youngkato
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 3,638
- 3,641
Kabla ya kuomba leseni ya biashara, ni muhimu kujua upo kwenye kundi gani. Kila aina ya biashara ina leseni yake kulingana na ukubwa wa mtaji na huduma inayotolewa. Hii ndiyo njia ya kuhakikisha unaanza safari yako ya kibiashara kwa usahihi na kisheria.
Leseni Kundi A ni Kwa Biashara Kubwa
Hili ni kundi la biashara zenye mtaji mkubwa na athari pana kwa uchumi. Zinafanyiwa tathmini na taasisi ya kitaifa (BRELA) na huhitaji maandalizi ya kina. Mifano ya biashara katika kundi hili ni:
- Biashara za kuuza bidhaa nje ya nchi (exporters)
3. Bandari, vilabu vya usiku, bima
4. Huduma za utalii
5. Benki na taasisi za kifedha
6. Maduka ya kubadilisha fedha (bureau de change)
Mamlaka ya kutoa leseni: Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA)
Leseni Kundi B ni Kwa Biashara Ndogo na Za Kati
Hiki ni kundi kwa wajasiriamali na wafanyabiashara wengi wa kawaida. Kama unamiliki au unapanga kufungua moja ya hizi, basi upo Kundi B:
- Migahawa na hoteli za kawaida
3. Wakala wa bima na usajili wa abiria
4. Viwanda vidogo
5. Udalali, ushauri wa kitaalamu, na huduma nyingine za taaluma
6. Uuzaji wa bidhaa kwa jumla au rejareja
Leseni hutolewa na: Afisa Biashara wa Halmashauri yako ya Mtaa, Wilaya au Jiji.
Kwa nini hii ni muhimu?
Kujua kundi lako hukuwezesha kuandaa nyaraka sahihi, kulipa ada sahihi, na kuepuka kucheleweshwa au kukataliwa kwa maombi yako ya leseni.Sisi tunakusaidia kuchagua kundi sahihi, kukusanya nyaraka na kukamilisha mchakato wa kupata leseni yako ya biashara kwa haraka!
📞 Wasiliana nasi sasa: +255693880325