Take a look

Take a look

Daaa...kweli nimekumbuka Tarime sec,shule kama jeshi..mwenye nguvu ndo anakula wazembe mtabaki kuona struggle 4 food pembeeni...bwaloni mkono kila siku,wanafunzi 80% wababe na kauzu mbaya,nawakumbuka wapishi wakongwe kama Mzee chris huyu anakupiga uparo(chakula kidogo) ukiomba akuongezee unasikia" karibu kesho"! Mama mariana,mwita na wengine wengi.MSOSI huo ilikuwa ijumaa yaani toka asubuhi unawaza utapateje msosi,so inawabidi kutengeneza team ya mapambano ili atleast kutoka na kitu. Nakumbuka sufuria likibebwa juu na uji,ugali,makande,wali,maharage linashuka chini tupu! Alafu hapo wanafunz wameungua vibaya,ni mwendo wa kuwakimbiza hospital. Mitaa ya buhemba,FDC na mazoez ndo ilikuwa mitaa ya wanajeshi wa tarime sec kujidai,mtaani wakurya wanatuogopa vibaya ukivaa t-shirt ya Tarime sec basi wewe mfalme kila unapopita ni kidole unanyooshewa,NAKUMBUKA form one yetu tuliteswa sana,tulipigwa sana,tulinyanyaswa sana na matokeo yake wanafunzi tukawa tunalala juu ya miti usiku kukwepa kipigo bwenini! Kuna mwezetu alipoteza maisha kwa kipigo,kweli mwanafunz wa tarime sec ni full mwanajesh ni kukosa gwanda tu.
 
Enzi hizoooo mwaka 1999 nikiwa Ihungo....kila j5 ilikuwa hii kitu na lazima ngumi zitokee hapo .....
 
Daaa...kweli nimekumbuka Tarime sec,shule kama jeshi..mwenye nguvu ndo anakula wazembe mtabaki kuona struggle 4 food pembeeni...bwaloni mkono kila siku,wanafunzi 80% wababe na kauzu mbaya,nawakumbuka wapishi wakongwe kama Mzee chris huyu anakupiga uparo(chakula kidogo) ukiomba akuongezee unasikia" karibu kesho"! Mama mariana,mwita na wengine wengi.MSOSI huo ilikuwa ijumaa yaani toka asubuhi unawaza utapateje msosi,so inawabidi kutengeneza team ya mapambano ili atleast kutoka na kitu. Nakumbuka sufuria likibebwa juu na uji,ugali,makande,wali,maharage linashuka chini tupu! Alafu hapo wanafunz wameungua vibaya,ni mwendo wa kuwakimbiza hospital. Mitaa ya buhemba,FDC na mazoez ndo ilikuwa mitaa ya wanajeshi wa tarime sec kujidai,mtaani wakurya wanatuogopa vibaya ukivaa t-shirt ya Tarime sec basi wewe mfalme kila unapopita ni kidole unanyooshewa,NAKUMBUKA form one yetu tuliteswa sana,tulipigwa sana,tulinyanyaswa sana na matokeo yake wanafunzi tukawa tunalala juu ya miti usiku kukwepa kipigo bwenini! Kuna mwezetu alipoteza maisha kwa kipigo,kweli mwanafunz wa tarime sec ni full mwanajesh ni kukosa gwanda tu.
Dah aisee poleni sana kwa life ya KIJESHI ya TARIME SEC na kuteswa kwenu form one aiseee....
Ila shule zote a ukanda ule ngoma ni nzito sana ..nakumbuka MARA secondary enzi hizo siku wakiwa na mechi na ALLIANCE(Musoma Tech) au mwembeni lazima kinuke...
Nasikia kuna kipindi Tarime Sec iliponea chupu chupu kupigwa moto na madenti kisa wamepikiwa ugali mchungu...
Dah kweli maisha ya shule safari ndefu
 
ahhhhh mzee wangu chale mpishi mkuu pale mkwawa high school...hahaaaa usinifanyie hivi bana
 
Kweli mkuu...maisha ya shule siri ya aliyeyapitia...na ukishakaa sana lazima kuna vijitabia utajifunza tuu hata kama hutaki..Kama kutojipenda penda na kuwa rough ni kawaida sana

Hapo kwenye red umegonga vijana wa Ifunda tech, kwa wale wastaarab walikua wanoga(Kunyaka) wekeend tu tena mchana, the rest ni full passport kwenda mbele.

