Takwimu za Deni la Taifa kwa sasa

Takwimu za Deni la Taifa kwa sasa

Wanakopa tu hawajali ili wajenge mavituvitu ambayo mengine siyo ya maana

Ngoja siku washtukie Jeshi la Mabeberu limeuzingira mlima Kilimanjaro kwamba wataendesha utalii miaka 200 kujilipa deni kisha ndo waturudishie!
 
Rais wetu ataendelea tu hamna hoja waponzani 2020 ni kupita bila kipingamizi,deni litalipwa tu
 
Napata hisia mbaya uyu raisi akimaliza muda wake yatatokea makesi mengi sana ya kudai fidia na kesi nyingi serikali itaangukia pua na itashindwa kulipa kwa yale madeni makubwa sana mwisho wa siku ni makubaliano katika mikataba fulani ata kama ni ya kinyonyaji lakini zitatumika rasilimali zetu kulipa madeni pole pole na hapo ndio itaonekana nchi imekwama
 
Yaani hapa ndipo ninapoamini kwamba hawa vijana wa Lumumba wanaotoa mapambio kila siku na sasa kaka yao Pascal Mayalla kaamua kujiunga nao kuna chochote kitu wanakipata..maana kwa akili ya kawaida huwezi kuona mambo yanakwenda hovyo na ukasifu kwamba yanakwenda vizuri ni ukichaa wa hali ya juu kufanya hivyo
Mkuu Kiluwiluwi cha Chura, Tadpole, it's just an attitude of mind, unaiangalia Tanzania kwa mtizamo gani in between positive attitude or negative attitude. Ukiamua kuangalia from negative perspective kutafuta mabaya tuu na mapungufu, then utakacho ona ni mabaya tuu hivyo unaweza kumuona Magufuli na serikali yake ya awamu ya tano kama ni mashetani na hawana zuri au jema lolote na hata wakifanya mema, utatafuta kasoro.

Lakini ukiamua kuangalia with positive perspective kuangazia mema na mazuri, then utayaona hayo mema na mazuri, hivyo ukimpima Magufuli alipoingia aliikuta wapi Tanzania na sasa ameifikisha wapi, utakubaliana na ukweli halisi, something is being done, hivyo kwa watu wenye positive outlook kwao Magufuli ni kama masiya fulani aliyeletwa na Mungu kuikomboa Tanzania, kutoka nchi masikini ya kutupwa hadi nchi ya uchumi wa kati.
P
 
Kwa neno moja tu tunaweza kusema, Mzee Mkapa alikuwa ni "Mpiganaji wa uchumi".
Nyie watu hamjui mnataka nini
2015 mlikua mnapiga kelele mkapa kaua uchumi kauza mashirika yenye nguvu kwa bei ya kutupa kama NBC,SIGARA NA TBL,mkaenda mbali zaidi kutaka afungwe kwa kujimilikisha mgodi wa kiwira kwa shilingi milioni 70,leo umekuja na ugunduzi mpya kuwa mkapa alikua mpiganaji uchumi!!
Yooote haya kutafuta kumfanya Magufuli aonekane si lolote mpaka mnasahau maandishi yenu yapo humu ukibisha nakutolea thread zako ulizokua ukisema mkapa fisadi
 
Uchanganuzi wako (analysis) ni shallow.

Usiliangalie deni kwa kiasi tu (value), chukua deni kisha gawanya kwa pato la taifa.

Nikupe mfano: Mtu mwenye kipato cha 100,000 na deni la 60,000 ana hali mbaya kuliko mtu mwenye kipato cha 1,000,000 na deni la 500,000 licha ya kwamba mwenye 500,000 ana deni kubwa kuliko mwenye deni la 60,000 (ability to service the debt).

Pato la taifa katika awamu ya Nyerere na pato la taifa wakati wa Magufuli ni vitu viwili tofauti kabisa. Uchambuzi wako ungejitosheleza endapo ungekuja na takwimu za kipato wakati wa Nyerere na Wakati wa Magufuli.


Wewe unaye bisha ndio unatakiwa uje na uchambuzi wako wa kutete.ukiulizwa kwa nini wakati wa mkapa yeye alipunguza kutoka 18T hadi 10T sijui utasemeje??
 
