Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Wadau, hivi hawa Takukuru wameshindwa kazi? Wameshindwa kabisa kubaini chanzo (origin) ya kadi feki za CCM lukuki zilizotumika katika kura za maoni za chama hicho hivi karibuni?
Inavyoonekana ni kwamba ama hawataki kufanya uchunguzi wa kina kuhusu chanzo cha kadi hizo -- kwa maana ya kubaini kiwanda/viwanda na wamiliki/mmiliki wake -- au wamekatazwa kufanya uchunguzi wa kina.
Hii inashangaza na kuchekesha -- na hapo ndiyo tunaona kuwa harakati zote za Taasisi hiyo katika zoezi zima la kura za maoni za CCM hazikuwa lolote bali ni kiini macho tu, au changa tu la machoni -- na lengo kuu ni kujaribu kuweka/ku-enforce maadili ndani ya chama hicho, maadili ambayo yanaendelea kutoweka kila siku au tayari yametoweka kabisa.
Huwezi kutangaza zimekamatwa kadi feki -- huku hufanyi jitihada zozote kujua nani mhusika mkuu wa kadi hizo. Ni rahisi kumuuliza yule aliyekamatwa nazo wapi kazipata, kama ni tawi la CCM, maafisa husika nao waulizwe -- vivyo hivyo hadi kufikia mtu wa mwisho. Ni rahisi tu, unless huyo mhusika (origin) ni mtu mkubwa katika CCM -- na katika nchi pia -- ambaye hatakiwi akaguswa kwani yeye ni Mungu-mtu.
Na hili ndilo ninalosuspect -- ndiyo maana mtiririko mzima wa ku-trace hizo kadi feki hautakiwi kufanywa.
Nadhani wadau mnaweza kubaini ni nani au akina nani katika nchi hii wenye sifa hizi za U-Mungu-mtu.
Inanikumbusha suala la wizi wa EPA uliofanywa na kampuni ya Kagoda. Pamoja na kwamba mabilioni yale yalipitia matawi ya benki za CRDB na kulipwa kwa mwizi/wezi husika, lakini Takukuru haikutaka, au ilikatazwa kufuatilia mtiririko wa wapi fedha hizo ziliishia baada ya kutoka benki. Takukuru wamekuwa mabubu hapo.
Rafiki yangu kutoka Wilaya ya Nzega kanieleza kuwa Takukuru hawakuonekana kabisa wakifanya kazi yao, bila shaka kwa maelekezo -- kwamba wasiuingilie mchakato wa jimbo hilo la uchaguzi. Anasema siku chache kabla ya kura za maoni katika jimbo hilo maafisa wa Takukuru kutoka mkoani Tabora waliamrishwa kurudia njiani wakati walikuwa wakisafiri kuelekea Nzega.
Anasema katika jimbo hilo mamia ya kadi feki zilitumika bila pingamizi zozote, kwani kulikuwa hakuna mamlaka ya kuzifuatilia.
Takukuru, kweli hamna kabisa na uchungu wa nchi hii, katika kusaidia kuleta haki na maadili ili kuepusha farakano katika nchi hii huko baadaye?