MWANALUGALI
JF-Expert Member
- Feb 1, 2010
- 601
- 34
Natangaza kuwa nitafanya maandamano ya amani siku ya jumanne tarehe11.1.11 kuanzia saa nane mchana kupinga serikali kuilipa Dowaans mabilioni ya fedha ambazo ni za udanganyifu! sihitaji kibali cha Polisi wala sihitaji kuungwa mkono na chama changu wala taasisi yoyote. Mimi nitaandamana kama mwananchi wa kawaida ninayechukizwa na hatua ya serikali ya kudiriki kutangaza kwamba itawalipa matapeli wa Dowans ambao ni ndugu na richmond.
Mwananchi yeyote anayetaka kuandamana pamoja nami anaweza kufanya hivyo ila naomba tuwasiliane na kushauriana kupitia JF na awe na nia njema kwa nchi yetu. Naomba atakaye taka kuandamana aandike bango kwa gharama yake na wala asitake kuyafanya maandamano haya kuwa ya kisiasa. Nategemea maandamano haya yaanzie kwenye makutano ya barabara ya Nyerere na Nelson Mandela (TAZARA) halafu yataelekea makao makuu ya TANESCO ambako nitawasilisha waraka wa kupinga kulipwa Dowans kwa Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco,. nahitaji ushauri na kuungwa mkono.
Mwananchi yeyote anayetaka kuandamana pamoja nami anaweza kufanya hivyo ila naomba tuwasiliane na kushauriana kupitia JF na awe na nia njema kwa nchi yetu. Naomba atakaye taka kuandamana aandike bango kwa gharama yake na wala asitake kuyafanya maandamano haya kuwa ya kisiasa. Nategemea maandamano haya yaanzie kwenye makutano ya barabara ya Nyerere na Nelson Mandela (TAZARA) halafu yataelekea makao makuu ya TANESCO ambako nitawasilisha waraka wa kupinga kulipwa Dowans kwa Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco,. nahitaji ushauri na kuungwa mkono.