Tamthilia zinaharibu wake zetu

Tamthilia zinaharibu wake zetu

Molembe

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2012
Posts
9,932
Reaction score
11,851
Sisi wanaume yetu mpira na sasa hivi mashabiki wa Arsenal wanachekaaaaa huku wale wa Man u wakiendelea kufa kwa presha,

Nirudi kwenye mada unajua wanawake wanapenda tamthilia hasa za kifilipino na Mexico tena hata kama hajui kingereza husikia na kuelewa na ukitaka anune mpaka apasuke weka mpira wakati kuna tamthilia kuepusha haya mtoto wa kiume unajichanga unanunue Tv mbili moja chumbani na sebuleni sasa na mimi wenye chumba kimoja sijui,

Nirudi kwenye mada unajua zile tamthilia wanaigiza sasa hawa wanawake wa kibongo wanataka mapenzi kama yale ya kithamthilia oh! mara baby,sweetie mara honey na outing wakati usawa wenyewe wa kulenga kwa manati, kumbukeni na wao wanaigiza hawafanyi hayo yote mnayoyaona.
 
ukiitwa baby,honey ni tamthilia?
unataka uitweje?
 
Kwahiyo na wao pia wanataka wakae kwenye majumba ya fahari,aende ofisini kwa mumewe wakafanye mapenzi,mara kampigia mume njoo nyumbani ukifika Taa zimezimwa mishumaa tuuuuuuuuuu yani rahaaaa,huyo anaeyafanya pale kama sikulipwa hayafanyi hata ..............
 
Dont be so hard na wewe kukuita baby kosaa jmn?
 
Sasa hapo wameangalia tu kwenye TV sasa sijuwi ingekuwaje kama wangekuwa wanaenda kuishi huko hata miezi kadhaa
 
Wakati wa lamja demivida ndo nilikuwa nachumbia yanii asikwambie mtu ikifika tu jamani baby angalia tamthilia siku hizi kwisha habari yake majukumu yashakuwa mengi huku kazi akirudi home mtoto Siku hizi naona hana tena time nazo kawaachia Wadada wa ndani.
 
Nimemwambia wif baada ya news hasa star tv ibadilishwe tunaweka imanuel tv maana hata tunda limekua la mgao
labda siku hakuna tamthilia ndo napata tunda.
 
Nimemwambia wif baada ya news hasa star tv ibadilishwe tunaweka imanuel tv maana hata tunda limekua la mgao
labda siku hakuna tamthilia ndo napata tunda.

Kama mimi nachukia siku zenye tamthilia sana hasa za startv.
 
Bora mie siangaliagi hayo naangaliga za kihindi tu
 
Kama mimi nachukia siku zenye tamthilia sana hasa za startv.

Kwani taamthilia inafika hadi asubuhi? Ikiisha saa 6 usku si utakula tunda? Mimi sioni kama hilo ni tatizo ebu msiwaharibie starehe wenzenu.
 
Wakati wa lamja demivida ndo nilikuwa nachumbia yanii asikwambie mtu ikifika tu jamani baby angalia tamthilia siku hizi kwisha habari yake majukumu yashakuwa mengi huku kazi akirudi home mtoto Siku hizi naona hana tena time nazo kawaachia Wadada wa ndani.

la mujer de mi vida ilikuwa nzuri kwa kweli
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom