masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 17,882
- 13,172
Kwa gazeti lililojipatia sifa hapa nchini Tanzania Daima inaelekea halina sifa za watu makini hasa kwenye uhariri na uchambuzi wa habari.
Mimi ni msomaji mzuri sana wa habari karibu zote na hata maoni ya wahariri na nina tabia ya kuwapigia simu waandishi au wahariri wa karibu vyombo vyote ninapoona msimamo au habari haina ukweli au inakinzana na uchambuzi wa habari yenyewe.
Leo tar 5 April katika maoni ya Tz Daima kuna Tahriri inayosema "Serikali iwafukuze wamachinga kwa kuwapa maeneo mbadala".
Nikampigia simu mhariri wa habari kwa simu iliyoainishwa gazetini mwao,(jina,simu na namba siitaji).
Nikampa maoni yangu kuwa
Majibu niliyopata hapo ya kusikitihsha kwa mtu ambaye anapaswa kujua kukubali au kutokubali maoni.Yakaanza matusi na shutuma kuwa "nyie watu wa system ndio mnaua nchi, mmefeli kuendesha nchi, mjinga we usinipigie tena, na mimi nimesafiri huko ulaya na ninajua"
It was no use.
Baada ya hapo nikamwambia asante ndugu
Akanijibu usinipigie tena.
Ndio Tanzania Daima -Sauti ya Watu
Mimi ni msomaji mzuri sana wa habari karibu zote na hata maoni ya wahariri na nina tabia ya kuwapigia simu waandishi au wahariri wa karibu vyombo vyote ninapoona msimamo au habari haina ukweli au inakinzana na uchambuzi wa habari yenyewe.
Leo tar 5 April katika maoni ya Tz Daima kuna Tahriri inayosema "Serikali iwafukuze wamachinga kwa kuwapa maeneo mbadala".
Nikampigia simu mhariri wa habari kwa simu iliyoainishwa gazetini mwao,(jina,simu na namba siitaji).
Nikampa maoni yangu kuwa
- kimsingi biashara ya machinga ni ukiukwaji wa ulipaji kodi
- kwamba kutafutiwa sehemu nyingine ni swala lisilowezekana, kama ilivyo machinga complex
- kwamba vitu vyote vinavyouzwa na machinga vimeagizwa nje na machinga ni outlet ya kutolipa kodi
Majibu niliyopata hapo ya kusikitihsha kwa mtu ambaye anapaswa kujua kukubali au kutokubali maoni.Yakaanza matusi na shutuma kuwa "nyie watu wa system ndio mnaua nchi, mmefeli kuendesha nchi, mjinga we usinipigie tena, na mimi nimesafiri huko ulaya na ninajua"
It was no use.
Baada ya hapo nikamwambia asante ndugu
Akanijibu usinipigie tena.
Ndio Tanzania Daima -Sauti ya Watu