Nyie watu hamjui mnataka nini
2015 mlikua mnapiga kelele mkapa kaua uchumi kauza mashirika yenye nguvu kwa bei ya kutupa kama NBC,SIGARA NA TBL,mkaenda mbali zaidi kutaka afungwe kwa kujimilikisha mgodi wa kiwira kwa shilingi milioni 70,leo umekuja na ugunduzi mpya kuwa mkapa alikua mpiganaji uchumi!!
Yooote haya kutafuta kumfanya Magufuli aonekane si lolote mpaka mnasahau maandishi yenu yapo humu ukibisha nakutolea thread zako ulizokua ukisema mkapa fisadi
Yes,inawezekana angesimamia ubinafisishaji vizuri basi uchumi kwa kipindi kile ungekuwa zaidi ya hapo.kuongezeka kwa uchumi kipindi chake haiondoi maana kuwa alifanya ufisadi.
 
Mkuu Kiluwiluwi cha Chura, Tadpole, it's just an attitude of mind, unaiangalia Tanzania kwa mtizamo gani in between positive attitude or negative attitude. Ukiamua kuangalia from negative perspective kutafuta mabaya tuu na mapungufu, then utakacho ona ni mabaya tuu hivyo unaweza kumuona Magufuli na serikali yake ya awamu ya tano kama ni mashetani na hawana zuri au jema lolote na hata wakifanya mema, utatafuta kasoro.
Lakini ukiamua kuangalia with positive perspective kuangazia mema na mazuri, then utayaona hayo mema na mazuri, hivyo ukimpima Magufuli alipoingia aliikuta wapi Tanzania na sasa ameifikisha wapi, utakubaliana na ukweli halisi, something is being done, hivyo kwa watu wenye positive outlook kwao Magufuli ni kama masiya fulani aliyeletwa na Mungu kuikomboa Tanzania, kutoka nchi masikini ya kutupwa hadi nchi ya uchumi wa kati.
P
..Naam mkuu pasco tumeingia uchumi wa kati je ni serikali ya awamu ya tano ndio iliyotufikisha hapa kwa miaka hii minne?....je ni strategies gani zinazoonekana zimefanywa na Magufuli kutufikisha hapa tulipo? je ni ujenzi wa miundombinu tu ndio umetufikisha kwenye uchumi wa kati?

Magufuli kaendeleza pale ambapo aliishia mtangulizi wake aliyepita na huyu hasa ndie aliyetufikisha kwenye uchumi wa kati kwa asilimia 80% kwa kuwa ameondoka uchumi ukiwa unapaa kwa asilimia 7..kuja Magufuli kasi ya ukuaji wa uchumi ikashuka jiulize tumefikaje uchumi wa kati na kasi ya ukuaji imeshuka? kwa asilimia kadhaa?

Magufuli nampa heko kwa kupambana na mafisadi tu ila suala la uchumi amefeli vibaya mno na nashangaa hizi sifa anazopewa zinatoka wapi? hapo ndipo nnapokuwa na walakini tena nikashangaa hadi wewe una ushaidi kabisa ya kuwa uchumi unakufa(Rejea thread yako uliyoandika na ukasema hali imekuwa ngumu mmelazimika kufunga kampuni yenu na kupunguza wafanyakazi kwa asilimia kubwa tu).

Pia sekta nyingine rejea korosh,mbaazi(kwenye kilimo),sekta binafsi kila siku zinakufa pia kijamii tunaona kabisa kuna ukiukwaji mkubwa sana wa haki za binadamu kuliko awamu zote.

Ninachojiiliza kwanini nyie waimba mapambio wake mnayaona haya lakini mnazidi tu kusifu? tena ikizingatia wewe ulijua kabisa raisi atakayekuja ni Magufuli na ukatutahadharisha kwamba jamaa ni mbabe ana maamuzi ya ajabu sana(means ulimjua vizuri kitambo sana) na ukasema kuwa hukubali yeye kuwa raisi iweje leo unatumia nguvu kubwa kuunga mkono mazuri na kuacha kukosoa anapokosea?kwanini hutaki kubalance mizani?
 
Hatuwezi kuwa na deni hilo wakati tunajenga miradi mikubwa kama SGR, Stigula goji, ndege tumenunua kwa cash yote hiyo ni kwa pesa yetu ya ndani tuliyoibana toka kwa nafisadi. Rais haendi nje tumebana matumizi sana. Sasa deni linaongezeka kutokana na nini?! Tafadhali rais itisha mkutano ikulu TBC live kukanusha uongo wa mabeberu hawa
 
Safari hii tutafunga Mstaafu.............
Tena bila kubadili katiba.........
Maana hata yeye ameivunja sana........
Msitutanie kabsaa......
Hakuna ku-balanceana tena......
 
Hii imekaa vibaya mno na ukweli mchungu kwa wale wa kusupport maendeleo ya awamu hii ya tano.
Nalog off
 
Dola moja wakati wa JKN ilikuwa sh ngapi?
Dola moja wakati wa AHM je?
Wakati wa BWM?
Wakati wa JK?

