Tambua sababu kuu za vita ya Ethiopia

Tz boy 4tino

JF-Expert Member
Sep 14, 2014
1,598
1,816
Wakati Watu wengi wakiamini sababu kuu ya vita Ethiopia ni ukabila, Jambo hilo siyo kweli.

Sababu kuu ya vita ya Ethiopia ni maslahi mapana ya mabeberu. Hii ni baada ya kutishika na msimamo wa Ethiopia haswa katika utekelezwaji wa miradi ya maendeleo.

Je, ni vipi Ethiopia inatishia maslahi mapana ya mabeberu?

Katika miaka ya karibuni Ethiopia imekuwa ikitekeleza miradi mikubwa ya maendeleo yenye malengo ya kunyanyua watu wake kiuchumi na kuwaondoa katika dimbwi la umasikini.

Baadhi ya miradi hiyo ni kama vile The Grand Renaissance Ethiopia Dam “Bwawa kubwa zaidi barani Afrika , na mabwawa mengine makubwa matatu ambayo yakikamilika yataifanya nchi hiyo kuwa na zaidi ya Mega Watts elfu kumi ( 10,000 MegaWatts ). Kwa lengo la ufafanuzi tu, Mega Watts 10,000 ni zaidi ya umeme unaozalishwa jumuiya ya Afrika Mashariki nzima.

Miradi mengine inayoendelea Ethiopia, ni uboreshaji wa miundombinu, special economic zones n.k.

Je ni vipi miradi hii inahatarisha maslahi ya mabeberu?

- Miradi hii itaenda kufanya asilimia mia ya wananchi wa Ethiopia kuwa na umeme, itaondoa utegemezi wa Ethiopia kwa nchi Za magharibi kwa kiwango kikubwa, unaenda kuifanya Ethiopia kuifanya Ethiopia kuwa huba ya viwanda vya kuongeza thamani hivyo kuuza bidhaa zao kwa bei ya juu.

- Mbali na hayo jambo kubwa linalowaogopesha zaidi nchi za magharibi. Ni namna bwawa kubwa la Ethiopia linavyoweza kuwa msingi wa mapinduzi ya mikataba ya kinyonyaji iliyowekwa na wakoloni , ambayo iliwekwa kwa lengo la kuhakikisha nchi za kusini mwa jangwa la Sahara ( nchi za watu weusi) zinabaki masikini kwa kipindi kirefu.

Miongoni mwa mikataba hiyo ni mkataba wa matumizi ya Mto Nile, kwa muda mrefu nchi Za magharibi zimekuwa zikitumia mkataba huo kuhujumu miradi ya maendeleo katika nchi za Afrika Mashariki haswa inayohusiana na usambazwaji wa Maji na umeme.

Ushindi wa Ethiopia unaonekana waweza kuwa chachu ya mkataba huo kuvunjwa. Kwa ufupi mkataba huo unaipa haki Misri katika upangaji wa matumizi ya mto Nile pamoja na vyanzo vyake vyote jambo ambalo halina mantiki yoyote .

- Sababu kuu ya tatu ni namna utekelezwaji wa miradi mikubwa ya maendeleo nchini Ethiopia inavyotekelezwa. Wakati nchi nyingi Za Afrika hujikuta ikiingia mikataba isiyokuwa na tija, katika utekelezwaji wa miradi ya maendeleo. Mengine ikipelekea hata uuzwaji wa rasilimali muhimu katika mataifa yao. Hali ipo tofauti nchini Ethiopia, kwani nchini humo miradi mingi inamilikiwa na serikali ya nchi hiyo kwa kiwango kikubwa.

Kwa Ethiopia kutekeleza miradi mikubwa ya kiwango kile na mabeberu kutokuwa na chao katika miradi hiyo, ni jambo linalowakwaza sana na linaenda tofauti na maslahi yao mapana ambayo ni kuhakikisha wana udhibiti na nafasi katika miradi mikubwa ya maendeleo inayoendelea katika nchi za kusini mwa jangwa la Sahara.

Tunapozungumzia nchi za Magharibi hapa tunamaanisha zote na haziishii kwa nchi zilizowahi kuwa na makoloni Afrika kama Uingereza, Ufaransa n.k. bali ni nchi zote za magharibi zina obligation ya kutekeleza hii ajenda.

Swala la nchi za magharibi kuhujumu maendeleo ya nchi kusini mwa jangwa la Sahara wala siyo siri na huko nyuma kabla ya maendeleo ya sayansi na teknolojia, hiyo mikakati walikuwa wakijadili wazi kwenye mabunge yao Ulaya.




Hizi ni baadhi tu ya sababu kwa nini ile vita ni zaidi ya wengi wafikiriavyo. Kwa ufupi tu , yote yanayoendelea nchini Ethiopia ni kutokana na tishiyo la maslahi mapana ya mabeberu, hamna swala ukabila/uonevu, wala bwawa la Ethiopia kutishia janga la upatikanaji wa maji nchini Misri. Zote ni propaganda.
 
