El Roi
JF-Expert Member
- May 29, 2020
- 263
- 502
Kuna mashirika ambayo pamoja na nchi kuwa na mamlaka zinazosimamia utekelezaji wa sheria ( law enforcement entities) bado yenyewe hayaguswi na hilo. They are immune to laws of the land .
Tanesco ni shirika ambalo kweli nashangaa kama lina mifumo na kama vyombo vya serikali vya kutekeleza sheria vinaliona shirika hili.
Nadiriki kusema rushwa iliyoko Tanesco bila shaka imeruhusiwa na nchi iwe hivyo ilivyo.
Mimi ni mteja niliye jaza fomu ya kuomba umeme tangu mwaka 2019. Mwaka 2020 maeneo yote ya waliomba huduma hiyo yalipewa umeme isipokuwa maeneo machache na langu likiwepo. Katika kufuatilia Kwa Nini maeneo kadhaa yamerukwa, niliambiwa maeneo hayo survey haikufanyika. Maelezo hayo yalinishangaza kwa sababu hili kilikuwa eneo la mradi na surveyor alikuja mpaka kwetu.
Baada ya kulalamika sana, tuliletewa Tena surveyor ambaye hata hivyo michoro yake hakuipeleka mahali husika.
Baadae nikauona uongozi hata hivyo nikaambiwa hata bila kificho na moja ya wafanyakazi kwamba nijiongeze bila hivyo umeme itakuwa hadithi. Nilidhani anatania , lakini kweli imekuja kuwa hivyo. Tanesco wakihongwa watakupa huduma hiyo within no time, nguzo zitapatikana, na hiyo control number utaitwa haraka na umeme utakufikia.
Nimeshuhudia kwa macho yangu nguzo zinafichwa mpaka mtaani zikisubiri wenye hongo watoe ili huduma iwafuate, nimeshuhudia umeme ukiwekwa kupitia nahali popote mara mtu anapotoa rushwa. Nimekutana na maroli yenye nguzo watu wakiwa wanauza nguzo shilingi 50 000 kwa nguzo, ukienda usiye na rushwa unaambiwa " nguzo hakuna tunasubiri budget ya serikali'. Mwaka wa budget mpaka unakwisha, bado unaambiwa subiri, mwaka wa kwanza wa pili nakuendelea .
Baada ya kuwa nimefanya zoezi hili kwa muda mrefu wa kufuatilia zimwi linaitwa umeme , nikajagundua
1) Rushwa imehararishwa Tanesco.
Usitegemee kupata huduma hii kwa kufuata njia za kawaida.
Maana hata baada ya kuwa nifuata kila nilichoambiwa bado eneo letu hilo dogo la watu wasiotaka kujichangisha halina umeme Wala miundo mbinu yoyote. Nimesema wasiojichangisha Kwa sababu hii ndo lugha tunayoambiwa " changangisheni Ili mpate umeme". Na kweli mahali watu wanachanga umeme utapita hata chini ya ardhi ili aliyetoa rushwa apewe.
2) Hakuna Seniority kabisa.
Baada ya kuwaona mameneja na mpaka wao kuja kuona eneo na kukiri uhitaji wetu ni wa kweli, wafanyakazi wa chini hawatekelezi kabisa maagizo. Nakumbuka mtu mmoja alinambia katika harakati hizi za kutafuta umeme ( Natumia kutafuta maana umeme ni bidhaa adimu chini ya Tanesco hii ya Arusha) jiongeze, maana hao wote ni mfumo ( syndicate).
Sasa naamini Tanesco wote ni kambale na wanajuana sana madeal Yao.
3) Hakuna uendelevu ( consistency)
Tanesco kila mtu ana lake na kusema. Meneja atakwambia vingine, huyu atakwambia hivi na huyu hivi. Mwishoni niliuliza yakini mbona hatupatiwi huduma hii na hasa wakati huu wa budget. Nikaambiwa natakiwa niombe Tena Kwa njia inaitwa e connect. Nikauliza, naombaje Tena wakati ombi langu ni buck logged kwa muda wa miaka karibu minne sasa? Nikaambiwa hiyo ndo njia. Inauma unapoona umeme unafungwa kwingine kama uyoga huku kwetu tukiambiwa jiongeze, omba Kwa e connect nk.
Hapo nyuna mtu aliwahi kusema kwamba umeme wa Tanzania ni siasa. Mimi nasema umeme wa Tanesco Arusha ni rushwa, rushwa, rushwa tupu.
