Tamko la makanisa kuhusu gesi Mtwara

Tamko la makanisa kuhusu gesi Mtwara

Effective leadership is not about making speeches



leadership is defined by results not attributes
 
Ni kitu gani au ni kikao kipi kilichoamua kubadili Ilani ya CCM 2010-15? CCM wamenadi Ilani yao kuwa watajenga mitambo Mtwara, sasa kwanini wabadilishe? Hii issue inaweza kuleta balaa kwa CCM 2015!

Watanzania tutumiage akili zetu angalau mara moja kwa mwaka jamani. Nani aliyekwambia wewe kuwa ILANI ya uchaguzi ni sheria au mkataba wa kuidai serikali? Umeshasema ni ilani ya CCM, sasa hiyo CCM yenu kama iliwaahidi jambo kwa nini mnalihusisha na mambo ya nchi?

CCM hawa hawa ndio waliowaahidi Mahakama ya Ndoa na Kugombania Mali za Marehemu, sasa hamkuweza kujua kuwa hawa ni waongo?

Hawa wachunga mbuzi waliotoa hili tamko nao ni sawa tu na wavaa makubazi. Nani aliwaambia Kinyerezi kunajengwa mtambo wa kuchakata gesi?

Jamani mashabiki wa fujo, Kinyerezi hakujengwi mtambo wa kuchakata gesi. Kinyerezi kunajengwa Power Plant na gesi ambayo haijachakatwa huwa kama matope mazito, je haya yanasafirishwa kwenye bomba kwa uchawi wa huyo bibi yenu au?

Mi nashindwa kuelewa mishipa ya makoo inawatoka kisa nini, hata mnachodai hakieleweki. Muambiwe mara ngapi kuwa gesi itachakatwa huko na sio Kinyerezi?
 
Ukiwauliza Ccm leo watasema ilani yao ya uchaguzi haijasema kama ilivyo andikwa.HAta jamaa ni waongo wa ajabu wameshazowea kudanganya kila kukicha.. Sssa wamrumbuka wakimbie kivuli chao sssa.
 
SEHEMU YA TAMKO LA VIONGOZI WA DINI YA KIISLAMU MTWARA


  • Ahadi ya Kikwete kipindi cha kampeni ni kuijenga bandari ya Mtwara na kujenga kinu cha kufua umeme kutokana na gas Mtwara

KAULI HII YA VIONGOZI WA DINI KWA WENYE UELEWA SERIKALI IFIKIRIE UPYA

  1. Mtwara ina Bandari yenye kina kirefu katika Afrika ya mashariki yote lakini mpaka sasa mipango ya kuiendeleza imekuwa ni kizungurumkuti. Wananchi wana taarifa kuwa mipango ya kuiendeleza Bandari ya Mtwara imepindishwa na kupelekwa Bagamoyo.
  2. Wananchi wanakumbuka kwa uchungu zao lao la biashara la muhogo ambalo serikali ya Tanzania huru imeliacha linakufa kuwa zao la biashara.
  3. Wakulima wengi wanalima mihogo mingi na wanaishia kuitupa tu baada ya kuoza maana si tu kwamba haina soko bali hata teknolojia ya kulitunza kwa muda mrefu hawana. Mashamba wanayo na wanalima kwa bidii wanavuna mihogo mingi lakini wa kumuuzia tayari serikali ilishampoteza na haina mpango wa kulifufua zao hili kama zao la biashara.
  4. Wananchi wa Mtwara na kusini kwa ujumla wana kilio cha muda mrefu cha zao la korosho na mpaka sasa serikali inababaisha tu haina mpango wowote wa kuboresha soko la zao hili. Wananchi sasa wanapomaliza kuvuna korosho zao wanaambulia vikaratasi tu na kutakiwa wasubiri pesa zao kwa muda mrefu bila kuzipata. Ingawa ni jambo liliowazi kuwa zao la korosho linachangia kiasi kikubwa tu cha fedha katika serikali. Kwa mfano, kuna takwimu zinaonesha kuwa Katika Mwaka wa Uchumi unaoishia Novemba 2012, Korosho imeliingizia Taifa jumla ya dola za Kimarekani 151 milioni sawa na shingi billion mia mbili arobaini na moja na million mia sita (TZsh241,600,000,000). Katika mwaka 2011 zao hili liliingiza dola 130 milioni sawa na bilioni mia mbili na nane (208,000,000,000) wakati Pamba iliingiza dola 53 milioni tu sawa na shingi billion themanini na nne na milioni mia nane (84,800,000,000).


