Habari, Mimi ni mkazi wa Morogoro vijijini. Biashara yangu ni ya kukoboa zao(silitaji kwa sababu binafsi) ni mwaka wa tatu sasa nafuatilia kuwekewa umeme katika kiwanda hichi kidogo maana natumia diesel lakini gharama nnazopewa ni zaidi ya milioni kumi, ikiwemo na kununua transform.
Wataalam hili suala limekaaje maana nashindwa kuelewa. NINUNUE transformer kivipi wakati ni wajibu wa TANESCO kutupatia huduma kwa malipo husika ya huduma hi.. na ugumu wa kuwekewa umeme unakuja wapi jamani. MSAADA
Hii taarifa ya kulipa milion kumi na kununua transformer umepewa kwa utaratibu gani? Wamekuandikia ukalipie wapi? Na je meneja wa TANESCO hapo Morogoro vijijin ulimuona? Akaridhia hizo gharama?
Habari, Mimi ni mkazi wa Morogoro vijijini. Biashara yangu ni ya kukoboa zao(silitaji kwa sababu binafsi) ni mwaka wa tatu sasa nafuatilia kuwekewa umeme katika kiwanda hichi kidogo maana natumia diesel lakini gharama nnazopewa ni zaidi ya milioni kumi, ikiwemo na kununua transform
Kama utakumbuka Maelekezo ya Serikali hapo awali hakuna mteja anayepaswa kununua kifaa chochote cha kumfungia umeme bali ni jukumu la TANESCO kusogeza miundombinu ya umeme kwa wateja wake, tafadhali tusaidie taarifa zifuatazo
Jina
Namba ya Simu
Wilaya
Na kiasi ulichodai kuambiwa ulipie ili tukupatie ufafanuzi kwa taarifa kamili
Kama utakumbuka Maelekezo ya Serikali hapo awali hakuna mteja anayepaswa kununua kifaa chochote cha kumfungia umeme bali ni jukumu la TANESCO kusogeza miundombinu ya umeme kwa wateja wake, tafadhali tusaidie taarifa zifauatazo...
Sikuandikiwa kwa barua nimembiwa kwa maneno tu. Meneja nimeonana nae, hata namba ninayo Ila siku hizi hataki hata kupokea simu. Nimeongea nae sana. Bila mafanikio.