Tanganyika itahitaji wanaharakati wao

Tanganyika itahitaji wanaharakati wao

Kamundu

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2006
Posts
9,272
Reaction score
13,910
Wenzetu zanzabar wamefanikiwa kubadili katiba yao, wamefanikiwa kuondoa vifungu ambavyo vipo kwenye katiba ya muungano ambavyo hawavipendi lakini hakuna mtu au watu wanaopigania Tanganyika kwenye Muungano huu.

Hadi mkuu wa majeshi Tanzania naye kawa chawa tu yaani Watanganyika ukiacha majembe machache kama Warioba na Lissu wamekuwa waoga na wazembe wa kufikiria na kuendeshwa na wanzanzibari. Kwanini Zanzibar walifanikiwa kutengeneza katiba yao wakati katiba hii ya wiki moja ya 1977 bado ipo!!
 
Wenzetu zanzabar wamefanikiwa kubadili katiba yao, wamefanikiwa kuondoa vifungu ambavyo vipo kwenye katiba ya muungano ambavyo hawavipendi lakini hakuna mtu au watu wanaopigania Tanganyika kwenye Muungano huu. Hadi mkuu wa majeshi Tanzania naye kawa chawa tu yaani Watanganyika ukiacha majembe machache kama Warioba na Lissu wamekuwa waoga na wazembe wa kufikiria na kuendeshwa na wanzanzibari. Kwanini Zanzibar walifanikiwa kutengeneza katiba yao wakati katiba hii ya wiki moja ya 1997 bado ipo!!
Inasikitisha sana kwa kweli.
 
Si mmeona saa hizi Fatma Karume alivyoingia mitini??

Ungetegemea kwa mauaji ya October 29 , kama angekuwa kafanya jiwe Fatma angekaa kimya kama alivyokaa kimya kwa Samuya.
 
Zanzibar walifanikiwa kutengeneza katiba yao wakati katiba hii ya wiki moja ya 1997 bado ipo!!
  1. Katiba hii iliyopo ni ya 1977 na sio 1997!
  2. Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye katiba moja tuu, katiba ya JMT.
  3. Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani unaojitegemea.
  4. Katiba ya JMT inaitambua katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ila haiitambui katiba hii ya sasa ya Zanzibar ya toleo la 2010 kwasababu inakwenda kinyume na katiba ya JMT.
  5. Hivyo hiyo katiba ya Zanzibar unayoizungumzia wewe, ni katiba ambayo ipo, ila ni ipo ipo tuu kwa Wanzanzibari lakini kitaifa, haipo kwasababu haitambuliki na katiba mama ya JMT Tanzania Nchi 1 ya JMT, Zanzibar Kujiita Nchi, Sio Uhaini?. Zanzibar Iadabishwe Kuondoa Ubatili wa Katiba Yake ili Tuitambue au Tumchelee Mwana Kulia?
P
 
  1. Katiba hii iliyopo ni ya 1977 na sio 1997!
  2. Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye katiba moja tuu, katiba ya JMT.
  3. Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani unaojitegemea.
  4. Katiba ya JMT inaitambua katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ila haiitambui katiba hii ya sasa ya Zanzibar ya toleo la 2010 kwasababu inakwenda kinyume na katiba ya JMT.
  5. Hivyo hiyo katiba ya Zanzibar unayoizungumzia wewe, ni katiba ambayo ipo, ila ni ipo ipo tuu kwa Wanzanzibari lakini kitaifa, haipo kwasababu haitambuliki na katiba mama ya JMT Tanzania Nchi 1 ya JMT, Zanzibar Kujiita Nchi, Sio Uhaini?. Zanzibar Iadabishwe Kuondoa Ubatili wa Katiba Yake ili Tuitambue au Tumchelee Mwana Kulia?
P

