TANGA: Mvua kubwa iliyodumu kwa siku nzima yaleta maafa

Hii ya Tanga sijawahi Iona ni mvua nzito utadhani ghalika kuu.

Msiwaachie watoto kwenda shule
 
Jamani watu wa Tanga poleni sana. Hapo ndio nyumbani nilipozaliwa na kukulia.

Mapango ya Amboni (Kiomoni) hayawezi kuathirika kwa sababu mto Mkulumuzi utabeba maji yote kwenda baharini.

NGUZO wewe sio mtu wa Kiomoni kweli? Nina swahiba wangu pale.
Hapana kaka
 
Chumbageni pia hali ni tete. Yani ikiendelea tena kwa masaa mawili tu nyumbani kwetu kutakumbwa na mafuriko pia.
 
Salam wakuu,

Mpaka naandika bandiko hili Muda huu, mvua kali sana bado inashuka eneo la Tanga mjini na vijana vyake. Ni mvua ambayo Kama ikiendelea kupiga namna hii non-stop basi Kesho tutegemee mengine kwenye front pages. Haijakata tangu saa9 usiku wa kuamkia leo na hapa bado inapiga.

Maafa (ambayo hayadhibitishwa na mamlaka rasmi):

1. Mtu mmoja amoteza maisha eneo la kange baada ya kusombwa na maji
2. Nyumba tatu zimebomoka
3. Barabara ya makorora imafungwa na mamlaka ya jiji kuepusha maafa. (Hii imedhibitishwa)

Waungwana sala zenu zinahitajika kwa wana Tanga. Hii mvua tunayoiomba tunaomba iwe na kiasi...

Amen.

UPDATES:

Barabara ya kuelekea kasera imefungwa na hivyo waliopo eneo Hilo ni Kama wapo kisiwani. Ninavyoandika hapa, wanamaji na polisi wamefika kuwapa pole wahanga ambao wapo upande wa pili wa barabara, (walikuwa wanatoka mjini kwenda kasera). Na wamekwama. Kwa hesabu ya haraka hawapungui watu Mia mbili. Ni janga


Wakazi wa Sahare beach wako mbioni kufutwa kwenye ramani ya tanga ikiwa mvua hii itapiga kwa masaa mengine manne mfululizo kuanzia sasa.

Maeneo korofi Kama kwanjeka na mikanjuni Kesho watahitaji usafiri mbadala kutoka makwao. Sala zenu waungwana.

Umeme umekatika.... Kwa Hali ilivyo Nadhani kuna nguzo itakuwa imeanguka. Tusubiri tamko.
Poleni sana Wana Tanga!
 
Hata Mimi huku mkanjuni hali si nzuri kabisa....maternity blocks waanze kuzifanyia ukarabati wa nguvu kwaajili ya kupokea team vibendi .
 
Mvua hii na Amini itakuwa ni Adhabu kutoka kwa Muumba wenu watu wa Tanga mmezidi kuogelea ktk Madhambi maana ukipita ktk viunga vya Tanga jioni na usiku huoni zaidi ya Maovu Viunga vya Raska Zone ndo usiseme watu wanafanya matendo ya kifirauni kwaiyo hiyo mvua isiyo katika Itakuwa kana kwamba mnachuma kile ambacho kimepandwa na mikono yenu na adhabu ya Muumba wetu huwezi izuia kwa mikono bali yatakikana watu wa Tanga mbadilike ndugu zetu muache uovu uliyipita mipaka kwa mfno Uko Tanga kuna kikundi cha Ngoma kiitwacho Baikoko hawa watu wanapendwa sana Tanga karibu Harusi nyingi wanapenda kuwaalika watu hawa nadhani watu wa Tanga mnajua vitu wanavyovifanya ktk Maharusi yenu alafu nyinyi mnawashangilia na kuwatunza watu hawa wanaocheza Uc** wa Mnyama Kweli!!! Mambo haya ndo mnataka Mola wenu asiwaadhibu hapa Duniani?
 
Naungana na wote wenye kuwaombea wahanga wa mvua hizi za kupitiliza,Naomba muumba awape faraja na wepesi kwa kuwalinda na madhila mvua kubwa hizi,Amen.Mwenyezi unatusikia na kwako tu ndiyo tegemeo ninakuomba huruma zako ziwe pamoja na wakazi wa Tanga na Tanzania kwa ujumla kwani mvua hizi zimeripotiwa maeneo mengi ya nchi,Amen.Kwa wafiwa poleni sana kwa kuondokewa na Mwenyezi awape subira,Amen.Kwa walioiaga Dunia Mwenyezi wape mwisho mwema,Amen!
 
Kwa mujibu wa watabiri wa hali ya hewa, mvua kwa Tanga zitanyesha hadi usiku.
mida ya saa tano asubuhi ndo itakua kubwa zaidi hadi karibia saa nane mchana
 
Back
Top Bottom