SOTI
Member
- Sep 9, 2011
- 79
- 22
Kwa aliyefuatilia mjadala HotMix EATV ataamini kuwa kuna uchakachuaji wa hali ya juu kuhusu idadi ya wajumbe. Takwimu zilizo kwenye katiba zinaonesha Zanzibar wajumbe 212 na Bara 416 jumla 628. 2/3 ya zanzibar kwa takwimu hizi ni wajumbe 142. Siku ya kutangazwa matokeo tuliambiwa na katibu wa bunge kuwa Zanzibar ni 219 ambapo 2/3 ni 146 wakati bara ilikuwa 411 jumla 630. Kumbuka mwanzoni idadi ilikuwa Zanzibar 210 na Bara 419 jumla 629. Waliopewa jukumu la kudanganya umma wamefanya kosa kubwa sana kushindwa kuweka sawa takwimu. Kwa takwimu hizi hata kama haujui statistics ni dhairi tumedanganywa lakini Mungu Kawaumbua.