Taka za sumu

Hebu cheki hii link kwanza: http://www.bbc.co.uk/swahili/news/story/2004/06/000000_amkanabbc.shtml
Yaani inafikia hatua kukubali nchi zetu kufanywa jalala tena la taka za sumu? Tumetoka wapi, tuko wapi na tunakwenda wapi? hii si afrika jamani?
source bbc news

BBC News said:
Kipindi cha televisheni cha BBC Newsnight kimepata ushahidi ambao unathibitisha kwamba kampuni ya Trafigura ilifahamu vyema kwamba uchafu ilioutupa nchini Ivory Coast mwaka 2006 ulikuwa na sumu kali....

Mara nyingi nikuwa nahoji uzalendo wa hao wakuu (viongozi wetu), kwani huhitaji kuwa na digrii kufahamu kuwa taka za sumu zitawadhuru wananchi wako.

Vitu kama hivi ni kusubiri halafu nchi zilizoathirika zikipata viongozi wazuri kuanza kudai fidia nyingi sana.
 
Ivory Coast wakati huo kulikuwa na vaccum ya uongozi. Walikuwa wanatwangana wenyewe kwa wenyewe - na jamaa wakatumia mwanya huo kumwaga mataka yenye sumu.
 
Back
Top Bottom