Maswala ya chakula tulikuwa na mzee Meki, sema tulikosa makande ila wali twice a week. Wali mnaweka kwenye mfuko wa rambo kwa ajili ya nyuka (uji) na asubuhi lazima uanike juani ili kuondoa sisimizi, I miss those days.

Thanks mkuu.
 
Dah aisee poleni sana kwa life ya KIJESHI ya TARIME SEC na kuteswa kwenu form one aiseee....
Ila shule zote a ukanda ule ngoma ni nzito sana ..nakumbuka MARA secondary enzi hizo siku wakiwa na mechi na ALLIANCE(Musoma Tech) au mwembeni lazima kinuke...
Nasikia kuna kipindi Tarime Sec iliponea chupu chupu kupigwa moto na madenti kisa wamepikiwa ugali mchungu...
Dah kweli maisha ya shule safari ndefu

aisee Tarime sec ilikuwa kila mwezi wa nane lazima mgomo utokee na mwez huo ulijulikana kama mwez wa shetani! Ukifika pawe na shida au la,lazima mgomo utokee,kuna mgomo ambao sitausahau pale wanafunz walipompiga teacher,choma gari la shule,toboa vigae nyumba za walimu, bomoa duka la shule(bia,soda,nk ilikuwa zawadi), then nyumba ya headmaster ikapasuliwa mlango na yeye akashinikizwa kupasua tv yake kwa mikono yake mwenyewe,mzee wa watu alitetemeka akajikojolea mwisho akanyanyua tv yake na kuipiga chini! Maaskari (ffu)walikuja gari 4 waliambulia patupa baada ya wao kupigwa vibaya na gari kupasuliwa vioo,form one(nyumbu,nguruwe,nyoya) kazi yetu ilikuwa kukusanya mawe na kuwaletea wakubwa zetu.Mgomo ulidumu siku tatu,siku ya nne ffu magari zaid ya 20 (tarime+musoma) walitushinda baada ya kugeuza shule kuwa uwanja wa vita,tulikusanywa wanafunz wote,tukalala kifudifudi,mkuu wa mkoa akafunga shule kwa mda usiyojulikana na kupewa dk 3 tuwe tumepotea maeneo ya shule,KWELI sijui nilifauluje kwa njisi shule ilivyokuwa?!!! Na baada ya kujiunga kidato cha tano kweli nilikutana na maisha mapya ambayo sikuyazoea mfano kuchapwa,kwenda paredi,kupiga magoti,kukaguliwa usafi wa mwili na mabweni,kilanja kuwa na uwezo juu yako,kukaa darasani masaa yote,vipindi vya dini nk,bt nashukuru Mungu nilikuja kuwa the best baada ya kujua maana ya mwl,kiraja,dini nk
 
nakumbuka kuna washikaji walikuwa wanaitwa wadudu kwa jinsi ambavyo walikuwa wanafukia nguna
 
Nawakumbuka Mwakamomla, Mwakangata , Mwakatobe ,Njonjoma e.t.c, wadau wa from the bush wataipata.
 
Nilikosomea o-level hii kitu haikuwepo enzi zetu sijui siku hizi, ila niliikuta nilikosomea a-level.
 
Dah yamenikumbusha sana Kifungilo jamani... Alikuwa anayapika mbibi ukilogwa ukamwita bibi utamkoma... Anataka kuitwa dada hata kama umri wakuitwa dada umeisha.. tulikuwa tunayagombania achaga tu!
 
Back
Top Bottom