PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,725
Unapoingia kwenye geti la Hospitali ya Mount Meru, mkono wa kulia kuna Transfoma ya Tanesco, ambayo iko katika njia ya waenda kwa miguu.
Jana nikiwa natoka ofisini kwangu, niliona kwa mbele yangu Mdada mmoja akipiga makelele na kurukaruka huku akiwa amenaswa kwenye waya unao'support Transfoma hiyo.
Mara wakawa wamekusanyika watu wengi sana kumsaidia dada huyo, lakini kwa bahati nzuri alifanikiwa kujitoa, lakini alikumbwa na mshituko mbaya sana kiasi alikuwa akihema na kutoa jasho jingi.
Katika maelezo yake anasema kuwa akiwa anapita eneo hilo alishikilia waya hiyo, ambayo ni ya ku'support transfoma, (ni zile zinazoshikilia nguzo, na kisha kuchimbiwa ardhini) na katika hali ya kawaida waya hizo hazina umeme, lakini alipigwa shoti ya hatari, na katika mshituko sandal yake moja ikavuka, na ndo hali ikawa mbaya, akawa amenga'ng'ania hapo akishindwa kujitoa, huku akirushwarushwa!
Watu waliokusanyika wanasema kwamba hali hiyo imeshawahi kujitokeza tena mara kadha mahali hapo, na waliripoti Tanesco, lakini hakuna kilichofanyika.
Nami kwakuwa nilikuwa na namba ya simu ya Meneja nikaamua bila kujiuliza kumpigia, ambapo simu yake aliyoitoa kwa Public haikupatikana!.
Lakini nimeweka kwenye ratiba yangu kuwa nitapita hapo ofisini kwao muda wowote kuwaeleza juu ya hatari hiyo.
Tafadhali Staff wa Tanesco, ondoeni hatari iliyopo eneo hilo, maana wakati mwingine itakuwa ni kilio na majuto.
Jana nikiwa natoka ofisini kwangu, niliona kwa mbele yangu Mdada mmoja akipiga makelele na kurukaruka huku akiwa amenaswa kwenye waya unao'support Transfoma hiyo.
Mara wakawa wamekusanyika watu wengi sana kumsaidia dada huyo, lakini kwa bahati nzuri alifanikiwa kujitoa, lakini alikumbwa na mshituko mbaya sana kiasi alikuwa akihema na kutoa jasho jingi.
Katika maelezo yake anasema kuwa akiwa anapita eneo hilo alishikilia waya hiyo, ambayo ni ya ku'support transfoma, (ni zile zinazoshikilia nguzo, na kisha kuchimbiwa ardhini) na katika hali ya kawaida waya hizo hazina umeme, lakini alipigwa shoti ya hatari, na katika mshituko sandal yake moja ikavuka, na ndo hali ikawa mbaya, akawa amenga'ng'ania hapo akishindwa kujitoa, huku akirushwarushwa!
Watu waliokusanyika wanasema kwamba hali hiyo imeshawahi kujitokeza tena mara kadha mahali hapo, na waliripoti Tanesco, lakini hakuna kilichofanyika.
Nami kwakuwa nilikuwa na namba ya simu ya Meneja nikaamua bila kujiuliza kumpigia, ambapo simu yake aliyoitoa kwa Public haikupatikana!.
Lakini nimeweka kwenye ratiba yangu kuwa nitapita hapo ofisini kwao muda wowote kuwaeleza juu ya hatari hiyo.
Tafadhali Staff wa Tanesco, ondoeni hatari iliyopo eneo hilo, maana wakati mwingine itakuwa ni kilio na majuto.