pmwasyoke
Platinum Member
- May 27, 2010
- 4,889
- 3,584
Inafaa sasa JK achukuwe maamuzi mazito -- ayabwage fasta!!
Hatachukua hatua hiyo abadan. Tutumie kura zetu kuiondoa CCM katika kila kura - iwe za chaguzi ndogo au uchaguzi mkuu.
Inafaa sasa JK achukuwe maamuzi mazito -- ayabwage fasta!!
Wezi wa Kura hao Umesahau?Hatachukua hatua hiyo abadan. Tutumie kura zetu kuiondoa CCM katika kila kura - iwe za chaguzi ndogo au uchaguzi mkuu.
Ni kweli kabisa ili na yeye ajue machungu ya Mgao; Ni jambo la kawaida kwa vingozi wetu kuishi maisha tofauti na wananchi kitu ambacho kinasababisha kutothamini na kutatua matatizo yanayokabili jamii.KAMATI ya Hesabu za Mashirika ya Umma(POAC), imeagiza Bodi ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuondoa jenereta la dharura lililopo nyumbani kwa Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, William Mhando kuanzia leo ili naye ajue machungu ya kukatika umeme mara kwa mara.
William Ngeleja ni janga la kitaifa. Sijui kwa nini JK anaendelea kumkumbatia mtu ambaye ameshindwa kabisa kuongoza wizara yake. Toka nchi imepata uhuru haijapata tokea waziri ameshindwa kiutendaji kama Ngeleja. Sijui atahadithia nini watoto na wajukuu zake kwani miaka yote ya uongozi wake umeme wa mgao, madini yanaporwa na wazungu bila kodi, mafuta yanachakachuliwa na wauzaji wanaiamulia serikali cha kufanya. Kikwete watose hawa washkaji zako kina Ngeleja kwani mzigo uliompa ameshindwa kuubeba...
Ni bora, sasa atajua uchungu wananchi wanaoupata... wakati wa JK Nyerere Wakurugenzi walikuwa hawana Genereta