"
  1. Katiba ya JMT inaitambua katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ila haiitambui katiba hii ya sasa ya Zanzibar ya toleo la 2010 kwasababu inakwenda kinyume na katiba ya JMT."
Sasa najiuliza kama ni kweli haitambui mbona inaendelea ? Yaani kama sisi wenyewe hatuwezi kusimamia hata katiba yetu nani atasimamia? Ndiyo maana nasema tunahitaji wanaharakati wa Tanganyika. Hatuwezi kuwa tunasema tu kuna matatizo halafu tukitaka kupigania hiyo katiba tunaongelewa tena kama kila kitu kipo sawa. Tupende kuangalia uhalisia
 
Sasa najiuliza kama ni kweli haitambui mbona inaendelea ? Yaani kama sisi wenyewe hatuwezi kusimamia hata katiba yetu nani atasimamia? Ndiyo maana nasema tunahitaji wanaharakati wa Tanganyika. Hatuwezi kuwa tunasema tu kuna matatizo halafu tukitaka kupigania hiyo katiba tunaongelewa tena kama kila kitu kipo sawa. Tupende kuangalia uhalisia
Katiba ya JMT, haiitambui mabadiliko ya katiba ya Zanzibar ya 2010, ila imeyaacha yaendelee kwasababu hayatuhusu!, hayo ni mambo yao ya ndani.
P
 
Katiba ya JMT, haiitambui mabadiliko ya katiba ya Zanzibar ya 2010, ila imeyaacha yaendelee kwasababu hayatuhusu!, hayo ni mambo yao ya ndani.
P

Yaani mambo yetu sasa ya ndani ni yapi wakati hakuna Tanganyika? Ni sawa uwe na chumba kimoja kwenye nyumba yako na kusema hujali kinachoendelea na wanaweza kufanya lolote ndani ya chumba hicho lazima kuwe na limit ya uhuru. Huwezi kutunga katiba mpya kinyume tena na katiba ya nchi!!! yanatuhusu . Yaani Bro P ni kosa sana kuchukulia vitu kama hivi powa tu na ndiyo maana tumefika hapa ! Haya yasingeweza kutokea wakati wa Nyerere tujiulize kwanini?
 
Yaani mambo yetu sasa ya ndani ni yapi wakati hakuna Tanganyika? Ni sawa uwe na chumba kimoja kwenye nyumba yako na kusema hujali kinachoendelea na wanaweza kufanya lolote ndani ya chumba hicho lazima kuwe na limit ya uhuru. Huwezi kutunga katiba mpya kinyume tena na katiba ya nchi!!! yanatuhusu . Yaani Bro P ni kosa sana kuchukulia vitu kama hivi powa tu na ndiyo maana tumefika hapa ! Haya yasingeweza kutokea wakati wa Nyerere tujiulize kwanini?
Sisi Tanzania tuna tatizo moja kubwa, hakuna elimu yoyote kuielimisha jamii kuhusu huu muungano wetu adhimu na adimu, hivyo wengi hawaujui huu muungano wetu zaidi ya kujua kuwa Tanganyika na Zanzibar ziliungana kuunda nchi moja ya Tanzania. Hivyo naomba nikupige darasa la muungano.
  1. Kuna aina 3 za miungano duniani, union, federation na confederation
  2. Union na muungano wa nchi mbili zaidi kuunda nchi moja.
  3. Federation ni muungano wa nchi mbili au zaidi kuungana kuunda taifa moja, lakini zile nchi zina utawala wake wa ndani.
  4. Confederation ni nchi kuungano kuunda nchi moja huko kila nchi ikijitegemea kwa mambo yake ya ndani.
  5. Muungano wetu ni muungano very unique, kimataifa ni muungano wa union, zile nchi zote zinakufa, inabaki nchi moja mpya, Tanganyika ilikufa na Zanzibar ilikufa, ikazaliwa Tanzania. Hivyo kimataifa Tanzania ni nchi moja ya JMT, yenye serikali moja, rais mmoja, uraia mmoja wa JMT.
  6. Kitaifa muungano wetu ni wa federation ya nchi moja yenye, kasehemu kanakojitegemea (Zanzibar) yenye serikali mbili, serikali ya JMT ambayo ndio serikali ya nchi, na SMZ, ambayo ni serikali ya kale kajisehemu kanakojitegemea mambo yake ya ndani, hivyo sehemu yenye mambo yake ya ndani ni Zanzibar tuu, Tanzania haina mambo yake ya ndani ni mambo ya kitaifa.
  7. Tuna marais wawili, rais wa nchi JMT, na rais wa kale kajisehemu.
  8. Tuna urais mmoja wa Tanzania, ila wale wa kale kasehemu pia wana utambulisho wa ziada wa ukaazi. Wanzanzibari wana haki zote za Utanzania, ila Watanzania ambao sio w kale kajisehemu hawana haki ya kule kwenye kajisehemu, wenye haki hiyo ni wale wakaazi tuu wa kale kajisehemu.
  9. JMT ina katiba yake ya nchi nzima, ila kale kajisehemu kana kajikatiba chake cha kale kajisehemu kwa mambo yake ya ndani ya kajisehemu ambayo hayaihusu JMT.
  10. Katiba ya JMT haiitambui katiba ya kajisehemu, kwasababu katiba yake iko kinyume na katiba ya JMT.
P
 
