unazi kutuelemea.Tanganyika inabeba mzigo wa Mafisadi Papa na sasa ndiyo washauri wa SSH.
 
Wakati anachukua Nchi kuongoza kama Rais wa awamu ya Sita baada ya Kifo cha JPM, deni lilikuwa Trilioni 62.

Miaka yake minne, deni limefika Trilioni 116

Ni ongezeko la Trilioni 54 ndani ya miaka 4

Ukifanya Hesabu za kutoa na Kujumlisha, ni wastani wa kukopa shilingi Trilioni 13.5 Kila Mwaka 🙌

Anyways, Mchumi wetu, Daktari Mwigulu Nchema hakawii kusema deni ni himilivu, kwahiyo angependa tuendelee kukopa 😜
Zitto Kabwe yule aliekuwa anapiga makelele enzi Magu yupo?

Mbona hili hasemi au kwa vile salamaleko mwenzie?
 
Deni kubwaaa au ndio maana serikali inalipa mishara kwa awamu maana hadi Leo baadhi ya wafanyakazi hawajapata mshahara!
 
Zitto Kabwe yule aliekuwa anapiga makelele enzi Magu yupo?

Mbona hili hasemi au kwa vile salamaleko mwenzie?
Zitto hawezi kusema hili, tayari mrija wake wa kula Keki ya Taifa haujaguswa

Kingine, aliyepo ni ndugu yake katika Imani
 
Mbona ghafla bini vuu..
October hakikisha unatiki, sijui utatiki nini we tiki tu itajulikana hukohuko..
 
Back
Top Bottom