TANESCO: Rationing is back!

mkuu hizi ndio wanaita visioni twente twente 2020.......... Jamani sio kila jambo mnaliweka kisihasa daah wakati mwngine naingia uoga na uwezo wa wawakilishi wangu huko mjengoni ............
 
infinite solution ni kuachana na umeme wa dharura baaaaasi ... Haya mambo mengine sie pale slab tulikuwa tunayaita chai tu ......... Siasa kwenye fani za watu mbaya sana nakuonea huruma mhandisi mwenzagu mhando daah
 

Haya ndiyo mawazo na uwezo wa Mtu anayetaka Urais kwa udi na uvumba...

Hivi anashindwa kuelewa root cause ya matatizo ya umeme ni ufisadi ambao watuhumiwa wake ndiyo wanamtumia kwa sasa kuivuruga CDM especially Rostam?
 
Yaani kwake anajivunia jenereta ambapo anajaziwa mafuta kutokana na pesa za walipa kodi
 
Zitto ni mnafki tu Hana jipya.
Actually ni ujinga wa kutupwa kumwondolea jenereta mkuu wa shirika la Tanesco maana inaelekea hiyo ni hatua ya chuki binafsi tu.
It is also a populist move with no positive effects to the whole power problem.
Waziri wa uchukuzi akaendeshe dala dala mwenyewe basi ili kupunguza tatizo la usafiri DSM
Magufuli je? ashike sululu na kujenga barabara mwenyewe
Na Waziri wa elimu akafundishe mpaka kieleweke.

Hili ndio tatizo la kuwa na wabunge wasio na solutions za nchi wala hawajui wachangie vipi kutatua matatizo yetu.

Mbaya zaidi ndio waakuwa wa kwanza kukimbilia kutaka Urais!
Je tutafika?
 
Na Zitto hana Genereta nyumbani kwake? kama angekuwa na Uchungu pia ama analo aliondoe pia
 
Maamuzi ya wabunge kuelekeza hoja yao kwa Mkurugenzi haina mshiko hata kidogo, maana huyu ni bangusilo. Niliyasema haya miaka 6 iliyopita kuhusu swala la Umeme Dar na Tanzania ya kwamba hata huo umeme wa dharura ulokusudiwa bado ulikuwa hautoshi. Na nilipinga wazo la kununua mitambo ya Dowans kwa sababu nilijua haiwezi kubadilisha kitu chochote mbali kabisa na scandal kubwa iliyotokana na mkataba mbovu..Kilichofanyika ni usanii mtupu wa JK na Lowassa kutuhadaa wananchi.

Jamani Dar inakua haraka sana, na huwezi kuboresha kitu chochote bila kuwepo msingi bora..Ujenzi wa majengo makubwa yanayohitaji nguvu kubwa ya Umeme, ongezeko kubwa la biashara na huduma mjini, hivi vyote vinahitaji umeme ambao pia unahitaji vyanzo iwe gas au generators kuongeza kiwango cha nguvu za umeme ktk grid ya taifa kulingana na maendeleo yenyewe. Hizi fikra za kuongeza ajira wakati miundo mbinu haitoshelezi mtaweza vipi kuzalisha hizo ajira na huduma za kudumu?.. Hivi kweli mnafikiria kosa ni la Tanesco? hamuoni matumizi makubwa ya umeme nchini yanavyoongezeka kupita uzalishaji wake?.

Mimi nadhani kuna tatizo ndani ya Bongo zetu, tuna mapungufu makubwa sana ya uwezo wa kufikiri kiuchumi na ndio maana reli ya kati hadi leo imelala ati nguvu kubwa inawekwa kuingiza malori nchini kama ndio usafiri wa kuaminika. Tazameni traffic barabarani yaani mtu huwezi fanya mambo mawili kwa wakati mmoja, huwezi tembelea maduka mawili sehemu mbili tofauti isipokuwa kila mmoja wetu ananunua vitu kwa machinga barabarani kwa sababu hatuna Mall sehemu ambayo mtu anaweza ku shop kwa mara moja vitu tofauti. Majimbo hayajitoshelezi kwa kila kitu na bado yanapanuka kwa kasi ambayo miundombinu ni ile ile toka tupate Uhuru..

Badala ya kumwadhibu Mkurugenzi wa Tanesco, mimi ningeshauri - Makao makuu yahamie Dodoma, tuondoe vurugu za viongozi wenyewe kwanza Dar na wabunge wote rudini majimboni kwenu na muishi na wananchi mnao wawakilisha nanyi mlijue joto la jiwe..kwa nini nyote mna makazi Dar tuu?..Kila mbunge anayeingia madarakani lazima atafute nyumba Dar acha wale waliotangulia..Huko kwenu mnakowakilisha hamtaki kuishi kwa nini..
 
