Tanzania bado japo sio mbali tena

Shocker

JF-Expert Member
Sep 15, 2012
1,930
3,803
Kuhusu maandamano na uwajibikaji wa wananchi katika kuiwajibisha Serikali au kupinga jambo wakiwa kama waTanzania kwa ujumla wao,hizi za kina Chadema na ACT Wazalendo na wengine kama wapo ni mwanzo ulio mbali na hali halisi inavyokuwa, Tanzania hatujakumbwa na baa la njaa ya kufa mtu, Tanzania haijakosa hela ya kulipa mishahara na mambo mengi ambayo yanawagusa wananchi wote kwa ujumla wao

Sasa ikiwa hali inayofanywa na CCM itaendelea kuteka uchaguzi na mataifa yanayoisaidia Tanzania kuona misaada yao inaishia njiani na watakaposimama kikamilifu kutoa hata ndururu kulisaidia bunge na serikali basi hapo joto la shida na kulipana mishahara litakuwa juu na kumgusa kila mtu na kutakuwa hakuna tena kuoneana aibu na kuvumiliana.

Kuwekewa vikwazo vya uchumi ni jambo hatari sana hasa kwa dunia ya leo ambapo nchi zinategemeana kwa shida na furaha,Tanzania hatujawahi kuwekewa jambo hilo,ikiwa nchi tajiri zikiwekewa vikwazo zinayumba itakuja kuwa Tanzania.

Ukiwekewa vikwazo hata Mwenyezi Mungu anaviongeza vikwazo,muhogo hauoti wala mvua hazipo inakuwa ni mswalie mtume tu,sana sana tutatumia akiba kwa miaka miwili mitatu na kufunga mkaja lakini kila siku inakuwa ngumu,vikwazo ni hatari kwa serikali,serikali nyingi huanguka.

Ipo kujikaza kuwa tutavuka lakini sio rahisi kama mnavyosema,chukulia serikali inakosa hela ya kulipa mishahara kwa muda wa miezi sita tu basi vumbi lake sio dogo, tutaanza kubeba hela kwenda sokoni kwa mikokoteni.
 
Ungetulia ukaandika kwa utulivu nadhani unayo pointi.
Ila kwa sasa wapinzani waliokuwa wanakwamisha maendeleo sasa hawapo, watakao kwamisha maendeleo kwa sasa ni "wadhungu".
Ushindi wa kishindo upo sambamba na anguko la kishindo.
Wacha wawe mbwa leo kwa kubweka lakini kesho ijayo ccm itaanza kumlinda mbwa, ambaye habweki.
 
Endeleeni kuwaza vikwazo tu
Na hata mkilala oteni ndoto za vikwazo
Upo sawa kabisa kwa sasa hizi ni ndoto,ndoto ambazo hazipo mbali,hizi sio ndoto za Tanzania ya viwanda kwamba baada ya miaka mitano tutakuja na uongo mwengine wa miundo mbinu.

Ndoto hii ipo na ipo kweli pale tu shida itakapochukua mkondo wake hata kwa afande Siro,pale tu shida itakapochukua mkondo wake kwa Mkuu Mabeyo na wengine wengi ,ndio hapo ndoto itakapokaribia kuwa kweli,usitegemee itakuja kama uyoga na kufa kama uyoga.

Ndio nikasema tusiombee mambo ya vikwazo,ipo haja ya kuweka mikakati ya kuepuka jambo hilo,hivi kuna ugumu gani wa kuweka tume iliyo huru ya uchaguzi inayoheshimika ? tatizo na shida zipo wapi ? Kuna shida gani kuzuia wasimamizi kuja kushuhudia uchaguzi wetu ?

Umeona tumewazuia kuja lawama zimevuka mipaka pengine wangelikuja wangeweza kusema turekebishe makosa.

Hakuna ulazima kwamba ni lazima mtu huyu ashinde,hivi ndani ya CCM hakuna wabunge,kama ambavyo wananchi waliwachagua kutoka huko vijijini,mnawabadilishia nini ?

