Tanzania Bustani ya Edeni

Tanzania Bustani ya Edeni

Clemence Mwandambo

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2018
Posts
1,384
Reaction score
1,438
TANZANIA BUSTANI YA EDENI

Ndugu zangu Mimi Clemence Kenan Mwandambo najisikia raha kuzaliwa Tanzania, Bustani ya Edeni, nchi ambayo ni mwanzo wa kuumbwa kwa ulimwengu. Ebu tafakari hili.

Kanisani wanasema mtu wa kwanza aliitwa Adam, aliishi kwenye bustani ya Edeni na hapo Ndipo Mungu kwa mara ya kwanza alizungumza na mwanadamu. Na niliposoma vitabu vya historia, vinasema fuvu la mtu wa kale liligundulika TANZANIA, Ndipo nilipotafakari! Hah hivi si mtu wa kale ni adam?

Kumbe fuvu la Adamu liligundulika Tanzania, Oldivai Georgie, nchini Tanzania.
Kumbe nimekanyaga nchi uliyoishi Adamu, kumbe nimezaliwa kwenye bustani ya Edeni? Mahala ambapo Mungu alizungumza na Adamu? Kumbe nina bahati kuzaliwa Tanzania, nchi takatifu, nchi ya Adamu na Eva.

Hiyo ndiyo bahati tuliyonayo watanzania, hatuna sababu ya kuwa wanyonge, tunahitaji kusonga mbele katika imani, tubadirike, tuiambie dunia, na Dunia itetemeke, tuwafundisha watoto wetu kuanzia chekechea mpaka chuo kikuu, tujibland, tuonekane hivyo, watalii wakamiminike, waione nchi aliyoishi Adamu.

Wote tukanene hilo kuanzia raisi wa nchi mpaka mwananchi wa kawaida. Watu waione Tanzania tofauti, tujione hivyo na tukaonekane hivyo.

WATU WOTE WENYE MAPENZI MEMA MUKANIUNGE MKONO KATIKA KAMPENI HII TUINADI NCHI YETU. NA KILA MZALIWA WA TAIFA HILI AKAJIVUNE KUWA MTANZANIA.
0755068357/0653068355
 
Nabii Hebron kayaongelea sana haya mambo tangu 2010's
 
Mbona ni kinyume chake kwani ni nchi ya wapiga dili na blaablaa tu ! Labda JPM afungue njia na kuonyesha ulinwengu kuwa bustani ya Eden ilikuwa TZ .
 
Kwa hiyo Adamu na Eve walipotimuliwa Eden walirudi kwa mlango wa nyuma na kuendelea kuisha hapo mpaka waliaga dunia.
 
Jivunie nchi yako , sawa ila swala la blaablaa na upigaji dili ni tatizo mf. Ukinunua wembe wa Tz sh 200 ni butu ila wa Kenya kwa pesa ileile ni mkali kiasi unaondoka na ngozi , ninunue wa nchi yangu au Kenya ? Yote hayo ni dili na blaablaa
 
Back
Top Bottom