  • Wananchi wa Mtwara na kusini kwa ujumla wanazidi kulia tu na kusuasua kwa ujenzi wa Barabara ya Mtwara-Lindi-Dar es Salaam. Wanazidi kuumia wanapoona ile mikoa inoyoheshimiwa na serikali ikiwa na Barabara nzuri zinazopitika tena ujenzi wake umekamilika kwa muda mfupi sana.
  • Miaka minane ya Mh. Rais Kikwete zile kilomita 60 za barabara kutoka Ndundu mpaka Somanga hazijaisha lakini gesi anataka kuiwekea bomba na mradi ukamilike kwa miezi 18.
  • Wananchi wameshuudia reli ya kusini iking’olewa bila sababu za msingi na huku ikijulikana kuwa reli ni moja ya miundombinu muhimu katika kuchochea uchumi na maendeleo ya jamii kwa ujumla. Reli haikung’olewa katika mikoa ambayo serikali inaiheshimu.
  • Wananchi wa Mtwara wameshuhudi mashine ya maji kitangali Newala ikiondolewa na kupelekwa Dodoma ambayo ilikuwa msaada kutoka Finland.
  • Wananchi wa Mtwara wameshuhudia kiwanda cha samaki Mtwara kikiondolewa na kupelekwa Dar es Salaam.

  • Wananchi wa Mtwara wameshuhudia taa za mwanga mkali za uwanja wa ndege Mtwara ziking’olewa na kupelekwa Arusha.
  • Wananchi wa Mtwara wameshuhudia mkataba wa kutumika bandari ya Mtwara na Malawi kibiashara ukipindishwa na kupelekwa Bagamoyo.
  • Wananchi wa Mtwara wamekaa na giza kwa muda mrefu na giza hilo limechangia kutokuwepo kwa kichocheo cha uchumi kwa kukosekana umeme wenye uhakika.
  • Ni hivi karibuni tu baada ya kugunduliwa gesi na kumekuwepo na nishati ya umeme ambao hautoshi kwa maana ya kumfanya mjasriamali mwenye mtaji kuweza kuwekeza Mtwara katika sekta ya viwanda. Mwenyezi Mungu anasema:-
“Kwa hakika MwenyeziMungu anaamrisha uadilifu,na kufanya ihsani,na kuwapa jamaa(na wengineo),na anakataza uchafu na uovu,na dhuluma.Anakunasihini ili mpate kufahamu(mfuate)”(Qur’an 16:90)

“Na timizeni ahadi mnazozitoa kwa jina la MwenyeziMungu mnapoahidi;wala msivunje hizo ahadi baada ya kuzithubutisha,hali mmekwisha mfanya MwenyeziMungu kuwa shahidi wenu.Hakika MwenyeziMungu anayajua yote mnayoyayafanya”(Qur’an 16:91)