Sisi Tanzania tuna tatizo moja kubwa, hakuna elimu yoyote kuielimisha jamii kuhusu huu muungano wetu adhimu na adimu, hivyo wengi hawaujui huu muungano wetu zaidi ya kujua kuwa Tanganyika na Zanzibar ziliungana kuunda nchi moja ya Tanzania. Hivyo naomba nikupige darasa la muungano.
  1. Kuna aina 3 za miungano duniani, union, federation na confederation
  2. Union na muungano wa nchi mbili zaidi kuunda nchi moja.
  3. Federation ni muungano wa nchi mbili au zaidi kuungana kuunda taifa moja, lakini zile nchi zina utawala wake wa ndani.
  4. Confederation ni nchi kuungano kuunda nchi moja huko kila nchi ikijitegemea kwa mambo yake ya ndani.
  5. Muungano wetu ni muungano very unique, kimataifa ni muungano wa union, zile nchi zote zinakufa, inabaki nchi moja mpya, Tanganyika ilikufa na Zanzibar ilikufa, ikazaliwa Tanzania. Hivyo kimataifa Tanzania ni nchi moja ya JMT, yenye serikali moja, rais mmoja, uraia mmoja wa JMT.
  6. Kitaifa muungano wetu ni wa federation ya nchi moja yenye, kasehemu kanakojitegemea (Zanzibar) yenye serikali mbili, serikali ya JMT ambayo ndio serikali ya nchi, na SMZ, ambayo ni serikali ya kale kajisehemu kanakojitegemea mambo yake ya ndani, hivyo sehemu yenye mambo yake ya ndani ni Zanzibar tuu, Tanzania haina mambo yake ya ndani ni mambo ya kitaifa.
  7. Tuna marais wawili, rais wa nchi JMT, na rais wa kale kajisehemu.
  8. Tuna urais mmoja wa Tanzania, ila wale wa kale kasehemu pia wana utambulisho wa ziada wa ukaazi. Wanzanzibari wana haki zote za Utanzania, ila Watanzania ambao sio w kale kajisehemu hawana haki ya kule kwenye kajisehemu, wenye haki hiyo ni wale wakaazi tuu wa kale kajisehemu.
  9. JMT ina katiba yake ya nchi nzima, ila kale kajisehemu kana kajikatiba chake cha kale kajisehemu kwa mambo yake ya ndani ya kajisehemu ambayo hayaihusu JMT.
  10. Katiba ya JMT haiitambui katiba ya kajisehemu, kwasababu katiba yake iko kinyume na katiba ya JMT.
P

Sasa kwanini tuna Raisi wa Zanzibar na Raisi wa Tanzania? Zanzibar ina mpaka katiba. Kama wanapenda muundo huu basi kuwe na serikali ya Tanganyika maana kwasasa hakuna nchi yenye mfumo wa kijinga hivi
 
CCM walikataa No reform no election. Wamekaribisha mjadala waliokuwa wanakwepa.

