Tunashkur mkuu,cc ambao 2ko mikoani huku huwa tunaonewaga!SASA hata nikija Tz,nakuwa carefu na sampo kama izo
Ha..ha..ha..ha Ajira millioni moja za Kikwete.
Wewe ulitaka fanya nini hapa?
Hawa jamaa ni hatari, wamenijaribu mara kadhaa bila mafanikio..Huwa natumia principle yangu moja tu "I dont mess with anyone I dont know". Kuna siku jamaa alinisimamisha maeneo ya ubungo stand ya mkoa kwenye kituo cha basi kwenda mjini majira ya saa mbili kasoro usiku na kuanza mazungumzo nami
Jamaa: Samahani za leo
Mimi:Nzuri
Jamaa: Hapa naweza pata gari za masaki?
Mimi:Hapana,labda upande gari za msasani halafu ukapande gari nyingine mbele kwa mbele ,kondakta atakueleza zaidi
Tukiwa tunaendelea na mazungumzo akajitokeza mshikaji aliyeonekana kufuatilia maongezi yetu na kudakia mazungumzo nitamwita rafiki
Rafiki: ebwana vipi, anataka kwenda Masaki?
Mimi: Ndio
Rafiki: Sasa hapa unapanda gari za Msasani ukishuka unapanda bajaji,kwani unaelekea Masaki sehemu gani?
Jamaa:Barrick
Rafiki: Barrick saa mbili usiku huu? au una appointment na mtu pale?
Jamaa:Ndio,nina madini nauza kuna mtu pale naenda kuonana nae anisaidie kunielekeza wapi nitauza kirahisi
Rafiki: Ebwana angalia mjini hapa mzee,kuwa makini! Sasa hakuna shida mimi najua masoko tutakusaidia na mshikaji hapa utauza hayo madini ila na sisi itabidi ututoe.
Jamaa: Sawa haina shida,nitashukuru sana
Mimi: Sasa kwa sababu rafiki anajua mahali pa wewe kuuza madini yako atakusaidia mimi nina mambo yangu mengi nikasepa
Nikaondoka kisha nikasimama mbele kidogo kuna jamaa anauza pweza nikanza gonga kipande moja baada ya nyingine huku nawacheki kwa kuibia,walikuwa wakiniangalia kwa makini na hasira hivi,kama watu wanaotafuta namna ya kuni attack.baada ya dakika chache nilipotupa jicho sikuwaona tena..
Kuwa makini na matapeli na usisahau hawana alama usoni!!
kweli mkuu inabidi tukate bima..ila kwa upepo huu unaweza kukuta hata bima bado ukapewa ya kuchakachuaKikatie bima kilaputopu chako wasije kukuzidi mahesabu watoto wa jiji.
Hawa jamaa ni hatari sana maana hawana alama usoni. Ni kuwa makini tu.
mbaya zaidi, hawa jamaa wanafuatilia watu tokea bank..hii ilitokea kwa mama flani ninayemfahamu ..ambaye alifuatiliwa na mwanamke mwenzake ambaye alimtapeli kwa staili kama hiyo ya dhahabu..na kuchukua laki 4 zake...nadhani wanatumia dawa pia..maana huyo mama kazubaa anakuja shtuka baadae hata hata senti kwenye pochi..ikabidi apigiewatu simu kwenda mchukua alipo maana hata nauli hakua nayo...so issue ya dhahabu au madini achaneni nayo....na si kila mtu ni wa kuongea nae....unatiririka tu,....wengine sio watu...
Wengine wanakuwa na mambo ya ushirikina kwa hiyo unakuwa kama umepumbazwa vile. Ukishaibiwa ndio fahamu zinakurudia..Wanaoibiwa nao maboya sana. Yaani mtu anakuambia ana madini ya dhahabu halafu wewe unaamini kirahisirahisi tu.
Wanaoibiwa nao maboya sana. Yaani mtu anakuambia ana madini ya dhahabu halafu wewe unaamini kirahisirahisi tu.
Kuna dada mmoja maeneo ya kimara mwisho naye yalimkuta hayo.Alijikuta anawapeleka matapeli waliodai ni waganga nyumbani kwake.Walimwambia kwamba walioteshwa kuhusu matatizo aliyonayo na kwamba wangempatia tiba.Dada alijikuta akiwapeleka home na kuwakabidhi bila hofu wala wasi TV,radio,woofer n.k.Ile jamaa wanampa kisogo tu ndo akastukia jina la mchezo kwamba keshapigwa na wajanja,i mean ameogeshwa roundabout saa 6 mchana kweupeeee bila ukungu.Hakuna cha sababu za kumcheka!hawa jamb ni noma siku hiz wanatumia mazingambwe....
Kuna dada mmoja maeneo ya kimara mwisho naye yalimkuta hayo.Alijikuta anawapeleka matapeli waliodai ni waganga nyumbani kwake.Walimwambia kwamba walioteshwa kuhusu matatizo aliyonayo na kwamba wangempatia tiba.Dada alijikuta akiwapeleka home na kuwakabidhi bila hofu wala wasi TV,radio,woofer n.k.Ile jamaa wanampa kisogo tu ndo akastukia jina la mchezo kwamba keshapigwa na wajanja,i mean ameogeshwa roundabout saa 6 mchana kweupeeee bila ukungu.