Sasa ghafla, wanakutana na mpango wa kustukiza wa serikali kutaka kusafirisha gesi hiyo kwenda Dar es Salaam bila kueleza kwa nini kituo cha kufulia umeme unaotokana na gesi asilia inakopatikana gesi hiyo kisijengwe Mtwara?. Wanapojaribu kuihoji serikali wanaambulia matusi, kejeli na kupuuzwa kutoka kwa viongozi wao waliowategemea kuwatetea. Kwao wanaona ni hujuma tu wanataka kufanyiwa kama walivyofanyiwa huko nyuma na ndio maana wameamua KUFA na GESI indepo na mara hii serikali itawapuuza. Serikali imefikia upeo wa juu wa kuwapuuza wana Mtwara na WanaMtwara nao wamefikia upeo wa juu wa uvumilivu na ndio maana wanasema GESI KWANZA UHAI BAADAYE. Haya ndio mazingira halisi ambayo ndiyo KIINI cha mgogoro wa gesi Mtwara. Sio wanasiasa bali ni historia ya kudharauliwa ndio yaliyoibua mgogoro huu wa gesi kama tulivyoeleza hapo juu. WanaMtwara wana mfano wa gesi ya Songosongo inayopelekwa Dar es Salaam. Zipo taarifa zinazoelezea kwamba kodi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa asilimi 0.3 (0.3%) ilikuwa inalipwa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala na kampuni ya Pan Africa Energy. Ni baada ya juhudi za mbunge wa Kilwa Kaskazini Murtaza Mangungu kuingilia kati ndio kodi ikaanza kulipwa Kilwa.

TAMKO
SHURA YA MAIMAM INAUNGANA NA WANANCHI WA MIKOA YA KUSINI KUITAKA SERIKALI ISITISHE MPANGO WA KUSAFIRISHA GESI ASILIAYA MTWARA KUPELEKWA DARES-SALAAM NA BADALA YAKE MTAMBO WA KUFUA UMEME WA MEGAWATT 300 UJENGWE MTWARA KAMA ULIVYOKUSUDIWA AWALI KABLA YA USHAURI MBAYA WA TPDC KWA SERIKALI. NA KWA KUWA TUNAAMINI KUWA SERIKALI YETU NI SIKIVU ITATUSIKILIZA WANANCHI WA MIKOA HII YA KUSINI kama ilivyowasikiliza wananchi wote wa Tanzania tulipoitaka serikali kuwa na mjadala kuhusu kuandikwa kwa KATIBA MPYA ingawa msimamo wa serikali mwanzo ulisema katiba iliyopo inakidhi haja za wakati huu.
Ee ALLAH shuhudia kuwa tumefikisha na tumetekeleza wajibu wetu
.
 
Chama cha Mapinduzi katika Ilani yake ya uchaguzi ya mwaka 2010 inatamka wazi katika Ibara ya 63 kifungu cha H na K juu ya gesi ya Mnazibay Mtwara na Songo songo Kilwa, Lindi kuhusu umeme wa (240 MW) Kinyerezi na (300MW) Umeme wa Mnazi bay Mtwara……

-Vifungu hivi vinafafanua:

• Gesi ya Mnazi bay itakuwa kwa ajili ya Mitambo ya kuzalisha umeme ambayo itajengwa Mtwara (300MW)

• Mitambo ya kuchakata gesi kujengwa Mtwara

• Ujenzi wa viwanda Mtwara ili malighafi itokanayo na gesi itumike kutengeneza mbolea, plastic vikiwemo na viwanda vya Cementi

2. Gesi ya Songo songo inafafanua wazi kuwa gesi hiyo itapelekwa Kinyerezi . Dar –es –Salaam kwa madhumuni hayo hayo.

• Kuendeleza viwanda mbali mbali

• Kuzalisha umeme (240 MW)

• Kuchakata gesi kwa kujenga mitambo

Katika ahadi ya Rais wa Jahuri ya Muungano wa Tanzania alizotoa wakati wa Kampeni za uchaguzi katika hotuba yake ya tarehe 29/10/2010 alitamka wazi kuwa Mkoa wa Mtwara uwe tayari kwa maendeleo makubwa ambayo yanakuja kutokana na gesi iliyogunduliwa katika Mkoa wa Mtwara huko Mnazi bay

Ndo maana naipenda JamiiForums kwa kutoa nafasi ya wadau mbalimbali kushusha data za uhakika kama katika nukuu hapo juu * (maandishi rangi nyekundu).

