Tanzania: Bei ya mafuta yapanda!

hivi ulishawahi jiuliza kwa nini tz dola inapanda sana kuliko kushuka maana huu ni mwezi wa Sita tokea iwe 1500/$...

Je tatizo ni nini hasa na unataka nini kifanyike ili hii hali tuikwepe?

usiku mwema..
Mkuu ndetichia, kapfo mangi, mbonyi tsa mfiri?
Kwa mawazo yangu tu serikali ingetenga mfuko wa ruzuku kwa hii bidhaa, pindi bei inapokwenda juu watukinge na maumivu sisi wananchi, mafuta yana muitikio mkubwa sana kwa uchumi wa nchi na maisha kiujumla. Shilingi yetu nayo inateketea kila kukicha shauri ya mlinganyo wa biashara ya ndani na nje ya nchi, naona upande wa ndani umeelemewa zaidi. Pia ni wakati mzuri kuanzisha soko la minada ya mazao (commodity exchange market).
 
tusio na magari raha, labda ninywe ya buku tano tu.

mafuta yakipanda, shughuli nyingine za kiuchumi zinazotegemea nishati hiyo huthaminika zaidi pia...kwa hiyo konnie hata sisi TZ 11 tutazidi kufulia tu
 
Kuna kitu kimoja sikjui kama utekelezaji wake ulianza, kama kumbukumbu zangu zipo sawa nakumbuka serikali ilihaidi baada ya miezi mitatu(hiyo nadhani ilikuwa mwaka jana mwishoni au mwaka huu mwanzoni), serikali itakuwa ikiagiza mafuta badala ya kutumia makampuni...Hivi hii ishu imeanza utekelezaji? maana walisema ikianza bei itadrop tremendously
 
Kuna kitu kimoja sikjui kama utekelezaji wake ulianza, kama kumbukumbu zangu zipo sawa nakumbuka serikali ilihaidi baada ya miezi mitatu(hiyo nadhani ilikuwa mwaka jana mwishoni au mwaka huu mwanzoni), serikali itakuwa ikiagiza mafuta badala ya kutumia makampuni...Hivi hii ishu imeanza utekelezaji? maana walisema ikianza bei itadrop tremendously
 
Asubuhi nshapita vituo kama vitatu hivi vya Mafuta vikiwepo Victoria pale,Sayansi na hiki cha hapa Leaders ni wananambia hakuna mafuta ghafla nlipatwa na waswasi na kuhisi lazima watakuwa wameficha mafuta n ahapa sasa napigia mstari fikra zangu, hii ni hatari kwakweli.
 
Mwezi Mei: zilipungua: Petroli imepungua kwa TZS 48/lita sawa na asilimia (2.16); Dizeli imepungua kwa TZS 54/lita sawa na asilimia (2.59)


Mwezi Juni zikaongezeka: Petroli imeongezeka kwa Sh 6/lita sawa na asilimia 0.26; Dizeli imeongezeka kwa Sh 37/lita sawa na asilimia 1.82.

Mwezi Julai zikapungua: Petroli imepungua kwa TZS 9/lita sawa na asilimia 0.41; Dizeli imepungua kwa TZS 42/lita sawa na asilimia 2.02; na Mafuta ya Taa imepungua kwa TZS 40/lita sawa na asilimia 1.94

Mwezi Agosti zikapungua: Petroli TZS 170/lita sawa na asilimia 7.81; Dizeli TZS 98/lita sawa na asilimia 4.81; na Mafuta ya Taa TZS 102/lita sawa na asilimia 5.05.

Source: EWURA - Energy & Water Utilities Regulatory Authority of Tanzania

Mwezi Septemba, zikaongezeka: Petroli TZS 291/lita sawa na asilimia 14.50; Dizeli TZS 199/lita sawa na asilimia 10.26; na Mafuta ya Taa TZS 67/lita sawa na asilimia 3.47.
 
[h=3][/h]

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli nchini ambapo bei ya petroli, dizeli na mafuta ya taa zimepanda.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Meneja Uhusiano wa Ewura, Titus Kaguo jana bei mpya zitaanza kutumika kuanzia leo.
"Sambamba na kupanda kwa gharama halisi za uagizaji wa mafuta kutoka kwenye Soko la Dunia, bei za jumla na rejareja kwa mafuta aina zote zimebadilika ikilinganishwa na taarifa iliyopita ya Agosti 1, 2012," ilieleza taarifa hiyo.
Kaguo katika taarifa hiyo alieleza kuwa bei za rejareja kwa Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa zimeongezeka, ambapo Petroli imepanda kwa Sh 291 kwa lita sawa na asilimia 14.50; Dizeli Sh 199 kwa lita sawa na asilimia 10.26; na Mafuta ya Taa Sh 67 kwa sawa na asilimia 3.47.
"Bei za jumla kwa kulinganisha matoleo haya mawili zimebadilika kama ifuatavyo: Petroli imeongezeka kwa Sh 291.54 kwa lita sawa na asilimia 15.07; Dizeli Sh 199.57 kwa lita sawa na asilimia 10.68 na mafuta ya taa kwa Sh 67.29 kwa lita sawa na asilimia 3.63," aliseleza katika taarifa hiyo.
Alisema kampuni za mafuta zipo huru kuuza bidhaa za mafuta ya petroli kwa bei ya ushindani ilimradi bei hizo ziko chini ya bei kikomo kama ilivyokokotolewa na kanuni mpya iliyopitishwa na Ewura na kuchapwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 454 la Desemba 23, 2011.
 