Kuna Bendera kama buku hivi za Tanganyika zimeanza kusambazwa mitaani
 
Sisi Tanzania tuna tatizo moja kubwa, hakuna elimu yoyote kuielimisha jamii kuhusu huu muungano wetu adhimu na adimu, hivyo wengi hawaujui huu muungano wetu zaidi ya kujua kuwa Tanganyika na Zanzibar ziliungana kuunda nchi moja ya Tanzania. Hivyo naomba nikupige darasa la muungano.
  1. Kuna aina 3 za miungano duniani, union, federation na confederation
  2. Union na muungano wa nchi mbili zaidi kuunda nchi moja.
  3. Federation ni muungano wa nchi mbili au zaidi kuungana kuunda taifa moja, lakini zile nchi zina utawala wake wa ndani.
  4. Confederation ni nchi kuungano kuunda nchi moja huko kila nchi ikijitegemea kwa mambo yake ya ndani.
  5. Muungano wetu ni muungano very unique, kimataifa ni muungano wa union, zile nchi zote zinakufa, inabaki nchi moja mpya, Tanganyika ilikufa na Zanzibar ilikufa, ikazaliwa Tanzania. Hivyo kimataifa Tanzania ni nchi moja ya JMT, yenye serikali moja, rais mmoja, uraia mmoja wa JMT.
  6. Kitaifa muungano wetu ni wa federation ya nchi moja yenye, kasehemu kanakojitegemea (Zanzibar) yenye serikali mbili, serikali ya JMT ambayo ndio serikali ya nchi, na SMZ, ambayo ni serikali ya kale kajisehemu kanakojitegemea mambo yake ya ndani, hivyo sehemu yenye mambo yake ya ndani ni Zanzibar tuu, Tanzania haina mambo yake ya ndani ni mambo ya kitaifa.
  7. Tuna marais wawili, rais wa nchi JMT, na rais wa kale kajisehemu.
  8. Tuna urais mmoja wa Tanzania, ila wale wa kale kasehemu pia wana utambulisho wa ziada wa ukaazi. Wanzanzibari wana haki zote za Utanzania, ila Watanzania ambao sio w kale kajisehemu hawana haki ya kule kwenye kajisehemu, wenye haki hiyo ni wale wakaazi tuu wa kale kajisehemu.
  9. JMT ina katiba yake ya nchi nzima, ila kale kajisehemu kana kajikatiba chake cha kale kajisehemu kwa mambo yake ya ndani ya kajisehemu ambayo hayaihusu JMT.
  10. Katiba ya JMT haiitambui katiba ya kajisehemu, kwasababu katiba yake iko kinyume na katiba ya JMT.
P
Moja ya weakness kubwa ya CCM ni kutotoa elimu juu ya muungano, kujisahau kuwa vizazi na matishio ya Taifa hubadilika kila mahala.

CCM ilipaswa isimame kama chama huru na kwa hekima kuelezea kuwa yaliyotokea October 29 hayahusiani na Uzanzibar au Utanganyika, ila kwa sababu ya Chama-Dola ikajisahahu.

Yale yaliyovikuta vituo vya mafuta, mali za wana ccm na ofisi zao ndio yanaandaliwa kuwakuta Wazanzibar walioko Zanzibar na visasi kwa Watangayika walioko Zanzibar.

Samia atoke haraka madarakani kama wanataka kuzuia umwagaji wa damu ulioko mbele
 
Polepole alitoa onyo la kiutamaduni kuwa Makamu wa Rais hatakiwi kuwa Rais wa serikali ijayo watu wakampuuza wakaenda Kwenye uchaguzi wa October 29, Samia akiwa anagombea peke yake bila mpinzani uchaguzi ukaharibika watu wakauana Wakaichukia Zanzibar na Tanzania.

It does not make any sense mtu kutoka Kizimkazi apewe madaraka ya kuitawala/kimaaumuzi juu ya ardhi yote ya Tanganyika, wazee waliomtuma Polepole waliliona hili na wakataka Samia apumzike kwa amani.
 
Back
Top Bottom