Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,627
- 154,987
Kuna bwana mmoja alikuwa hana ajira kwa muda mrefu licha ya kuwa alikuwa na elimu ya chuo kikuu.
Ili maisha yaendelee ilibidi ajishikize kwenye ajira ya udereva wa taxi.
Bahati nzuri kulikuwa na ndugu yake aliyekuwa masomoni nje, akamuunganisha na dada mmoja mwenye kampuni kubwa ya clearing and forwarding ili jamaa akaajiriwe kama meneja wa masoko kwenye kampuni hiyo.
Siku ya kukutana na mkurugenzi kwa ajili ya kwenda kufahamiana na kuanza kazi jamaa akaanzia kwenye kijiwe chake cha taxi. Akiwa kijiweni hapo akapita dada mmoja mwenye bonge la wowowo, akiwa anafanya mazoezi ya matembezi ya asubuhi. Taxi dereva msomi akaanza kupiga miluzi na kumfanyia kila aina ya dhihaka yule dada, dada akampuuza na kuendelea na mazoezi yake.
Muda ukafika, jamaa akawasha taxi yake na kuelekea kwenye miadi ya kazi .
Akafika kwenye hiyo ofisi na akaomba kuonana na mkurugenzi. Sekretari akamkaribisha ndani kwa mkurugenzi,. Kwa jinsi alivyokuwa amevalia na kwa kuwa ameketi, jammaa hakumkumbuka yule dada kuwa ndiye aliye mfanyia dhihaka asubuhi, lakini yule dada alimkumbuka vizuri.
Baada ya maongezi, yule dada akamuuliza ukimuona mwanamke mwenye makalio kama yangu huwa una behave vipi?
Dada akainuka na kugeka, jamaa bado hakupata picha.
Dada akamkumbusha mkasa wa asubuhi na kumweleze kuwa ame disqualify hiyo post ya umeneja, kwa hiyo aondoke.
Jamaa akatoka na aibu.
Jamani UHUNI HAULIPI.
Ili maisha yaendelee ilibidi ajishikize kwenye ajira ya udereva wa taxi.
Bahati nzuri kulikuwa na ndugu yake aliyekuwa masomoni nje, akamuunganisha na dada mmoja mwenye kampuni kubwa ya clearing and forwarding ili jamaa akaajiriwe kama meneja wa masoko kwenye kampuni hiyo.
Siku ya kukutana na mkurugenzi kwa ajili ya kwenda kufahamiana na kuanza kazi jamaa akaanzia kwenye kijiwe chake cha taxi. Akiwa kijiweni hapo akapita dada mmoja mwenye bonge la wowowo, akiwa anafanya mazoezi ya matembezi ya asubuhi. Taxi dereva msomi akaanza kupiga miluzi na kumfanyia kila aina ya dhihaka yule dada, dada akampuuza na kuendelea na mazoezi yake.
Muda ukafika, jamaa akawasha taxi yake na kuelekea kwenye miadi ya kazi .
Akafika kwenye hiyo ofisi na akaomba kuonana na mkurugenzi. Sekretari akamkaribisha ndani kwa mkurugenzi,. Kwa jinsi alivyokuwa amevalia na kwa kuwa ameketi, jammaa hakumkumbuka yule dada kuwa ndiye aliye mfanyia dhihaka asubuhi, lakini yule dada alimkumbuka vizuri.
Baada ya maongezi, yule dada akamuuliza ukimuona mwanamke mwenye makalio kama yangu huwa una behave vipi?
Dada akainuka na kugeka, jamaa bado hakupata picha.
Dada akamkumbusha mkasa wa asubuhi na kumweleze kuwa ame disqualify hiyo post ya umeneja, kwa hiyo aondoke.
Jamaa akatoka na aibu.
Jamani UHUNI HAULIPI.