Tangazo la maandamano ya amani kupinga kulipwa kwa dowans

MWANALUGALI

JF-Expert Member
Feb 1, 2010
601
34
Natangaza kuwa nitafanya maandamano ya amani siku ya jumanne tarehe11.1.11 kuanzia saa nane mchana kupinga serikali kuilipa Dowaans mabilioni ya fedha ambazo ni za udanganyifu! sihitaji kibali cha Polisi wala sihitaji kuungwa mkono na chama changu wala taasisi yoyote. Mimi nitaandamana kama mwananchi wa kawaida ninayechukizwa na hatua ya serikali ya kudiriki kutangaza kwamba itawalipa matapeli wa Dowans ambao ni ndugu na richmond.

Mwananchi yeyote anayetaka kuandamana pamoja nami anaweza kufanya hivyo ila naomba tuwasiliane na kushauriana kupitia JF na awe na nia njema kwa nchi yetu. Naomba atakaye taka kuandamana aandike bango kwa gharama yake na wala asitake kuyafanya maandamano haya kuwa ya kisiasa. Nategemea maandamano haya yaanzie kwenye makutano ya barabara ya Nyerere na Nelson Mandela (TAZARA) halafu yataelekea makao makuu ya TANESCO ambako nitawasilisha waraka wa kupinga kulipwa Dowans kwa Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco,. nahitaji ushauri na kuungwa mkono.
 
ukitoka TANESCO.... njoo samaki samaki mbezi beach utanikuta nikupe bia moja
 
Natangaza kuwa nitafanya maandamano ya amani siku ya jumanne tarehe11.1.11 kuanzia saa nane mchana kupinga serikali kuilipa Dowaans mabilioni ya fedha ambazo ni za udanganyifu! sihitaji kibali cha Polisi wala sihitaji kuungwa mkono na chama changu wala taasisi yoyote. Mimi nitaandamana kama mwananchi wa kawaida ninayechukizwa na hatua ya serikali ya kudiriki kutangaza kwamba itawalipa matapeli wa Dowans ambao ni ndugu na richmond.

Mwananchi yeyote anayetaka kuandamana pamoja nami anaweza kufanya hivyo ila naomba tuwasiliane na kushauriana kupitia JF na awe na nia njema kwa nchi yetu. Naomba atakaye taka kuandamana aandike bango kwa gharama yake na wala asitake kuyafanya maandamano haya kuwa ya kisiasa. Nategemea maandamano haya yaanzie kwenye makutano ya barabara ya Nyerere na Nelson Mandela (TAZARA) halafu yataelekea makao makuu ya TANESCO ambako nitawasilisha waraka wa kupinga kulipwa Dowans kwa Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco,. nahitaji ushauri na kuungwa mkono.

Kwa junsi serikali inavyoongozwa kwa woga na wasiwasi kupitiliza, sio ajabu wakatuma kikosi kizima toka FFU (amapo ni kilimeta chache toka ktk mahandaki yao -ukonga), waje walinde hapo TAZARA pote na yeyote anayeonekana kupita au kubeba hata bahasha binafsi akabururwa 'enti ni kutokana na taarifa za kiintelijensia" kuwa alikuwa anaashiria uvunjifu wa amani....!! :)

Hakuna utawala nchini hapa...geresha na uhuni tu kwa maslahi ya mafisadi. Ndio wanakula kupitia Dowans kufidia gharama zao ktk kampeni....
 
Kwa junsi serikali inavyoongozwa kwa woga na wasiwasi kupitiliza, sio ajabu wakatuma kikosi kizima toka FFU (amapo ni kilimeta chache toka ktk mahandaki yao -ukonga), waje walinde hapo TAZARA pote na yeyote anayeonekana kupita au kubeba hata bahasha binafsi akabururwa enti ni "kutokana na taarifa za kiintelijensia" kuwa alikuwa amebeaba 'kitu kinachofanana na bango ambacho kinaashiria uvunjifu wa amani....!! :); Sembuse ubebe bango lenyewe!!