CCM, serikali ya CCM na viongozi wake wakatae sasa hiyo siyo ILANI yao maana kila siku tunasikia wafanyakazi wa serikali wakibanwa watekeleze ILANI ya Uchaguzi ya CCM na si vinginevyo.
 
Muislamu adui yake ni Mkristo,adui wa mkristo ni shetani je muislamu ni nani?Safi sana walokolee nimewakubali mko juu ila sasa naombeni kwenye maandamano muwe mstari wa mbele ili wajue kwamba issue ya gesi ni zaidi ya uhuruu wa nchi
mkuu unaandiko linaloonyesha kuwa muislam adui yake ni mkristo? kuna meseji nimetumiwa hapa na mkristo mmoja inatia kinyaa kwa kweli. naona na wewe ni walewale. hakuna andiko linalosema kuwa adui wa muislam ni mkiristo. ila adui wa muislam ni yule anayetaka kuuharibu uislam kwa vyovyote vile iwavyo. kwa hiyo kama wakristo mnataka kuuharibu basi mtaingia kwenye kundi hilo. Kwa taarifa yako, uislam unafundisha kuishi na wasio waislam vizuri. mafundisho pia yanatufundisha kuishi na jirani yako vizuri bila ya kujali imani yake. mkuu acha kupotosha na kutengenezea watu chuki zisizo na chembe ya ukweli. Anyway unaweza endelea kama wewe si Mtz kwani kikiwaka hutakuwepo.
 
mkuu unaandiko linaloonyesha kuwa muislam adui yake ni mkristo? kuna meseji nimetumiwa hapa na mkristo mmoja inatia kinyaa kwa kweli. naona na wewe ni walewale. hakuna andiko linalosema kuwa adui wa muislam ni mkiristo. ila adui wa muislam ni yule anayetaka kuuharibu uislam kwa vyovyote vile iwavyo. kwa hiyo kama wakristo mnataka kuuharibu basi mtaingia kwenye kundi hilo. Kwa taarifa yako, uislam unafundisha kuishi na wasio waislam vizuri. mafundisho pia yanatufundisha kuishi na jirani yako vizuri bila ya kujali imani yake. mkuu acha kupotosha na kutengenezea watu chuki zisizo na chembe ya ukweli. Anyway unaweza endelea kama wewe si Mtz kwani kikiwaka hutakuwepo.
Huoni aibu kuamini hivyo?Uislamu unafundisha amani na kuishi vizuri na jirani?Kwahiiyo waislamu wote ni vilaza kwamba huwa hawaelewi hayo mafundisha mpaka wanachoma makanisa?Emu kamsikilize Shehe muuaji Ilunga ndo utaujua uislamu ni ush..twan..Mwanafunzi mtoro adui yake ni mwalimu Adui wa mwalimu ni Ujinga hivyo mwanafunzi mtoro ni mjinga..Waislamu ni janga la dunia
 
vitu viwili naviona hapa
1. TAMKO LA MAKANISA
2. TAMKO LA FPCT (MTWARA)

UANDISHI WA STAILI YA MAGAZETI YA UDAKU UNAPOTOSHA SANA
 
Ilani ya uchaguzi siyo biblical. Kwanza ieleweke kuwa Ilani inatekelezwa tu pale inapowekwa katika mipango ya Serkali inapopitishwa na Bunge au mabaraza husika (madiwani). Bahati mbaya wanasiasa wamekuwa wakiimba Ilani na kuwaaminisha wananchi kuwa ni lazima itekelezwe ilivyoandikwa. Ingekuwa hivyo CCM wasingepata uhalali wa kuanzisha mchakato wa Katiba mpya kwa sababu hauko katika Ilani Yao.