Asili ya makabila mengi ya Kaskazini mwa Tanzania hasa Arusha na Kilimanjaro ni Ethiopia. Mfano,Wapare,Wachaga na Wambulu,ukiangalia hata sura zao hasa vichwa vina mfano mkubwa na Waithopia.

Maana yangu ni nini? Ni kuwa, aina ya Maendeleo yanayotafutwa au yaliyopo Kaskazini yanalandana na ya Waethiopia. Maendeleo ya aina hizo ni inborn na hayategemei misaada sana,ni wao wenyewe!

Watu wa aina hiyo hawachelewi kuzushiwa mengi, kuchonganishwa nk ili kuwapunguza kasi.
 
Asili ya makabila mengi ya Kaskazini mwa Tanzania hasa Arusha na Kilimanjaro ni Ethiopia. Mfano,Wapare,Wachaga na Wambulu,ukiangalia hata sura zao hasa vichwa vina mfano mkubwa na Waithopia.

Maana yangu ni nini? Ni kuwa, aina ya Maendeleo yanayotafutwa au yaliyopo Kaskazini yanalandana na ya Waethiopia. Maendeleo ya aina hizo ni inborn na hayategemei misaada sana,ni wao wenyewe!

Watu wa aina hiyo hawachelewi kuzushiwa mengi, kuchonganishwa nk ili kuwapunguza kasi.
Wewe ni mtu muongo sana..kama hujui kitu nyamaza. Wapare na wachaga ni wabantu. Idiot!
 
Shida yangu kubwa siyo nchi za magharibi kuipendelea Misri ila namna nchi za maziwa makuu zilivyopiga kimya badala ya kuja na kauli moja kuiunga mkono Ethiopia.
 
Umeandika vizuri saana lakini mbali na mkono wa mataifa ya magharibi ile nchi pia ukabila unaigharimu saana. Hii vita misingi yake ni ukabila lakini mataifa ya magharibi yamejipenyeza kuchochea vurugu kupitia mgongo wa kikabila. Suala la ukabila lipo serious kupita unavyofikiria Ethiopia. Ni kitu cha kawaida kabisa kukuta makabila fulani hawaoleani na wala hawawezi kukaa eneo moja.

Vita hivi msingi mkubwa ni madaraka na ukabila, Meles Zenawi alipoitwaa nchi kijeshi kutoka kwa dikteta mwenzake Mengistu alipandikiza chuki mbaya kupita kiasi ya ukabila kwa kuipendelea kwa wazi kabisa kabila yake ya Tigray ilhali ni kijikabila kidogo kabisa Ethiopia kikiachwa mbali na majority Oromo na Amhara.

Serikali yake zaidi ya 90% ilikuwa ni watigray kwenye top positions. Mbaya zaidi hata kimaendeleo alipaendeleza zaidi Tigray region na kupatelekeza kwenye jamii nyingine hasa zaidi kwa hawa majority Oromo na Amhara. Ni katika kipindi chake cha utawala ndiyo vikundi vya uasi vilishamiri zaidi Ethiopia vikiundwa kwa misingi ya ukabila na vikipigania kujitenga kutoka Ethiopia.

Abby Ahmed kaingia madarakani na akataka kuondoa hali hiyo, yaani kutafuta sura ya kitaifa kwenye serikali yake badala ya kuwa na serikali iliyokuwa dominated na Tigray. Hicho kitendo kiliwakera watigray ndiyo wakajitangazia uasi dhidi ya federal govt ya Abby.
Mataifa ya magharibi yanaitamani destabilised Ethiopia ili kuendelea kucontrol lango la red sea ambalo lina umuhimu mkubwa sana kibiashara na kilichowatisha zaidi ni ukaribu wa kupita kiasi kati ya serikali ya Abby na wachina (Katika nchi ambazo mchina amewekeza na ameikopesha kwa afrika Ethiopia ipo top 3 kama sio ya kwanza . Wamagharibi wakaona watapoteza ushawishi katika kuicontrol red sea lango kuu la biashara kati ya Ulaya Magharibi na Asia na Africa pia kwa ujumla wake, hivyo kilivyonukishwa tu na watigray basi na wao ndiyo wakatia maguu mazima.

Hii vita sioni dalili ya kuisha leo wala kesho kutokana na uchochezi unaofanywa na mataifa ya magharibi, na Abbiy akiendelea kukaza itaugharimu sana uchumi wa Ethiopia kitu kinachoweza kuchochea uasi kutoka kwenye jamii nyingine dhidi ya serikali yake. Sasa hivi inflation rate ya fedha ya kihabeshi (Birr) dhidi ya fedha za kigeni inatisha kupita kiasi.
 
Utamu wa siasa za kibeberu ni kuwa hata bwana mkubwa aliiingizwa mkenge na Mabeberu kwa kumtumia kibaraka wa kujenga Mwalimu Nyerere Hydro electric power kwa kutumia vibaraka wao Misri
 
EAC mpaka kuleee! zimbabwe kabla ya mkoloni ilikuwa ni sehemu ya ethiopia lkn wakoloni walifanya yao kupitia mikataba mibovu ya Berlin....hii ikabadilisha Historia ya africa
 
Back
Top Bottom