Ilivykuwa ndani ya CCM yenyewe hakuna uhuru wa kuamua nani awe mbunge wetu ndio hivyohivyo kwenye kuendesha uchaguzi,ile kusema tuna taratibu zetu hizo ni sababu za kijinga ukilinganisha na mchakato wa awali wananchi walete majina ya wanaowataka,wameleta unasema huyu sie tunamuweka huyu,huko ni kufanyana wajinga.

Nikirudi ni hii ndoto ya vikwazo hii ndoto ikitimia tutakuwa hatarini kuliko tunavyofikiria ,wala siombei ni kitu kimoja ambacho kitaidhoofisha nchi na kuirudisha nyuma kabisa

Wewe fikiria tu ukisusiwa kuuziwa mafuta,utafanya nini ? Utatafuta black market au sivyo na ndio hivyo kwa bidhaa zote gharama atazibeba mlaji au mtu wa mwisho end user.

sasa serikali haina hela ya kulipa mishahara ,hakuna inachouza nje ili kupata hela ya kigeni itakubidi ushushe thamani na uprint noti ya milioni moja.

We wacha tu hili janga la vikwazo lipite mbali sana na nchi yetu.
 
Upo sawa kabisa kwa sasa hizi ni ndoto,ndoto ambazo hazipo mbali,hizi sio ndoto za Tanzania ya viwanda kwamba baada ya miaka mitano tutakuja na uongo mwengine wa miundo mbinu.

Ndoto hii ipo na ipo kweli pale tu shida itakapochukua mkondo wake hata kwa afande Siro,pale tu shida itakapochukua mkondo wake kwa Mkuu Mabeyo na wengine wengi ,ndio hapo ndoto itakapokaribia kuwa kweli,usitegemee itakuja kama uyoga na kufa kama uyoga.

Ndio nikasema tusiombee mambo ya vikwazo,ipo haja ya kuweka mikakati ya kuepuka jambo hilo,hivi kuna ugumu gani wa kuweka tume iliyo huru ya uchaguzi inayoheshimika ? tatizo na shida zipo wapi ? Kuna shida gani kuzuia wasimamizi kuja kushuhudia uchaguzi wetu ?

Umeona tumewazuia kuja lawama zimevuka mipaka pengine wangelikuja wangeweza kusema turekebishe makosa.

Hakuna ulazima kwamba ni lazima mtu huyu ashinde,hivi ndani ya CCM hakuna wabunge,kama ambavyo wananchi waliwachagua kutoka huko vijijini,mnawabadilishia nini ?

Ilivykuwa ndani ya CCM yenyewe hakuna uhuru wa kuamua nani awe mbunge wetu ndio hivyohivyo kwenye kuendesha uchaguzi,ile kusema tuna taratibu zetu hizo ni sababu za kijinga ukilinganisha na mchakato wa awali wananchi walete majina ya wanaowataka,wameleta unasema huyu sie tunamuweka huyu,huko ni kufanyana wajinga.

Nikirudi ni hii ndoto ya vikwazo hii ndoto ikitimia tutakuwa hatarini kuliko tunavyofikiria ,wala siombei ni kitu kimoja ambacho kitaidhoofisha nchi na kuirudisha nyuma kabisa,
Wewe fikiria tu ukisusiwa kuuziwa mafuta,utafanya nini ? Utatafuta black market au sivyo na ndio hivyo kwa bidhaa zote gharama atazibeba mlaji au mtu wa mwisho end user.
sasa serikali haina hela ya kulipa mishahara ,hakuna inachouza nje ili kupata hela ya kigeni itakubidi ushushe thamani na uprint noti ya milioni moja.

We wacha tu hili janga la vikwazo lipite mbali sana na nchi yetu.
Wananchi wamewanyima kura mmebaki kuweweseka kuilaumu tume ya uchaguzi. HUU NI UJUHA WA KIWANGO CHA 5G
 
Back
Top Bottom