TANESCO wanamhujumu Magufuli na Silaa

Lukolo

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
5,143
3,196
Tangu juzi umeme katika jimbo la ukonga umekatwa. Umeme huu ulikatwa saa moja kamili wakati taarifa ya habari ya channel ilipokuwa inaanza. Kwa harakaharaka vijana walijiridhisha kwamba TANESCO walikata umeme ili watu wasione msafara wa Lowassa kwenda kuchukua form. Lakini hadi kufikia hivi leo umeme haupo. Basi jana jioni nilipopita vijiweni, hoja ilikuwa ni kukosekana kwa umeme iwe ni sababu tosha ya kuinyima kura CCM.

Vijana walikuwa wanashawishiana na kutiana nguvu kwamba Lowassa aliingia mkataba wa Richmond ili kupunguza tatizo la umeme, kwahiyo alifanya hivyo kwa kujali matatizo ya watanzania, kwahiyo wapo tayari kumpa kura ili amalize kabisa tatizo la umeme ambalo imeonekana kwamba kwa serikali ya CCM halijapewa kipaumbele.

Nilishuhudia mahali pengine vijana wakiwaambia mama nitilie waliokuwa wamewasha mishumaa kwamba shida yote hii inatokana na kuichagua CCM, kwahiyo mateso hayo wanayoyapata yawe fundisho kwao kwamba CCM haifai. Jana maeneo yote ya Majohe na Chanika story zilikuwa ni kuinyima kura CCM ili kumaliza tatizo la umeme.

Kwa harakaharaka nawaza kwamba kukatwa kwa umeme kwa siku mbili na ukimya wa TANESCO, kutowajulisha wananchi sababu za kukatwa huko kwa umeme, kuna nia ya kuwaudhi wananchi ili wasiichague CCM/ Magufuli na pia wasimchague Slaa ambaye ni mgombea ubunge kwa jimbo la Ukonga.
 
Tataizo la umeme ni tanzania nzima
CCM ilishatuaminisha kwamba mgao ni ndoto sasa kukatiwa umeme kwa siku hadi mbili ndiyo kusema huo ni mgao au ni nini? Na katika hali hii ni kwa vipi mtu atashawishika tena kuichagua CCM ilihali biashara zake zinaharibika. Nafikiri hiyo ndiyo hoja ya vijana wa Ukonga.
 
Mtoa mada umekurupuka....hujui hal halis ya huo umeme unaozungumzia,fanya Research kwanza kabla ya kulaumu Tanesco.....Kabla ya kutoa mada uwe unajirizisha kwanza mwenyewe kisha late huku jukwaani.....Asante
 
CCM ilishatuaminisha kwamba mgao ni ndoto sasa kukatiwa umeme kwa siku hadi mbili ndiyo kusema huo ni mgao au ni nini? Na katika hali hii ni kwa vipi mtu atashawishika tena kuichagua CCM ilihali biashara zake zinaharibika. Nafikiri hiyo ndiyo hoja ya vijana wa Ukonga.

MACCM wenyewe wana kaa usemi.............WAMEYATAKA WENYEWE.........CCM MBELE KWA MBELE.
 
Mtoa mada umekurupuka....hujui hal halis ya huo umeme unaozungumzia,fanya Research kwanza kabla ya kulaumu Tanesco.....Kabla ya kutoa mada uwe unajirizisha kwanza mwenyewe kisha late huku jukwaani.....Asante

Tusaidie kidogo hiyo research anaifanyeje? hata mie na hamu ya kuifanya.
 
Mtoa mada umekurupuka....hujui hal halis ya huo umeme unaozungumzia,fanya Research kwanza kabla ya kulaumu Tanesco.....Kabla ya kutoa mada uwe unajirizisha kwanza mwenyewe kisha late huku jukwaani.....Asante

Kwanini apoteze muda wake kufanya Research ya umeme wakati inajulikana TATIZO ni serekali MBOVU ya CCM inayosimamia Tanesco
 
Raisi wa nchi ni Amiri Jeshi Mkuu. Maana yake yeye ndiye aliye na maamzi ya mwisho. Na unapomshauri Boss wako kuna kukubaliwa au kukataliwa. Kama wewe ungekuwa Lowassa na raisi akatupilia mbali mawazo na mapendekezo yako, ungefanyaje? Hakuna kinachoweza kufanyika nchini bili idhini ya raisi. Waziri mkuu na mawaziri wengine wote hawawezi kupitisha jambo bila ya mweshimiwa raisi kuidhini au kukubali. Tusubiri wakati wa kampeni za uchaguzi ndo tutasikia mengi kuhusu sakata zima la ufisadi Tanzania.
 
Nimesikia katika redio One kuwa tatizo huko ni transfoma imeungua, hivyo umeme hautakuwepo mpaka iletwe nyingine kutoka bagamoyo.
 