ili ni balaa lingine niloamka nalo leo!!
ivi serikali ya magamba si ilisema inairudisha ile TPD nini/kampuni ya mafuta au ruzuku ya serikali?
kipidni kile cha makampuni private yalipogoma...lilifikia wapi lile swala
 
hao jamaa nawafananisha na mbweha tu..sijawahi kuelewa wanafanya kazi kwa manufaa ya nani, ni mwisho wa mwezi wa nane nchi za africa mashariki zimeshusha bei za mafuta ikiwemo kenya na rwanda, sasa sijui bei wanazodai zimepanda kwenye soko la dunia ni zipi tena; naona bora warudishe mfumo wa zamani kila mtu ajue ata source wapi hiyo black gold ya mwarabu...
 
Kwani kazi yao kubwa ni kuzuia bei na kuhakikisha ubora wa mafuta au business as usual?
 

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli nchini ambapo bei ya petroli, dizeli na mafuta ya taa zimepanda.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Meneja Uhusiano wa Ewura, Titus Kaguo jana bei mpya zitaanza kutumika kuanzia leo.
"Sambamba na kupanda kwa gharama halisi za uagizaji wa mafuta kutoka kwenye Soko la Dunia, bei za jumla na rejareja kwa mafuta aina zote zimebadilika ikilinganishwa na taarifa iliyopita ya Agosti 1, 2012," ilieleza taarifa hiyo.
Kaguo katika taarifa hiyo alieleza kuwa bei za rejareja kwa Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa zimeongezeka, ambapo Petroli imepanda kwa Sh 291 kwa lita sawa na asilimia 14.50; Dizeli Sh 199 kwa lita sawa na asilimia 10.26; na Mafuta ya Taa Sh 67 kwa sawa na asilimia 3.47.
"Bei za jumla kwa kulinganisha matoleo haya mawili zimebadilika kama ifuatavyo: Petroli imeongezeka kwa Sh 291.54 kwa lita sawa na asilimia 15.07; Dizeli Sh 199.57 kwa lita sawa na asilimia 10.68 na mafuta ya taa kwa Sh 67.29 kwa lita sawa na asilimia 3.63," aliseleza katika taarifa hiyo.
Alisema kampuni za mafuta zipo huru kuuza bidhaa za mafuta ya petroli kwa bei ya ushindani ilimradi bei hizo ziko chini ya bei kikomo kama ilivyokokotolewa na kanuni mpya iliyopitishwa na Ewura na kuchapwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 454 la Desemba 23, 2011.

Poleni wenye Kilimo kwanza V8 mi na ki Vitz changu hainiumiz sana ndio Tz yetu jamani
 
hayo ndo maisha bora kwa kila mtanzania....

Ari zaidi, kasi zaidi na nguvu zaidi........

Wamethubutu, wameweza, wanazidi kusonga mbele kwa kutunyonga.......
 
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli nchini ambapo bei ya petroli, dizeli na mafuta ya taa zimepanda.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Meneja Uhusiano wa Ewura, Titus Kaguo jana bei mpya zilianza kutumika kuanzia jana (yaani 05 Septemba 2012)

"Sambamba na kupanda kwa gharama halisi za uagizaji wa mafuta kutoka kwenye Soko la Dunia, bei za jumla na rejareja kwa mafuta aina zote zimebadilika ikilinganishwa na taarifa iliyopita ya Agosti 1, 2012," ilieleza taarifa hiyo. Kaguo katika taarifa hiyo alieleza kuwa bei za rejareja kwa Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa zimeongezeka, ambapo:-

Petroli imepanda kwa Sh 291 kwa lita sawa na asilimia 14.50
Dizeli Sh 199 kwa lita sawa na asilimia 10.26;
Mafuta ya Taa Sh 67 kwa sawa na asilimia 3.47.

