TANESCO wanaficha jambo

TANESCO wanaficha jambo

kasenene

JF-Expert Member
Joined
Jun 6, 2008
Posts
1,632
Reaction score
2,414
Tuliahidiwa umeme tokea wiki mbili zilizopita kwamba mambo yataenda sawa, tunaenda sasa wiki ya tatu bila umeme watanzania tunazidi kugawana umaskini, watu humu ndani mpo kimya mnashadadia matokeo ya tafiti zilizofanywa Lumumba.

Mwenye habari za jikoni atujuze manake mramba (mkurugenzi) wa TANESCO kama kupiga ganzi, isije ikawa walikuwa wabasubiri pesa za MCC tulizonyimwa rasmi 17.09.2015
 
Only in tanzania huduma muhimu kama umeme unakosekana kwa wiki tatu kila siku asubuhi mpaka jioni na hakuna raia anaye lalamika....
 
watanzania raia sijui wana matatizo ganii, mnawaza sana siasa kuliko maendeleo yenu binafsi.
 
Niliskia kuna kiongozi mmoja wa nchi moja alimwambia kiongoz mmoja kwamba yeye anaongoza watu sio tz palipo na marehemu
 
Mambo ndo kama hayo watu hamna umeme then mnavunga ndo umarehemu wenyewe mpo kama hampo mxiuuuuuuuuu
 
Sehemu nyingine sio ata mbali kenya tu hapo wangesha jua
 
Ingekuwa ni Thread ina Muhusu Magufuli, Wema, Kibajaji au Lowasa ungewaona wengi waki changia. So i think the real change we need right now is to change ourselves first, after that ndio tu change mfumo wa nchi.. Tatizo la hii nchi ni wananchi wenyewe wala sio wanasiasa#WalkingDead
 
Tuliahidiwa umeme tokea wiki mbili zilizopita kwamba mambo yataenda sawa...tunaenda sasa wiki ya tatu bila umeme watanzania tunazidi kugawana umaskini...watu humu ndani mpo kimya mnashadadia matokeo ya tafiti zilizofanywa Lumumba..mwenye habari za jikoni atujuze manake mramba (mkurugenzi) wa TANESCO kama kupiga ganzi....isije ikawa walikuwa wabasubiri pesa za MCC tulizonyimwa rasmi 17.09.2015

Wewe upo dunia ipi?

Jana tena imetangazwa kuwa mitambo itakuwa ikifanya kazi kiukamilifu ifikapo Oktoba 18.
 
Faiza Foxy wewe ndo pengine tukuulize upo dunia ipi..tulianza kudanganywa kwa kupewa ahadi ya wiki wiki na mkurugenzi wa Tanesco na mara ya mwisho kuzungumza alisema tayari kila kitu kipo tayari tungepata umeme ijumaa ya wiki mbili zilizopita..uko wapi sasa umeme...leo hii tunambiwa mpaka mwezi wa kumi arafu siyo yeye tena mkurugenzi imetumwa tu taarifa...hujahisi kitu Foxy..upo dunia gani.....ukitaka kujua khali ni tete jiulize ni nguvu gani serikali ya chama tawala imejitahidi kuziba mashimo kwa kila jambo linalohusu huduma.za kijamii hasa katika kipindi hiki kuelekea 25.10.2015...unadhani kwanini la TANESCO limewashinda?....Foxy unaifahamu Pesa MCC ilikuwa ilpwe lini na je wamesemaje wafadhili....amka
 
Kinachonishangaza, ni watu kutokuona kukosekana kwa umakini katika mambo yote ya msingi katika maisha ya mtanzania, Miaka 53 ya uhuru, bado nchi ina mgao, miaka 53 ya uhuru, maji yenye vimelea vya kipindupindu yanatoka katika mfumo wa maji safi katikati ya jiji kuu la biashara Tanzania.
 
Tuna tatizo kubwa katika huduma muhimu kwa jamii. Maji, Afya, Umeme, Miundombinu pamoja na mipango miji, na Elimu.

Lakini pia rasilimali watu ni tatizo kubwa, waliwekwa kuwa dhamana yetu wengi ni wezi wa kutupwa, hawana utu na ubinafsi mwingi unawaongoza. TANESCO ni moja ya matatizo makubwa tuliyonayo nchini...
 
tunawalaumu sana viongozi wakati Tatizo kubwa ni sisi wenyewe wananchi ambao tunawaweka viongozi wakivurunda tunachukulia powa
 
Hoi ndio tanzania na watanzania wake.....

Maji hakuna
Huduma ya afya majanga
Umeme hakuna
Miundombinu chali

Halafu watu wako busy na lowasa na magufuli

Acha tanesco wakate tu......
 
Back
Top Bottom