TAKUKURU: Manispaa ya Mpanda imelipa Tsh. 220M kinyume na utaratibu, yakaletwa mabati yasiyo na kiwango

TAKUKURU: Manispaa ya Mpanda imelipa Tsh. 220M kinyume na utaratibu, yakaletwa mabati yasiyo na kiwango

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) Mkoa wa Katavi, imebaini mabati yenye thamani ya fedha Sh Milioni 220 yaliyonunuliwa kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari ya wavulana Katavi na Sekondari Rungwa kuwa yako chini ya kiwango.

Kaimu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Katavi, Daud Lyamongo akitoa taarifa ya ufuatiliaji wa utelelezaji wa Miradi ya Maendelo ya Robo Mwaka, Mei 27, 2025 amesema taasisi hiyo ilikagua miradi miwili ya elimu yenye thamani ya Sh Bilioni 4.3 na kubaini kasoro.

Lyamongo amefafanua baada TAKUKURU baada ya kufanya ukaguzi wa miradi hiyo walibaini Mzabuni alilipwa Sh 220,023,980 na Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kabla ya mabati kufika eneo la ujenzi kinyume na utaratibu.
 
Sasa Takukuru yeye kuchunguza tu, hana meno ya kuwapeleka Mahakamani?.wizi wa wazi wa aina hii utasikia Watuhumiwa wameshinda kesi...Rushwa Rushwa kila eneo.
 
Mambo ya ajabu sana nchi hii Bado yanafanyika. Usikute Mzabini akawa ni moja ya viongozi wakubwa wa Manispaa hapo hapo, Rubishi kabisa
 
kweli uchaguzi umekaribia yaani hawa umbwa ripoti ya CAG imeonyesha matakataka na madudu kibao hawajawahi kuinua hata pua zao leo hii nawasikia kila siku eti wanaokoa fedha , nchi ya kusadikika na mauzauza.
 
Back
Top Bottom