Ngoja twende pamoja, Mwaka 1985 wakati Nyerere anaondoka madarakani, deni la Taifa lilikuwa shilingi Trilion 3 na Dola ya kimarekani wakati ule ilikuwa Dola Moja sawa na Shilingi 102, Kwa hiyo ukichukua Trilion 3 ukagawa na 102 Maana yake ni kwamba Mwalimu aliacha Deni la DOLA BILIONI 29.41

Wakati Mwinyi anaondoka Madarkani mwaka 1985, Dola Moja ilikuwa ni sawa na shilingi 500, Kwa hiyo kama deni lilikuwa ni shilingi Trilion 18, Maana yake ni kwamba Ukichukua Trilion 18 gawanya kwa 500, Kwa hiyo mzee Mwinyi aliacha deni la Dola Bilioni 36

Wakati Beni anaondoka Madarakani Deni lilikuwa Shilingi Trilion 10, na exchange Rate ya Dola wakati huo ilikuwa dola moja sawa na sh 1050, Kwa hiyo ukichukua Trilion 10 gawanya kwa 1050 unapata Dola Bilion 9.52

Wakati JK anaondoka Dola moja ilikuwa inabadirishwa kwa sh 2200 na Deni lilikuwa Trilion 45, Ambapo ukiziweka katika dola hizi maana yake JK aliacha deni la dola Bilion 20.4

Katika Miaka Minne ya Raisi Magufuli Deni ni Trilion 61, Exchange rate ni sh 2300 per USD, tukiliweka hilo deni interms of USD Maana yake ni kwamba deni letu ni dola Bilion 26.4

Kwa Hiyo Relatively Utaon kwamba

Katika Utawala Mzima wa Mwinyi wa Miaka 10, Aliongeza deni kwa Dola bilion 36-29.41= 6.59

Mkapa alipunguza deni kwa 9.52-36 =-26.48
HAPA TUMPE KONGOLE SANA MZEE MKAPA ALIPIGA DIPLOMASIA YA MAANA, KAZI NZURI MNO MPAKA TUKAPUNGUZIWA DENI LA DOLA ZAIDI YA BILION 26

Jk yeye aliongeza deni kwa dola bilioni 20.4-9.52 = 10.33
JK aliongeza Deni la Dola bilion 10.33 Ndani ya miaka 10

Magufuli Ndani ya Miaka 4 ameongeza deni kwa dola bilion 26.4-20.4 = Dola Bilion 6
Ndani ya Miaka Minne Tu ya Utawala wake Magufuli kaongeza Deni kwa Dola Bilion 6

Hitimisho:
Pamoja na kwamba Kipindi Cha JKN tunaona deni kama dogo, lakini kwa mujibu wa Exchange Rate za wakati huo Lile lilikuwa ni deni Kubwa Kishenzi kuliko deni tulilonalo leo: Shilingi ya miaka hiyo ilikuwa na Thamani kubwa mno, na data zimeonyesha hivyo

Mzee Mkapa alipiga kazi Ya Kustahiki Medani ya Heshima kwa kuwezesha kuendesha diplomasia kali mpaka tukasamehewa zaidi ya Dola Bilion 26

Ukopaji wa AHM ulikuwa ni wa wastani wa dola bilion 6.59/10 =0.659 Billion Dollars kwa mwaka


Ukopaji wa JK ulikuwa ni wa watani wa Dola 10.33/10 = 1.3 Billion Dollars kwa mwaka

Ukopaji wa Magufuli ni wa wastani wa Dola Bilion 6/4 =1.5 Billion Dollars kwa mwaka
Kwa hiyo maana yake ni kwamba akitawala miaka 10, anaweza kutuongezea deni la trilion 15 katika deni aliloacha JK

Kiufupi ni kwamba JPM awe makini kwenye kukopa , kasi yake ya ukopaji ni kubwa mno, Rate yake ya Ukopaji ni kubwa kuliko rate ya Maraisi wote waliopita, Apunguze!
 
Mbona tunaaminishwa kwamba serikali inaokoa fedha nyingi sana...

Sasa inakuaje tena deni kuongezeka kwa kasi hivyo...



Cc: mahondaw
 
Si ndiyo tume nunua madege na mkulima amekamata moja

Tuna pesa za kutosha mpaka hatujui Trillion1.5 zimeenda wapi... inakuaje tena deni kuongezeka maradufu...

Fedha nyingi zimeokolewa kwa kutowapandishia wafanyakazi mishahara yao... inakuaje deni kuongezeka maradufu...


Cc: mahondaw
 
Back
Top Bottom