Unamaanisha ilani ya uchaguzi na ahadi za viongozi wakati wa kampeni ni utapeli? Kwa hiyo kiongozi au chama kinaweza kuahidi chochote na asiwajibike kutekeleza? Basi hatuhitaji chama wala ilani
 
safi sana viongozi kwa tamko zuri. Jamani wa tz tushikamane, tupendane na tuvumiliane, likinuka viongoz wanatukimbia cc tunabaki tunakufa kma kuku kwa ujinga wetu. Haya bwana cc wengine kikinuka tuna ka uwezo kidogo tunakimbia nchi. Kazi kwenu.
 
Ukiwauliza Ccm leo watasema ilani yao ya uchaguzi haijasema kama ilivyo andikwa.HAta jamaa ni waongo wa ajabu wameshazowea kudanganya kila kukicha.. Sssa wamrumbuka wakimbie kivuli chao sssa.

.
Aisee yaani ilani ya ccm wenyewe wanaikana kuwa haijasema kama ilivyoandikwa? Chichiem kiboko, ila kwa chacha watambue hakuna wa kudanganya tena Tanzania. Kweli tu ndio itawaweka huru.
.
 
.
Aisee yaani ilani ya ccm wenyewe wanaikana kuwa haijasema kama ilivyoandikwa? Chichiem kiboko, ila kwa chacha watambue hakuna wa kudanganya tena Tanzania. Kweli tu ndio itawaweka huru.
.
Ccm na watu wake wapuuuz wanachanganganya wananchi haya ni mambo ya kipuuz tu si wawasikilize wanamtwara?mmeambiwa barabara miaka 51 ya uhuru hazijakamilika,Jakayla kaahidi mambo lukuki mtwara leo bomba lijengwe Mitzi 18 Hata kichaaa hapa ataandamana kuna nini Ndani yake?kwetu huku tarime mambo ya kisenge hakuna,serikali acheni mambo yenu bwana mtafanya watu wampumbavu mpaka lini bwana?
 
Poleni wana ww kusini... Nadhani Sasa mtaelewa kwa nini tunawataka muikatae CCM kwenye chaguzi
 
Askofu Gabriel Mmole wa kanisa katoliki jimbo la mtwara nae atatoa tamko lini?
 
Unamaanisha ilani ya uchaguzi na ahadi za viongozi wakati wa kampeni ni utapeli? Kwa hiyo kiongozi au chama kinaweza kuahidi chochote na asiwajibike kutekeleza? Basi hatuhitaji chama wala ilani

Exterminator
Sisemi kwamba ni utapeli, lakini ifahamike kwamba katika mfumo wa vyama vingi ilani ya uchaguzi siyo biblical kwamba inatekelezwa ilivyo. Kumbuka yanayotekelezwa ni mipango ya Serkali ambayo inakuwa imepitishwa na vyombo husika. Ilani inakupa sera zitakazoongoza utekelezaji wa mipango ya Serkali na ili itekelezwe ni lazima ipitishwe na kupangiwa resources ikiwemo fedha. Bunge si lazima liwe na majority wa chama kilichoshika dola kwamba kila kilichowekwa kwenye Ilani ya chama kitapitishwa vilevile. Lakini pia Ilani za vyama zinaweka mambo mengine ambayo kiuhalisia yawezekana yasitekelezeke. Bahati mbaya tumetoka kwenye mfumo wa chama kimoja ambapo ilikuwa vigumu kutenganisha chama na Serkali (dola) ndiyo maana hata Ilani zingine za uchaguzi ni za ajabu. Unaahidi kujenga barabara, shule, daraja au kuleta maji sehemu Fulani kana kwamba huu si wajibu wa Serkali yoyote inayokuwa madarakani!
 
DINI & SIASA

dini inapotumika kwa nia njema huwa hakuna tatizo, ila dini inapotumika kwa kuzunguka ni tatizo
 
Back
Top Bottom