Tanzania: Deni la Taifa lafikia trilion 116

Tanzania: Deni la Taifa lafikia trilion 116

didy muhenga

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2022
Posts
2,055
Reaction score
3,436
Tanzania imefikia deni la taifa la trilioni 116 (dola za Marekani bilioni 46.6) hadi Juni 2025, likiongezeka kwa asilimia 1 ukilinganisha na Mei. Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ilieleza kuwa deni la nje linachangia asilimia 70.7 ya jumla, huku deni la umma likiwa sehemu kubwa zaidi kwa asilimia 85.4. Malipo ya huduma ya deni la nje mwezi Juni yalifikia dola milioni 234.4, yakihusisha marejesho ya mkopo na riba.

Kwa upande wa ndani, deni lilikuwa trilioni 35.5, likiongezeka kwa asilimia 0.9 kutokana na hati mpya za dhamana. Uchambuzi wa IMF unaonyesha deni la umma ni asilimia 35 ya Pato la Taifa, chini ya kiwango cha hatari, ingawa kushuka kwa thamani ya shilingi dhidi ya dola kumeongeza mashaka juu ya mzigo wa deni.

Wachambuzi wanasema ingawa deni ni kubwa, bado linaweza kudhibitiwa iwapo mazingira ya sasa ya kiuchumi yataendelea.

Saidia fundi

Screenshot_20250825_113032_LinkedIn.jpg
 
Deni la Chadema ,CCM kwenye deni haipo hata kidogo utafikiria na hawaliambatanishi na Rais Samia kuwa Deni na lake huku wakiuza migodi kama vile nchi ni yao duuu NIDA yangu nimeificha mwenyewe leo nasikia wanayo CCM wala sio TRA and INEC kimeniuma sana
 
Wakati anachukua Nchi kuongoza kama Rais wa awamu ya Sita baada ya Kifo cha JPM, deni lilikuwa Trilioni 62.

Miaka yake minne, deni limefika Trilioni 116

Ni ongezeko la Trilioni 54 ndani ya miaka 4

Ukifanya Hesabu za kutoa na Kujumlisha, ni wastani wa kukopa shilingi Trilioni 13.5 Kila Mwaka 🙌

Anyways, Mchumi wetu, Daktari Mwigulu Nchema hakawii kusema deni ni himilivu, kwahiyo angependa tuendelee kukopa 😜
 
Wakati anachukua Nchi kuongoza kama Rais wa awamu ya Sita baada ya Kifo cha JPM, deni lilikuwa Trilioni 62.

Miaka yake minne, deni limefika Trilioni 116

Ni ongezeko la Trilioni 54 ndani ya miaka 4

Ukifanya Hesabu za kutoa na Kujumlisha, ni wastani wa kukopa shilingi Trilioni 13.5 Kila Mwaka 🙌

Anyways, Mchumi wetu, Daktari Mwigulu Nchema hakawii kusema deni ni himilivu, kwahiyo angependa tuendelee kukopa 😜
imagine anapewa mitano mengine🤣🤣🤣
 
R
Tanzania imefikia deni la taifa la trilioni 116 (dola za Marekani bilioni 46.6) hadi Juni 2025, likiongezeka kwa asilimia 1 ukilinganisha na Mei. Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ilieleza kuwa deni la nje linachangia asilimia 70.7 ya jumla, huku deni la umma likiwa sehemu kubwa zaidi kwa asilimia 85.4. Malipo ya huduma ya deni la nje mwezi Juni yalifikia dola milioni 234.4, yakihusisha marejesho ya mkopo na riba.

Kwa upande wa ndani, deni lilikuwa trilioni 35.5, likiongezeka kwa asilimia 0.9 kutokana na hati mpya za dhamana. Uchambuzi wa IMF unaonyesha deni la umma ni asilimia 35 ya Pato la Taifa, chini ya kiwango cha hatari, ingawa kushuka kwa thamani ya shilingi dhidi ya dola kumeongeza mashaka juu ya mzigo wa deni.

Wachambuzi wanasema ingawa deni ni kubwa, bado linaweza kudhibitiwa iwapo mazingira ya sasa ya kiuchumi yataendelea.

Saidia fundi

View attachment 3452298
Hadi April 2021 deni la taifa lilikuwa trilioni 60.9 kwa mujibu wa Waziri wa Fedha Mwigulu akinukuliwa na Ayo Media.
Maana yake baada ya hapo ongezeko ni la Mama
 
Back
Top Bottom