Tanesco wamesema Transformer iliungua kutokana na uchakavu wa miundombinu na sasa wanaitoa Transformer nyingine Bagamoyo ili kuja kuibadilisha hivyo mtoa post unaweza kuedit thread yako ili usihusishe Tanesco na hayo ya vijana wa vijiweni
 
Mtoa mada umekurupuka....hujui hal halis ya huo umeme unaozungumzia,fanya Research kwanza kabla ya kulaumu Tanesco.....Kabla ya kutoa mada uwe unajirizisha kwanza mwenyewe kisha late huku jukwaani.....Asante

Mi namsapot mtoa mada...️uku sengerema kila siku asubuhi umeme unakatika na kurudi saa moja-mbili usiku lakini juzi EL alivyoenda kuchukua form umeme ulirudi saa saba usiku na ulikatika saa kumi na mbili asubuh yote hiyo tusione maandamano/Habari na kujua kinachoendelea.....chakushangaza leo umeme upo wakati tumeshazoea kuuona mida kama hii
 
Mtoa mada umekurupuka....hujui hal halis ya huo umeme unaozungumzia,fanya Research kwanza kabla ya kulaumu Tanesco.....Kabla ya kutoa mada uwe unajirizisha kwanza mwenyewe kisha late huku jukwaani.....Asante
Acha kuwayawaya , afanye research kwani yeye mtumishi wa Tanesco au anasomea mambo ya electric distribution. TANESCO wenyewe hawajasema lolote sasa wewe uo utafiti uufanye kwa gharama za nani?!! mashaka yanakuja zaidi umeme kukatwa kila saa moja hasa siku UKAWA inapokuwa na tukio muhimu.
N.B. CCM ijue inapokata umeme inasababisha huduma kama maji kukosekana hivyo kuongeza chuki kwa wapiga kura, pia karaha kubwa iko hospital kwa wagonjwa wanaohitaji kufanyiwa upasuaji na kufanyiwa vipimo mbalimbali. Naishauri CCM ifikirie njia nyingine ya kuthibiti wapinzani na siyo hii inayoiongezea CCM chuki kubwa kwa wapiga kura, kama tabia hii itaendelea CCM subirini kipigo kikali octoba.
 
Kwa hiyo umeme wakikatiwa CCM ndio Tanesco wanahujumu wagombea wa CCM ila wakikatiwa UKAWA Tanesco wako sahihi?
 
huku kwetu hamna umeme kabisa, shughuli za kiuchumi zimesimama, nini kitakachonishawishi kuipigia CCM kura?

Viwanda havizalishi matokeo yake wafanyakazi watapunguzwa, tatizo la ajira litaongezeka. Hii itasababisha shida kubwa kwa familia nyingi.

Mtawashawishi vip wawapigieni kura? Chama changu CCM mbona watuangusha hivi kusimamia misingi ya uchumi wetu?

Kila tukijaribu kukutea tunazidiwa na ukweli mchungu ulio wazi kama huu ambao hata mwananchi wa kawaida kijijin humdanganyi maana anona hali halisi.

Wawajibisheni Tanesco wanatuhujumu sana.
 
Mwanza nipo Igoma Nina zaidi ya wiki 3 umeme nakutana nao usiku kwa usiku siku mbili zilizopita unarudi saa 5 usiku 12 asubuhi WANAKATA!!!
 
shidah iko mwishoni next wiki tunaanza kutumia umeme utokanao na gesi. ukiona mateso yanazid bhas uokovu unakalibia
 
Mtoa mada umekurupuka....hujui hal halis ya huo umeme unaozungumzia,fanya Research kwanza kabla ya kulaumu Tanesco.....Kabla ya kutoa mada uwe unajirizisha kwanza mwenyewe kisha late huku jukwaani.....Asante
Bila shaka unafanya kazi TANESCO. Na bila shaka ni sehemu ya wale waliokurupuka kuueleza umma wa Tanzania kwamba mgao wa umeme kwa sasa itakuwa ndoto? Kama TANESCO walitamka dhahiri shahiri kwamba mgao wa umeme ni ndoto, sasa hiki kinachotokea kwanini tusikichukulie kwamba kina lengo la kumhujumu Magufuli? Kama wewe una unalolijua kuhusu TANESCO ambalo sisi hatulijui basi tuambie ili tujue kwamba TANESCO haimhujumu Magufuli. Halafu usinilaumu mimi, walaumu mama nitilie na vijana wa mtaani kwetu wanaohusisha kukatika kwa umeme na uchaguzi ujao.
 
Nimesikia katika redio One kuwa tatizo huko ni transfoma imeungua, hivyo umeme hautakuwepo mpaka iletwe nyingine kutoka bagamoyo.
Lol, I thought hiyo transformer nyingine inaletwa kutoka India; kumbe Bagamoyo? Hivi tunahitaji hata masaa matatu kutoa transformer Bagamoyo kuipeleka Kisarawe? Ni hujuma tu, hakuna lingine? Wanataka kumkosesha kura Magufuli hawa!
 
Tanesco wamesema Transformer iliungua kutokana na uchakavu wa miundombinu na sasa wanaitoa Transformer nyingine Bagamoyo ili kuja kuibadilisha hivyo mtoa post unaweza kuedit thread yako ili usihusishe Tanesco na hayo ya vijana wa vijiweni
TANESCO hawajui life span ya transformer zao? Na kutoa transformer Bagamoyo kwenda Kisarawe kunahitaji siku mbili? Kimsingi kama watu waliopewa jukumu la kusimamia huduma za jamii wameshindwa kutekeleza wajibu wao, na hasa tatizo la kukosekana kwa huduma linapojitokeza katika kipindi hiki ni haki ya vijana kulihusisha na kampeni, na kwa hakika ndivyo zinavyopigwa kampeni huko mitaani kwetu. To me, kushindwa kwa TANESCO kurespond kwa wakati, ni hujuma pia.
 
Back
Top Bottom