Tunapoongelea suala la TANESCO inabidi tukae na tutafakari kwa kina kuhusu haya tunayoongea na implications zake kwetu sote kama Wananchi. Uhusiano wa TANESCO na Serikali ni ule wa Baba na Mwana! TANESCO hawezi kufanya kitu chochote pasipo kumshirikisha baba yake ambaye ni Serikali, na ni Serikali kupitia kwa mdogo wake Wizara ya Nishati na Madini. Na TANESCO inawajibika moja kwa moja huko. Sasa kama Serikali haimruhusu kufanya maamuzi yake peke yake unategemea kitakachofuatia ni nini? Suala la umeme wa TANZANIA halijaanza leo kuwa na matatizo, limeanza mbali sana kwenye historia ya nchi yetu.TANESCO ni shirika ambalo lina wataalamu wengi sana, lina engineers wa kutosha, lakini hawapewi nafasi ya kujiendesha wenyewe kama lenyewe, Siasa na pressures za wanasiasa ni nyingi sana, na hayo muheshimiwa mwenyekiti wa kamati Zitto Kabwe anayozungumza ni propaganda tu kwa sababu ukweli halisi anaufahamu, na mimi binafsi sioni msingi wake haswa. TANESCO hawawezi kufanya makubaliano yoyote au kusaini mkataba wowote,bila kuishirikisha serikali. Na ni serikali hiyo hiyo leo ndio inaibana TANESCO kwa mambo ambayo wao wenyewe ndio chanzo cha yote hayo, wapi na wapi?Suala la jenereta la CEO wa TANESCO, ni incentive ambayo amepewa yeye akiwa kama mkuu wa kampuni, akiambiwa achukuliwe jenereta ili aone makali ya mgao wa umeme mimi binafsi nachukulia kama manyanyaso na masimango, i don not expect kuwa hana uwezo wa kununua standby generator yake mwenyewe kwa pesa zake endapo zipo hata kariakoo kwa bei nafuu tu. Nadhani kama ni ukali wa mgao uanzie kwa watendaji wakuu wa Serikali, na ofisi zake ndio ishuke chini mpaka kwa CEO...Zaidi sana inawezekana kuna watu wanaona anafaidi sana, so ni chuki tu, maana kusema ili na yeye aone uchungu, so much of hating...Cha msingi ni Serikali kuchukua wataalamu na kukaa na kuzungumza nao na kuwasikiliza na kufuata ushauri wa kitaalamu and not just some other person ambaye hata sio mtaalamu wa umeme ndio ambaye anatoa ushauri na kutoa maagizo. Je, wataalamu wanasemaje? Wenzetu nchi zingine wanathamini sana ushauri wa wataalamu wao na wanawasikiliza, and then ndo wanaproceed na mambo mengine. Kusema sijui generator lifanyweje doesnt solve anything.Naomba kuwasilisha
 
Analo lakini halilipiwi kwa kodi zetu kama la Mhando mkuu!

Mkuu linalolipiwa na kodi zetu liko magogoni kule.. La Mhando linalipiwa na Tanesco ambayo inafanya biashara ya umeme japo kwa hasara.. Na usisahau ni moja ya incentives kwa cheo cha CEO.. La Zitto kama analo ndilo linalolipiwa kwa kodi zetu.. Maana hata kama anatoa yeye hela mfukoni lakini unatokana na mshahara wake ambao kwa kazi yake ambayo haiingizi faida inabidi agharamiwe na kodi zetu..
 
Hii nami naunga mkono kwani wanatuchezea na huu umeme utafikiri kuwa na umeme ni fadhila bana..


 
Analo lakini halilipiwi kwa kodi zetu kama la Mhando mkuu!

Wabunge wetu badala ya kudeal na cross cutting issues za energy policy na implementation yake wnaanza kudeal na petty issues za kupoteza muda wao wa kufikiri!
This must stop maana Mhando and co. wakipewa jenereta na kulipiwa na kodi zetu so what!
Tumewaajiri ili wafanye kazi usiku na mchana, ili tuio gizani tuondokane na tatizo hilo.
Ukiona mwana siasa anaanza kushughulikia petty issues basi huyo hatufai katika kushughulikia matatizo ya kitaifa.
 
Jenerata lenyewe huwa ni kama mzigo kwa sababu lain anayokaa jamaa huwa umeme haukatiki ni kma ikulu kwa hiyo bado siyo suluhisho la tatizo la mgawo wa umeme kwa watz
 
Kama ninavyoona Genereta la Zitto Kable na la Mkurugenzi wa Tanesco yoote yanawaumiza walipa kodi masikini nchini

Sababu Zitto Mshahara wake na Marupurupu yoote yanatokana na Walipakodi Sawa na huyo Mkurugenzi...

Kama ni Mimi natoa Uamuzi woote wasingetumia Genereta; Hivyo kungeongeza Ufanisi na Uvumbuzi wa kutatulia Tatizo la

Umeme haraka iwezekanavyo...
 
Sawa kabisa, sasa hawa wabunge wasiishie hapo. Kila waziri au mbunge atumie huduma za sekta anayosimamia. Kwa mfano waziri wa afya atibiwe Muhimbili na siyo Ulaya, waziri wa elimu asomeshe watoto wake katika shule anazozisimamia na siyo za seminari au zilizoko nje ya nchi, mgawo wa umeme uwe kwa viongozi wote na usiishie kwa mkurugenzi wa TANESCO tu; hapa naona wabunge wamejichagulia mbuzi wa kafara. Huenda viongozi wakiupata uchungu wa uzembe unaofanyika katika maeneo wanayoyasimamia akili zitawarudia na wataanza kufanya kazi badala ya kufikiria kuzurura na kuiingiza nchi kwenye mikataba mibovu.
Je, wabunge wetu wanaiweza hii kazi?
 
hizo hela bilion 280 zingetosha kujengea mabwawa
hata matatu madogo ya kuzalisha hata megawati 80 kwa kila moja
nchi inaongozwa na vilaza wote. upuuzi mtupu
bora hiyo wizara ibinafsishwe tujue moja,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…