Lakini kwa kuwa sipendi kupuuza ushauri wa mtu najiandaa labda sasa niende kwa wanasiasa kama mkuu wa mkoa hivi au wilaya kuthibitisha kama kweli umeme ni siasa .
Inakera sana.
Tanesco ni shirika ambalo kweli nashangaa kama lina mifumo na kama vyombo vya serikali vya kutekeleza sheria vinaliona shirika hili.
Nadiriki kusema rushwa iliyoko Tanesco bila shaka imeruhusiwa na nchi iwe hivyo ilivyo.
Mimi ni mteja niliye jaza fomu ya kuomba umeme tangu mwaka 2019. Mwaka 2020 maeneo yote ya waliomba huduma hiyo yalipewa umeme isipokuwa maeneo machache na langu likiwepo. Katika kufuatilia Kwa Nini maeneo kadhaa yamerukwa, niliambiwa maeneo hayo survey haikufanyika. Maelezo hayo yalinishangaza kwa sababu hili kilikuwa eneo la mradi na surveyor alikuja mpaka kwetu.
Baada ya kulalamika sana, tuliletewa Tena surveyor ambaye hata hivyo michoro yake hakuipeleka mahali husika.
Baadae nikauona uongozi hata hivyo nikaambiwa hata bila kificho na moja ya wafanyakazi kwamba nijiongeze bila hivyo umeme itakuwa hadithi. Nilidhani anatania , lakini kweli imekuja kuwa hivyo. Tanesco wakihongwa watakupa huduma hiyo within no time, nguzo zitapatikana, na hiyo control number utaitwa haraka na umeme utakufikia.
Nimeshuhudia kwa macho yangu nguzo zinafichwa mpaka mtaani zikisubiri wenye hongo watoe ili huduma iwafuate, nimeshuhudia umeme ukiwekwa kupitia nahali popote mara mtu anapotoa rushwa. Nimekutana na maroli yenye nguzo watu wakiwa wanauza nguzo shilingi 50 000 kwa nguzo, ukienda usiye na rushwa unaambiwa " nguzo hakuna tunasubiri budget ya serikali'. Mwaka wa budget mpaka unakwisha, bado unaambiwa subiri, mwaka wa kwanza wa pili nakuendelea .
Baada ya kuwa nimefanya zoezi hili kwa muda mrefu wa kufuatilia zimwi linaitwa umeme , nikajagundua
1) Rushwa imehararishwa Tanesco.
Usitegemee kupata huduma hii kwa kufuata njia za kawaida.
Maana hata baada ya kuwa nifuata kila nilichoambiwa bado eneo letu hilo dogo la watu wasiotaka kujichangisha halina umeme Wala miundo mbinu yoyote. Nimesema wasiojichangisha Kwa sababu hii ndo lugha tunayoambiwa " changangisheni Ili mpate umeme". Na kweli mahali watu wanachanga umeme utapita hata chini ya ardhi ili aliyetoa rushwa apewe.
2) Hakuna Seniority kabisa.
Baada ya kuwaona mameneja na mpaka wao kuja kuona eneo na kukiri uhitaji wetu ni wa kweli, wafanyakazi wa chini hawatekelezi kabisa maagizo. Nakumbuka mtu mmoja alinambia katika harakati hizi za kutafuta umeme ( Natumia kutafuta maana umeme ni bidhaa adimu chini ya Tanesco hii ya Arusha) jiongeze, maana hao wote ni mfumo ( syndicate).
Sasa naamini Tanesco wote ni kambale na wanajuana sana madeal Yao.
3) Hakuna uendelevu ( consistency)
Tanesco kila mtu ana lake na kusema. Meneja atakwambia vingine, huyu atakwambia hivi na huyu hivi. Mwishoni niliuliza yakini mbona hatupatiwi huduma hii na hasa wakati huu wa budget. Nikaambiwa natakiwa niombe Tena Kwa njia inaitwa e connect. Nikauliza, naombaje Tena wakati ombi langu ni buck logged kwa muda wa miaka karibu minne sasa? Nikaambiwa hiyo ndo njia. Inauma unapoona umeme unafungwa kwingine kama uyoga huku kwetu tukiambiwa jiongeze, omba Kwa e connect nk.
Hapo nyuna mtu aliwahi kusema kwamba umeme wa Tanzania ni siasa. Mimi nasema umeme wa Tanesco Arusha ni rushwa, rushwa, rushwa tupu.
Lakini kwa kuwa sipendi kupuuza ushauri wa mtu najiandaa labda sasa niende kwa wanasiasa kama mkuu wa mkoa hivi au wilaya kuthibitisha kama kweli umeme ni siasa .
Inakera sana.