Bei za jumla kwa kulinganisha matoleo haya mawili zimebadilika kama ifuatavyo:

Petroli imeongezeka kwa Sh 291.54 kwa lita sawa na asilimia 15.07
Dizeli Sh 199.57 kwa lita sawa na asilimia 10.68
Mafuta ya taa kwa Sh 67.29 kwa lita sawa na asilimia 3.63

Kwa mtizamo wangu najaribu kuyaangalia maisha ya watanzania wengi walioko mjini na vijijini kwamba kwa hali hii ni vipi watajikwamua kwenye lindi la ugumu wa maisha - kwa vyovyote nauli zitapanda hata kama sio rasmi lakini wenye vyombo vya usafirishaji hawatabeaba mzigo huu bali watautupia kwa mlaji wa mwisho - bei za bidhaa mbali mbali zinazosafirishwa kutoka point moja kwenda nyingine zitapanda tu - hivyo watanganyika wengi itawalazimu kubadili staili za maisha ikiwemo badili Menyu ambapo labda itazimika kugonga chai asubuhi - mchana ukautazamu tu - halafu usiku kugonga posho ili kuepuka kuota njozi za mauzauza.

Kiwango cha upandaji wa mafuta kwa kipindi hiki ni kikubwa tangu ambapo nimekuwa nikufuatilia upandaji na ushukaji wa bei ya mafuta. NINACHOOMBA WANA JF:

a) Je upandaji huu wa mafuta ni kutokana na bei ya mafuta kupanda nje? au shillingi yetu kuwa hoi.
b) Je serikali imekosa kabisa namna ya kuokoa jahazi juu ya hili? au kuna watu wafaidika na upandaji huu
c) Kwa staili hii mbio ya kiranja mkuu "Maisha bora kwa kila Mtanznia" nini maana yake

Nawakilisha
 
Wanabodi,

Najaribu kutafakari Hawa jamaa wa Ewura vigezo wanavytumia Kubadili Bei ya Mafuta Kila Mwezi.

Naomba ieleweke kuwa Mimi hapa silalamiki kwasababu Bei imepanda, Hata Pia ingeshuka kwa kiwango Cha Tshs 291 kwa lita kama ilivyopanda sasa lazima ningejiuliza maswali tena mengi.

Mwanzo Nilifikiri wazo la 'BULK BUYING' Lingepunguza gharama kwa waagizaji kwahiyo mafuta yangeshuka bei lakini mambo yamekua tofauti kabisa na matarajio yangu.

Hatuwezi kulinganisha ''INFALTION RATE'' na ''RATE'' ya kubadilika kwa bei ya mafuta. naona havina uwiano kabisa. hapa EWURA mnatuburuza.

Hivi kweli EWURA hakuna maslahi binafsi yanawapa msukumo katika upangaji wa hizi bei?


10,000/= you get four litres of petrol, with the current traffic jam in Dar? This is all Bullshit!!!!!!!!!!!
 
Wanabodi,

Najaribu kutafakari Hawa jamaa wa Ewura vigezo wanavytumia Kubadili Bei ya Mafuta Kila Mwezi.

Naomba ieleweke kuwa Mimi hapa silalamiki kwasababu Bei imepanda, Hata Pia ingeshuka kwa kiwango Cha Tshs 291 kwa lita kama ilivyopanda sasa lazima ningejiuliza maswali tena mengi.

Mwanzo Nilifikiri wazo la 'BULK BUYING' Lingepunguza gharama kwa waagizaji kwahiyo mafuta yangeshuka bei lakini mambo yamekua tofauti kabisa na matarajio yangu.

Hatuwezi kulinganisha ''INFALTION RATE'' na ''RATE'' ya kubadilika kwa bei ya mafuta. naona havina uwiano kabisa. hapa EWURA mnatuburuza.

Hivi kweli EWURA hakuna maslahi binafsi yanawapa msukumo katika upangaji wa hizi bei?


10,000/= you get four litres of petrol, with the current traffic jam in Dar? This is all Bullshit!!!!!!!!!!!

so hurting. jikaze mwanaume
 
tusio na magari raha, labda ninywe ya buku tano tu.


we unaishi nchi gani? hujui bei ya mafuta inaathiri sana gharama za usafirshaji wa bidhaa na kufanya bidhaa zipande bei? Hujui pia nauli ya mabasi na daladala itapanda pia? Ni kweli huna gari, Je bidhaa za madukani na sokoni hutanunua? Je hutasafiri kwa gari au pikipiki?
Ukweli ni kwamba Hakuna anayepona pale ambapo bei ya mafuta inapanda. Tena wanaoumia zaidi ni watu wa kipato cha chini.
Please think beyond the black box. Badilika tafadhali.
 
Wakuu hapo ni wazi kabisa EWURA wanakula dili na wauzaji wa mafuta kupanga hizi bei mbona nchi nyingine za jirani bei zao haziongezeki kienyeji hivi?
 
Back
Top Bottom