TAKUKURU wamchefua Magufuli huko Dodoma

TAKUKURU wamchefua Magufuli huko Dodoma

Tabutupu

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2010
Posts
13,262
Reaction score
18,711
Ila TAKUKURU mmeonyesha mpo kutekeleza mambo ya kutumwa , vichwani zero kabisa.

Hivi jengo kama hili, na mnamwita Rais aje kuzindua, akili kweli hizi.

Magufuli amewaonya kwamba waache kujipendekeza kwa kutaka kujenga ofisi Chato.

Inaonekana afande wa TAKUKURU hamna kitu na anacho waza yeye ni kujipendekeza.

.
20200722_142757.jpeg
20200722_140555.jpeg
 
Kazi kweli, tunakoenda wateule si kila kitu ni cha kumwita mheshimiwa afungue vingine ni vya kawaida sana hata Diwani angeweza kufungua jengo kama hilo. Hakika alilingani na Thamani ya Pesa
 
Hii hata tajiri mtoto Kiduku Lilo hawezi kulaza wafanyakazi wake wa nyumbani maana ni ndogo na ya gharama ya kiwango cha barabara ya vumbi.

Tena unamwalika bosi wako aje kuzindua hili banda kweli??!!
Kutumbuliwa kwingine watu wanajitakia.
Nahisi leo huyu anatumbuliwa
 
Kwa alivyochefukwa leo huyo mjeda amekalia kuti kavu anaweza kutenguliwa make amemuonya kwa kumwambia ajiangalie vinginevyo atamvua nyota zake hadharani
 
TAKUKURU wameonyesha zarau kwa muh Rais kwa kumfananisha na kijengo ambacho hakina hadhi ya kuzinduliwa hata na Ndugai.
 
Mkurugenzi wa Takukuru amefeli kwenye maelekezo aliyopewa ya kuwatafutia kesi Chadema. Kwa speech ya mzee leo imeonekana kabisa kuwa Mwanajeshi alisimama kwenye nafasi yake na akataka kufunga jalada la chadema.

Mzee Magu akifanya kitu lazimaga kiwe na sababu nyuma yake.
 
Tuweke ushabiki pembeni, magufuli ana mapungufu yake kama binadamu lkn ukiitazama speech ya leo utagundua huyu jamaa yuko vizuri, kuanzia dhamira yake na hata uwezo wake wa kukemea mambo ya kipumbavu kwa baadhi ya watendaji wake.
 
Back
Top Bottom