Hakuna utawala nchini hapa...geresha na uhuni tu kwa maslahi ya mafisadi. Ndio wanakula kupitia Dowans kufidia gharama zao ktk kampeni....

"kutokana na taarifa za kiintelijensia" kuwa alikuwa amebeaba 'kitu kinachofanana na bango ambacho kinaashiria uvunjifu wa amani....!! :); Sembuse ubebe bango lenyewe!! nchi hii...kuna itelijensia au ni uozo mtupu!! mbona hatuzipati na wasafirisha unga waliojaa kila kona na akina Mwema wanawajua?
 
Ceteris peribus, Serikali imevunja contract inabidi ilipe.
Sikuungi mkono tena nakuonea huruma sana.
Tulia tu nyumbani na familia yako.
 
Kupinga Dowans isilipwe fidia?? Mzee hiyo ni serious zaidi watatuma vikosi vya majeshi yote ya ardhini na anga kupambana na wewe ili Dowans walipwe bila tatizo!
 
Dowans Tanzania Ltd

An electricity generating company, part of Dowans Holding owned by the Aladawi family of Dubai and Oman.

Watanzania wanafanywa mazezeta, Eti tunalazimishwa tulipe pesa kwa kampuni ya mfukoni, kampuni pesa kibao wakati haina hata website katika ulimwengu huu wa technologia.

Kampuni yenye watu wa kuunga unga.
 
Ceteris peribus, Serikali imevunja contract inabidi ilipe.
Sikuungi mkono tena nakuonea huruma sana.
Tulia tu nyumbani na familia yako.

Kila mtu anao uhuru wake wa kuchambua vitu. uchambuzi wangu unaonyesha kuwa kuna harufu ya wizi hapa na siwezi kuunga mkono wezi waibe kwenye hazina yetu hivi hivi. Kwanza nahisi hili ongezeko la gharama za umeme wakati umeme wenyewe ni wa mgao ni njia ya kutunyonya na kukusanya pesa za kuwalipa matapeli hao!! kamwe sikubali, heri ya lawama kuliko fedheha!! Nitaandamana hata kama wewe na wenzako hamtaniunga mkono!
 
Kupinga Dowans isilipwe fidia?? Mzee hiyo ni serious zaidi watatuma vikosi vya majeshi yote ya ardhini na anga kupambana na wewe ili Dowans walipwe bila tatizo!

Hata wakituma nini, mimi nitaandamana tu. Sihitaji ulinzi wa Polisi wala wa Sheikh Yahya! Mimi ninaye Mungu tu na nitakachokifanya ni kwa ajili ya utukufu wake maana ninapinga kuvunjwa kwa amri yake ya saba - usiibe. nitakuwa naitetea nchi yangu, maana watu walio na dhamana ya kuitetea ndiyo hao ambao wanashirikiana na Dowans1
 
kaka tangazo liwekwe pia kwenye magazetu ya kesho na jumatatu

I am sorry siwezi kufanya hivyo maana mimi si tajiri wala mfanyabiashara. Ni mfanyakazi tu kwenye taasisi ya umma ambako mishahara yetu ni midogo sana na haijapandishwa kitambo!!
 
Hayatakiwi kuishia TANESCO, yanatakiwa kuishia kwa huyo jamaa aliyetuambia mgao wa umeme utakuwa HISTORIA! Tanesco has nothing 2 do with this coz tangu mwanzo walishaliona hili na walimshangaa hata huyo aliyesema mgao utakuwa historia kwamba hizo data kapata wapi!
 
ukitoka TANESCO.... njoo samaki samaki mbezi beach utanikuta nikupe bia moja

Lat, Mwenzetu Mwanalugalu anachotuomba ni support - physical support. Sidhani kama anafanya hili kwa ajili ya bia. Unavyom-offer bia ni kama kumtukana vile kwa sababu unafanya wito wake ambao ni serious uwe kama wa mzaha. Wenye nguvu tutatengeneza bango na tutakuja. Tafadhali wananchi wenye nguvu na nafasi/wasaa tupeni support.
 
Back
Top Bottom